mwakatojofu
JF-Expert Member
- Dec 17, 2008
- 326
- 227
August;
sababu za kushushwa kwenye treni zilikuwa zipi? kama sio huku kuwa wamepishana na mkapa .
kuhusu kuwa sabotage mtu yoyote awe kiongozi au si kiongozi mambo yako yanaweza kubezwa au kuharibia ikiwa serikali iliopo madarakani wasinge penda kuona maendeleo yako. sasa hapa ina tegemeana na nguvu zako za kiuchumi au za kisiasa. mangeneyo itajumlisha au kutoa mwenyewe.
kuhusu kugombana na wenzie hilo lipo, lakini linategemeana na chanzo chake, je ni kupinga ufisadi au la. na hao viongozi wenzie wako kwenye payroll yanani? ni viongozi fuata upepo au independent. sasa hapa inabidi utumie akili yako binafsi kufanya analysis.
kuhusu viongozi wa juu kumuona wa maana au la hilo ni lao wamuachie basi , then ashindwe kwenye mchujo badala ya Malecela etc kuweka kiwingu au blah blah nyingi za utamaduni usio utamaduni. au tuseme utamaduni wa kudumisha ufisadi na maslahi binafsi
FMES,
watu wengi na mara nyingi husema ndani ya ccm na serikali mambo mengi yako ovyo. wenyewe humo wako kimya. vyama vya upinzan na watu wa kawaida/chini kila siku tunapiga makelele lakin wapi! no changes!
akitokea msekwa akasema ni kweli tunavyoona sie tumzomee? akitokea kitine akisema kweli mle ndani mko ovyo kwa nin tumzomee? wakisema hivyo wanatuunga mkono. japo kwa muda. lakin inatuhakikishia kuwa hatuko wrong
wakipata wakitakacho wanatumwaga tena. kimya. wanakosa ujasiri
lakin tunakuwa tumeshajua kuwa tuko sahih tunachopigania kila siku. kwamba tunachopigania ni haki tupu. kwamba tunachosema si majungu. kwamba tunasema ukweli tupu. mojawapo ya faida za hali kama hii ni kuwa inatupa nguvu kuendelea na tukifanyacho. huenda pia inaweza kutusaidia kujua tusichokijua. 'inside job?' mtu wa ndani anapodefekt inasaidia sana 'adui'
hata makamba akimwagwa mwache aje na shutuma kwa ccm. atatupa dondoo kadhaa. halaf atatupwa ubalozini. halaf kimya tena
one day YES tutapata wapiganaji wa kweli
Quote: semilong
JAMANI MBONA LIPUMBA AMEKUA CHALLENGED, JE CUF INADEMOKRASIA KULIKO CCM?
Mi naona hii chorus ya makundi mbalimbali ya wanaCCM imekua orchestrated na watu wa karibu na JK under JK's directives. Na hii si kwa ajili ya Shibuda,...actually Shibuda ni mtani wa JK, ila ni kwa watu wengine wenye nguvu za wajumbe nyeti.
Panic ninayoiona ni JK kushindwa kuwasoma au kuwaamini fully baadhi ya his former wanamtandao ambao kimsingi ndio wamemuweka hapo, but still anajua uwezo wao wa kupenyeza watu kwenye kila kikao nyeti na kutilt maamuzi in their favour. Vilevile anajua
ni vipi hawa jamaa wanaweza kuyumbisha nchi ili isitawalike kama kutakua na rafu kubwa pindi kinyang'anyiro kikifika. Sababu, JK mwenyewe na wanamtandao wenzake waliweza kusuka mpango kama huo wa kutishia kuyumbisha nchi kama jina la JK lingekatwa 2005.
Tabu inakuja wapi?...Tabu inakuja pale mwanachama mwenye ushawishi kwa wajumbe(sio watanzania) atakapotia jina lake, maana yake itakua wakati wa kujadili majina ya wagombea JK itabidi naye atoke nje, na kumuachia kiti makamu mmojawapo, ambao ukiangaliza JK ni ngumu kuwaamini 100%. Kazi ya wapambe wa huyo mshindani JK akiwa nje itakua ni kuhakikisha jina la mpinzani wake halikatwi na badala yake majina yapelekwe NEC. Kadri wigo wa wanachama unavyozidi kupanuka ndio risk ya JK kuzungukwa na watu aliewaamini inaongezeka, . Baada ya NEC, kikao chenye mamlaka ya kupitisha jina la mgombea wa urais ni mkutano mkuu wa taifa ambao una wanachama zaidi ya 1000.
Kitu cha kufanya...Kinga ni bora kuliko tiba. What JK anachojaribu kufanya ni kuwapreempt wanachama ili kujenga dhana ya usaliti kwa yeyote atakayejaribu kumpinga... Na si ajabu ukasikia kamati ya maadili imemvua kiongozi fulani mzito uanachama kama alivyoashiria Mzee Cigwiyemisi, kama hawa jamaa wataonekana kweli wamempania. JK hana uhakika vikao vya Dubai ni mikakati ya dowans tu au vinampa a sense of nostalgia ya vikao vyao kama hivyo Johannesburg 2002-2005 wakati wakijipanga kuchukua nchi.
In the end, kumuondoa the incumbent president kwa Tanzania ni ngumu sana, almost impossible...kwa kampeni za kawaida kama za akina Mwandosya au SAS, lakini kwa mafia waliomuweka magogoni, huwezi kuwarule out 100%, maana harakati zao, JK anazijua vilivyo na how far they are ready to go. Ndio maana all this makelele....
[SIZE="4
- [B][SIZE="4"]Anyways kwa kumaliza tu ni kwamba leo nimewauliza viongozi wengi ndani ya CCM, kuhusu hizi kauli za Shibuda, wakasema kwamba wamemzoea na huko ndani ya CCM hakuna kiongozi mwenye akili timamua anayeweza kulumbana na Shibuda mbele ya public[/SIZE][/B], wengi wao wakasema kwamba kama haya maneno yake yangekua yametamkwa na angalau Mwandosya, wangeshituka sana, na kwamba Shibuda ana matatizo mengi sana kisiasa kwa sababu huko Shinyanga haelewani na hata makatibu kata licha ya viongozi wa juu, lakini wakakubali kwamba ni haki yake kusema maoni yake pia.
Respect.
FMES![/SIZE]
Mkuu haitakuwa vibaya kama ukitumegea ni viongozi gani ndani ya CCM ambao uliongea nao kuhusu Shibuda. Please remember that this is JF where we dare to talk openly
Thanks
Shibuda ametumwa kupima upepo na kigogo mmoja anayetaka kugombea. Kama ilivyokuwa kwa Sabi Munasa wakati wa Mkapa
.......ndiyohiyo
1.
- Hakushushwa kwenye treni, angeshushwaje na yeye alikuwa ni mjumbe wa uchaguzi? Shibuda alikuwa ni supporter wa Malecela kwenye ule uchaguzi, aliposikia kuwa kuna njama za kuondoa jina lake ndio akaanza makelele mengi toka akiwa ndani ya treni, ilipofika Dodoma Malecela mwenyewe alimtumia watu wake kumtaka aache makelele na fujo kabla ya kushuka, na yeye alikubali bila tatizo, kwa hiyo la kukataliwa kushuka ni zile zile za waandishi wetu, ambao wewe unawafahamu sana kuliko wengine wengi humu JF.
2.
- Hapa mkuu umeniacha nje kabisaaa!
3.
- Malecela amezungumzia utamaduni wa CCM, akiwa na maana kwamba toka awamu ya kwanza CCM haijawahi kua na tabia za kuwaondoa marais wake bila kumaliza term zao, lakini hakusema kwamba huu ni utamaduni wa taifa ila amesema ndani ya CCM, it has nothing to na taifa unless kama tumekata tamaa kwamba hakuna alternative, then maneno ya Malecela yanakuwa na nguvu, lakini binafsi sioni tatizo kwa wananchi waliojitayarisha na waliopania kuliletea mabadiliko taifa lao, how could mstaafu kama Malecela akaweza kuweka kiwingu kwa taifa, unless kuna something tunaficha hapa.
- Shibuda, lets say he is for real, sasa huko kwenye uchaguzi ndani ya CCM si anawahitaji viongozi wa mkoa wake zaidi kuliko wengine, kwa mazingara yetu ya kisasa atapita vipi mpaka kuwa mgombea kama hawezi kuelewana hata na viongozi wa mkoa wake? Hivi kweli unaaamini wanasiasa makini kama Mwandosya, anaweza kwenda kinyume na viongozi wa mkoa wake? Hizi temporary fame za kina Shibuda, haziwezi kutusaidia taifa zaidi tu ya kuwapa nafasi zaidi mafisadi kutuchezea, siwezi hata siku moja kuunga mkono michezo ya kitoto kama hii ya Shibuda, kiongozi serious anayetaka kugombea urais wetu, hawezi kwenda kutukanana na viongozi wa mkoa wake as of Shibuda na kutegemea kutusaidia taifa kwa sababu he is not!.
FMES
- Mkuu wewe unajua kwamba hili huwa halinisumbui sana la kuwasema ni nani inapobidi, lakini kwa sababu hawakutaka niwa-disclose siwezi unajua tunapoongea nao huwa tunawauliza mapema kama ni on the record,
- Kwa hiyo no itakuwa vibaya kwangu kwa sababu bado tunahitaji info zaidi as we go on na vita vya mabadiliko, si unajua kua wote tunapigania one thing lakini kwa mitizamo mingi tofauti ingawa mingi tunakubaliana, lakini mininge kama huu wa Shibuda ndipo tunapoachana njia panda kwa sababu binafsi ninamuona ni tatizo kwa the big picture, ingawa ni nzuri temporary.
- Lakini naomba nikuhakikishie kwamba kila siku ya Mungu ninaongea na viongozi wengi sana ndani na nje ya CCM, infact katika siku tatu zilizopita hapa ninapoishi nilikuwa na kiongozi mmoja mzito sana ambaye siwezi kabisa kumtaja, lakini pia Bwana Beno Malisa naye alikuwepo, wote wameondoka tayari..
FMES!
Mzee wa masifa hata Obama ni rafiki yako Du!
😡
any way , ni mapema mno kuazana kujadiliana hili jambo, maana anaweza asifike popote, kwenye hizo juhudi zake, tukawa tumepoteza nguvu zetu bure. tusubiri wakati muafaka si sote tutakuwa na kitu cha kujadili na nina shukuru kwa mawazo yako
mkuu kwa dataz za ccm nakuaminia sana mkuu.tatizo masifasifa yako tu..
Na sisi Tanzania tunasikia vilio vya nchi kuyumba, nchi imetekwa na mafisadi, uchumi wetu uko mikononi mwa wageni. Hizi ni dalili tosha za kuonyesha vilio hivi ni kutokana na wananchi walio wengi kutoridhika na uongozi ulio madarakani ndiyo maana vinazidi kuongezeka kila kukicha. When you failed to deliver your promises, you should be kicked out of office. IT IS TIME FOR CHANGE, CHANGE THAT WE NEED FOR OUR BELOVED COUNTRY.
- Ni muhimu sana kusema maoni yetu mapema, maana tukinyamaza ni hasara zaidi.
FMES!
bak hapo umesema ukweli kabisa. Hakuna haja ya kutafuta excuse kwa kuwa na viongozi ambao wanashindwa kudeliver. Amepewa miaka 5 ameshindwa kujustify kwa nini apewe mingine 5 basi na aondoke. Na hapa jf ndiyo mahali pakuwatia shime wale ambao watakuwa na uwezo wa kuongoza. Siyo watu wa mitandao, makundi na kukosa ujasiri wa kufanya maamuzi magumu.
Hivyo basi ningependa tupige kura ya maoni humu jf kila wiki kuonyesha watu wangapi wangependa jmk aendelee kipindi cha pili.
Je, ungependa jmk agombee kipindi cha pili
ndiyo________ hapana
mimi naanza na hapana hivyo hadi sasa ndiyo (0) na hapana (1)