Shetani hana Rafiki, Antony Mtaka akiona cha moto

Shetani hana Rafiki, Antony Mtaka akiona cha moto

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
141,449
Reaction score
283,755
Taarifa Kamili hii hapa

Screenshot_20260707-200259~2.png
Screenshot_20260707-200323~2.png


TOA MAONI YAKO
 
Uchakachuaji na upindishaji matokeo upo kwenye DNA yao, haishangazi tena hata kura za maoni ndani ya chama kile cha kutegemea mitutu na dola uchaguzi wa wagombea kulikuwa kuna kupindisha matokeo wale wasiopata kura za kutosha wanapitishwa tu kwasababu mkuu kasema, maelekezo kutoka juu
 
Mleta mada umekuja kuleta hii taarifa kama wote tunafuatilia haya mambo. Eleza kinaganaga hiyo TOC ni nini inasimamia kitu gani, na maslahi gani kwa umma. Pia utueleze huyo Mtaka na Thadeo ni akina nani?
TOC - Tanzania Olympic Committee - Kamati ya Olimpiki Tanzania

Hii ni taasisi kuu inayohusika na mambo yafuatayo:

  • Kusimamia Michezo ya Olimpiki: Ndio chombo chenye mamlaka ya kuandaa, kuratibu, na kupeleka timu za Tanzania (wanamichezo wa hapa nchini) kwenye Michezo ya Olimpiki (Olympic Games) na michezo mingine mikubwa ya kimataifa kama Commonwealth Games (Michezo ya Jumuiya ya Madola).
  • Kukuza Vipaji vya Michezo: Wanajishughulisha na kuendeleza michezo mbalimbali nchini (kama riadha, ngumi, kuogelea, n.k.) kwa kushirikiana na vyama vya michezo husika, ili kupata vijana wenye viwango vya kushindana kimataifa.
  • Kupata Ufadhili na Udhamini: Wanasaidia wachezaji kupata "scholarships" (ufadhili wa mafunzo) na kambi za mazoezi ndani na nje ya nchi ili wajiandae vizuri kabla ya mashindano makubwa.

Thadeo ni rais mpya wa TOC.
 
Mkuu wa mkoa majukumu yake amemaliza hadi akaongeze hayo ya TOC. Naona uamuzi ulifanyika kwa maslahi mapana ya wananjombe.
 
Nilidhani band ya muziki ya CCM (TOT) imefanya uchaguzi.

Uzuri wa huko,huyo aliyedhulmiwa hawezi hata kujitokeza hadharani kupinga au hata kulaani.😀
 
Back
Top Bottom