Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
[h=1][/h]Posted on June 11, 2012 by zanzibaryetu
Katibu wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Yahya Khamis Hamad
SHERIA ya mabadiliko ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itawasilishwa kesho katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoanza kujadili bajeti ya mwaka wa fedha serikali ya mwaka wa fedha wa 2012/2013. Katibu wa baraza hilo, Yahya Khamis Hamad aliwaambiwa waandishi wa habari jana katika mkutano uliofanyika ukumbi wa baraza la wawakilishi, kwamba jambo la kwanza kuwasilishwa kwa wajumbe wa baraza ni sheria hiyo ambayo wananchi wanasubiri kuitolea maoni.
Hii itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi ambayo ni kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar kifungu 132 (2) ambayo inahitaji sheria zinazohusu muungano kuwasilishwa katika baraza alisema Hamad.
Hamad alisema katiba haitoi nafasi ya kujadili sheria hiyo kwani itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza na sio kuijadili, Hii ni kwa mujibu wa katiba lakini tusibiri litakaloweza kutokea baada ya kuwasilishwa sheria hiyo kwa sasa hatuwezi kujua nini kitatokea.
Katibu Hamad alisema sheria hiyo inawasilishwa katika baraza la wawakilishi katika kikao cha kesho kwa sababu ndicho kikao cha kwanza tangu bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitisha sheria hiyo.
Waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar Abubakar Khamis Bakari atatoa taarifa kuhusu sheria hiyo alisema Katibu huyo.
Akijibu suali la waandishi juu ya kuchelewa kwa kuwasilishwa sheria hiyo kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi, Katibu huyo alisema Bado hatujachelewa kuwapa wajumbe taarifa kwa sababu hiki ndio kikao cha kwanza aliongeza Hamad.
Tangu kupitishwa na bunge sheria hiyo na kusaniwa na Rais Jakaya Kikwete ilitarajiwa tume ya katiba ingeanza kazi zake ya kukusanya maoni ya katiba mpya mwezi huu, hata hivyo kikwazo kikawa ni kutowasilishwa katika kikao cha baraza la wawakilishi kama gazeti hili lilipoandika hivi karibuni.
Akizungumzia utaratibu wa kikao hicho ambacho ni bajeti ya pili tangu kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa. Katibu alisema hakuna mswada mwengine utakaowasilishwa isipokuwa miswada ya kuidhinisha matumizi ya fedha za serikali.
Alisema jumla ya masuali 197 yataulizwa na kupatiwa majibu na mawaziri wahusika ambapo tayari tayari matayarisho ya kikao hicho yameshakamilika ikiwemo wajumbe wote waliopo kisiwani Pemba kuwasili hapa Unguja.
Tokea kuapishwa kwa wajumbe wa tume ya katiba Rais Kikwete wananchi wa Zanzibar wamekuwa na maoni tofauti kuhusiana na suala la kuwasilishwa sheria hiyo ya katiba katika kikao cha baraza la wawakilishi.
Wazanzibari wengi wamekuwa na shauku kubwa wakitaka kujua kitakachotokea katika baraza hilo juu ya sheria ya katiba itakayowasilishwa na waziri wa katiba na sheria.
Katibu wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Yahya Khamis Hamad
SHERIA ya mabadiliko ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itawasilishwa kesho katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoanza kujadili bajeti ya mwaka wa fedha serikali ya mwaka wa fedha wa 2012/2013. Katibu wa baraza hilo, Yahya Khamis Hamad aliwaambiwa waandishi wa habari jana katika mkutano uliofanyika ukumbi wa baraza la wawakilishi, kwamba jambo la kwanza kuwasilishwa kwa wajumbe wa baraza ni sheria hiyo ambayo wananchi wanasubiri kuitolea maoni.
Hii itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi ambayo ni kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar kifungu 132 (2) ambayo inahitaji sheria zinazohusu muungano kuwasilishwa katika baraza alisema Hamad.
Hamad alisema katiba haitoi nafasi ya kujadili sheria hiyo kwani itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza na sio kuijadili, Hii ni kwa mujibu wa katiba lakini tusibiri litakaloweza kutokea baada ya kuwasilishwa sheria hiyo kwa sasa hatuwezi kujua nini kitatokea.
Katibu Hamad alisema sheria hiyo inawasilishwa katika baraza la wawakilishi katika kikao cha kesho kwa sababu ndicho kikao cha kwanza tangu bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitisha sheria hiyo.
Waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar Abubakar Khamis Bakari atatoa taarifa kuhusu sheria hiyo alisema Katibu huyo.
Akijibu suali la waandishi juu ya kuchelewa kwa kuwasilishwa sheria hiyo kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi, Katibu huyo alisema Bado hatujachelewa kuwapa wajumbe taarifa kwa sababu hiki ndio kikao cha kwanza aliongeza Hamad.
Tangu kupitishwa na bunge sheria hiyo na kusaniwa na Rais Jakaya Kikwete ilitarajiwa tume ya katiba ingeanza kazi zake ya kukusanya maoni ya katiba mpya mwezi huu, hata hivyo kikwazo kikawa ni kutowasilishwa katika kikao cha baraza la wawakilishi kama gazeti hili lilipoandika hivi karibuni.
Akizungumzia utaratibu wa kikao hicho ambacho ni bajeti ya pili tangu kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa. Katibu alisema hakuna mswada mwengine utakaowasilishwa isipokuwa miswada ya kuidhinisha matumizi ya fedha za serikali.
Alisema jumla ya masuali 197 yataulizwa na kupatiwa majibu na mawaziri wahusika ambapo tayari tayari matayarisho ya kikao hicho yameshakamilika ikiwemo wajumbe wote waliopo kisiwani Pemba kuwasili hapa Unguja.
Tokea kuapishwa kwa wajumbe wa tume ya katiba Rais Kikwete wananchi wa Zanzibar wamekuwa na maoni tofauti kuhusiana na suala la kuwasilishwa sheria hiyo ya katiba katika kikao cha baraza la wawakilishi.
Wazanzibari wengi wamekuwa na shauku kubwa wakitaka kujua kitakachotokea katika baraza hilo juu ya sheria ya katiba itakayowasilishwa na waziri wa katiba na sheria.