Sheria No.7 ya soka: Muda wa mchezo

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,498
37,792
Muda wa kawaida wa mchezo umetajwa katika sheria za FIFA kuwa ni dakika 90. Sheria No.7 Kati ya sheria 17 za soka imeelezea vema Muda wa mchezo.

Kanuni zinazotumika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia huko Qatar kuhusu Muda wa mchezo zimekuja kuondoa Tabia ya makipa na Wachezaji kujilaza chini bila sababu Kwa Muda mrefu kisha Muda huo kutofidiwa kikamilifu na hivyo kufanya baadhi ya Mechi zichezwe Kwa dakika 80 badala ya 90 huku Muda mrefu ukipotezwa na wachezaji hususan Makipa. Kanuni hii ikitumika kwenye ligi ya NBC itawasaidia Metacha Mnata wa SBS na Dida wa Namungo kubadilika na kuacha mpira utembee badala ya kujilazalaza.

Kombe la Dunia ukilala wewe lala lakini ujue Hakuna dakika itakayopotea bure. Refa ataongeza dakika zote ulizopoteza. Tangu Mechi ya ufunguzi Jana Kati ya mwenyeji Qatar na Ecuador, na ya Leo Kati ya England na Iran dakika zingionhezwa chache ni 5.

Leo England Vs Iran kipindi cha Kwanza zimeongezwa dakika 14 na kipindi cha pili zimeongezwa dakika 10. Yaani dakika za nyongeza Kwa Mechi nzima ni 24 ambazo ni zaidi ya nusu ya kipindi kimoja.

Hii ndo komesha ya wapoteza Muda Kwa makusudi.
 
Muda wa kawaida wa mchezo umetajwa katika sheria za FIFA kuwa ni dakika 90. Sheria No.7 Kati ya sheria 17 za soka imeelezea vema Muda wa mchezo.
Kanuni zinazotumika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia huko Qatar kuhusu Muda wa mchezo zimekuja kuondoa Tabia ya kipindi kimoja.
Hii ndo komesha ya wapoteza Muda Kwa makusudi.
Refa hutumia stopwatch hivyo yeye huhesabu sekunde kila mechi isimamapo na kuzijumlisha mpaka zitimie dakika tisini.
 
Okay somo zuri, kumbe hii ni sheria iliyokuja baada ya hii michuano ya kombe la dunia
 
Okay somo zuri, kumbe hii ni sheria iliyokuja baada ya hii michuano ya kombe la dunia
Hakuna niliposema imekuja baada ya Kombe la Dunia. Sheria yoyote duniani ili itekelezwe hulazimika kutungiwa kanuni. Kanuni za safari hii ziko tofauti na miaka mingine, mpira ukitoka nje stop watch inabonyezwa mpaka utakaporusha lakini zamani haikuwa hivyo. Ndo maana Mechi ya Holland Vs Senegal hujaona tukio la kusimama mchezo Kwa Muda mrefu lakini zimeongezwa DK8.
 
Sasa ikitokea katika zile alizoongeza halafu wakawa wanazipoteza, zitafidiwaje?
Kama umeangalia mechi ya USA vs Wales zimeongezwa dk 9 lakini mchezaji wa Wales alipoumia dk 5 refa ameonyesha saa yake kwamba anasimamisha muda akiendelea kulala.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom