SnowBall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2011
- 3,054
- 2,840
Baada ya mihangaiko na shughuli nyingi za Jiji letu hili niliamua kujipumzisha sehemu moja ili nivute muda kabla ya kurejea nyumbani. Actually ni sehemu ambayo upande mmoja kuna TV kubwa na kwa sababu kulikuwa na mpira sikutaka kukaa sehemu ambayo kuna kelele nyingi kwa sababu mie sio mpenzi sana wa mpira.Hivyo nillingia ndani zaidi kwenye utulivu!
Nilitafuta meza ambayo jirani yake kulikuwa na watu kama wa3 hivi na kwa sababu kulikuwa na kigizagiza sikuwatambua wahusika kwa haraka. Mhudumu alikuja na nikamuagiza ninachohitaji na wakati huo nilikuwa nabrowse hapa JF na kwa mbali niliona charge ya simu yangu ilikuwa karibu kwisha. So niliweka simu pembeni na kuanza kunywa kinywaji changu. Wakati napepesa macho vizuri kumbe wale waliokaa jirani kulikuwa na shemeji yangu (mke wa Rafiki yangu) tunayeheshimiana sana. Aliniona na alikuja kunisalimia na kisha kunieleza kuwa alikuja na rafikie ambaye pia alikuja na mpenzi wake (kulikuwa na mkaka kati yao)..hivyo walikuja kupata kinywaji kidogo na yeye alikuwa kamsindikiza shogaake.
Sikujali sana na nilienda kuwasalimia kwa pamoja. Sikukaa sana na nikaondoka nyumbani. Kwa kuwa simu yangu ilikuwa imeisha charge nilicharge na nikalala. Asubuhi wakati nafungua simu yangu nimekutana na message hii 'Samahani sana shemeji yangu naomba katu usimwambie rafiki yako kama tumekutana leo hapa..'. Ilikuwa ni message ya shemeji na inaonekana aliituma jana hiyohyo sikuisoma kwa sababu simu yangu ilikuwa imeisha charge.
Nimebaki najiuliza mchezo anaotaka kuniletea shemeji yangu!!..hasa nikizingatia kuwa alinitambulisha kuwa alimsindikiza rafikie kwa mtuwake...sasa iweje anipige mkwara??..Nimempigia simu rafiki yangu na ameniambia hayupo mjini kwa takribani siku tatu sasa na sijamueleza chochote..Hapa nilipo sijaijibu meseji na sijampigia simu shemeji kumuuliza chochote!!..Nimepanga nimyamaze kama meseji inavyosema but naona kama sitamtendea haki rafiki yangu..Lakini pia naogopa kama nita'expose' hii habari kwa rafiki yangu na kukawa na tatizo..nahisi nitakuwa..' more guilty'..Lakini kama alikuwepo m2 mwingine (kumbuka kulikuwa na watu wanangalia mpira) akaona na akasema kwa rafiki angu naona bado shemeji atajua mimi ndiye niliyemwambia mumewe..So,hapa nilipo i am really confused naona kama 'shemeji kaniuzia kesi bila kujijua'..
Hebu wadau nisaidieni ili niiweze kuihandle hii issue b4 haijawa tatizo kwangu!!!
Nilitafuta meza ambayo jirani yake kulikuwa na watu kama wa3 hivi na kwa sababu kulikuwa na kigizagiza sikuwatambua wahusika kwa haraka. Mhudumu alikuja na nikamuagiza ninachohitaji na wakati huo nilikuwa nabrowse hapa JF na kwa mbali niliona charge ya simu yangu ilikuwa karibu kwisha. So niliweka simu pembeni na kuanza kunywa kinywaji changu. Wakati napepesa macho vizuri kumbe wale waliokaa jirani kulikuwa na shemeji yangu (mke wa Rafiki yangu) tunayeheshimiana sana. Aliniona na alikuja kunisalimia na kisha kunieleza kuwa alikuja na rafikie ambaye pia alikuja na mpenzi wake (kulikuwa na mkaka kati yao)..hivyo walikuja kupata kinywaji kidogo na yeye alikuwa kamsindikiza shogaake.
Sikujali sana na nilienda kuwasalimia kwa pamoja. Sikukaa sana na nikaondoka nyumbani. Kwa kuwa simu yangu ilikuwa imeisha charge nilicharge na nikalala. Asubuhi wakati nafungua simu yangu nimekutana na message hii 'Samahani sana shemeji yangu naomba katu usimwambie rafiki yako kama tumekutana leo hapa..'. Ilikuwa ni message ya shemeji na inaonekana aliituma jana hiyohyo sikuisoma kwa sababu simu yangu ilikuwa imeisha charge.
Nimebaki najiuliza mchezo anaotaka kuniletea shemeji yangu!!..hasa nikizingatia kuwa alinitambulisha kuwa alimsindikiza rafikie kwa mtuwake...sasa iweje anipige mkwara??..Nimempigia simu rafiki yangu na ameniambia hayupo mjini kwa takribani siku tatu sasa na sijamueleza chochote..Hapa nilipo sijaijibu meseji na sijampigia simu shemeji kumuuliza chochote!!..Nimepanga nimyamaze kama meseji inavyosema but naona kama sitamtendea haki rafiki yangu..Lakini pia naogopa kama nita'expose' hii habari kwa rafiki yangu na kukawa na tatizo..nahisi nitakuwa..' more guilty'..Lakini kama alikuwepo m2 mwingine (kumbuka kulikuwa na watu wanangalia mpira) akaona na akasema kwa rafiki angu naona bado shemeji atajua mimi ndiye niliyemwambia mumewe..So,hapa nilipo i am really confused naona kama 'shemeji kaniuzia kesi bila kujijua'..
Hebu wadau nisaidieni ili niiweze kuihandle hii issue b4 haijawa tatizo kwangu!!!