McLaren
JF-Expert Member
- Feb 19, 2025
- 889
- 2,863
Wakuu,
Akizungumza katika kongamano la viongozi wa dini ya kiislamu leo, Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke amesema kuwa Waislamu mkoani Mwanza wameamua kujitokeza kwa wingi kusikiliza sera za wagombea na hatimaye kupiga kura kwa amani na utulivu ifikapo Oktoba 29, mwaka huu ili kulinda tunu ya amani iliyopo nchini.
Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
"Tunataka amani ya nchi hatuna sehemu nyingine ya kwenda, kwa sababu hapa ndipo penye amani ni wajibu wetu kuipigania nchi hii. Tunafanya dua mara kwa mara kuliombea Taifa, na siku ya uchaguzi hakuna atakayebaki ndani wote tutajitokeza kwa wingi kupiga kura,” amesema Sheikh Kabeke.
Akizungumza katika kongamano la viongozi wa dini ya kiislamu leo, Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke amesema kuwa Waislamu mkoani Mwanza wameamua kujitokeza kwa wingi kusikiliza sera za wagombea na hatimaye kupiga kura kwa amani na utulivu ifikapo Oktoba 29, mwaka huu ili kulinda tunu ya amani iliyopo nchini.
Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
"Tunataka amani ya nchi hatuna sehemu nyingine ya kwenda, kwa sababu hapa ndipo penye amani ni wajibu wetu kuipigania nchi hii. Tunafanya dua mara kwa mara kuliombea Taifa, na siku ya uchaguzi hakuna atakayebaki ndani wote tutajitokeza kwa wingi kupiga kura,” amesema Sheikh Kabeke.