Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,074
- 30,424
- Thread starter
-
- #121
Ralph...Hiyo hatua iliyochukuliwa dhidi ya huyo Municipal Education officer ni sahihi, na inapaswa wengine wote waliobainika kutenda mambo yanayoashiria ubaguzi wachukuliwe hatua. Mimi bado naona kuwa mengi ya matendo haya yalifanywa kwa utashi binafsi wa mtendaji, sio kwa kufuata maelekezo ya taasisi au mfumo wowote rasmi, hivyo ni bora kila case ikashughulikiwa binafsi. Na zikishashughulikiwa nyingi hivyo, hata mwingine anayetaka kufanya hivyo atasita.
Hili nalichukulia kama ubaguzi ninaouona nchi za Marekani na Ulaya dhidi ya watu weusi na wasiokuwa wazungu. Sera iko wazi kuwa ubaguzi ni kinyume cha sheria, lakini bado wapo wanaobagua hadi leo. Na dhambi nyingine zote ni hivyohivyo.
Nyiokunda,Hii dini ina inferiority complex nashukuru sipo huko
Duh!!!Uongo siyo Mzuri hata kidogo Ndugu yangu................mimi ni mwenye asili ya Kilwa na nimesomea huko shule ya msingi......Mzazi wangu ''Mungu ampunguzie Adhabu za Kabri'' Alinibadilisha Jina na kunipa jina la KIBANTU ili kuficha UISLAM wetu na hatimae nilipofika form 6 nilikuwa tunafuga Nguruwe.......yote hiyo ni kutaka kujua Mtu ana DINI gani........!!!!????? nimeshika mpaka Chetezo la Ubani KANISANI siku ya misa kama Mtoto wa kanisa la RC............!!!
.. lakini Mwalimu wa sheikh Mataka alimwambia japo anauwezo mkubwa HATOCHAGULIWA.... alijua kuwa kwa sababu ya Uislamu wake HAWATOMCHAGUA.mi nataka kumwambia anajua kuwa darasa la saba unachaguliwa, maana yake ni kuwa kama mmefaulu 100 na nafasi zipo 50 then unapita mstari pale kwenye watu 50 tu, ikitokea second selection then wale waliobak wanachukulia.
na nahis wanapanga aidha kwa alphabet au ufaulu. so kama ufaulu kwa mfano ni kuanzia 70% basi kama hao waliopata 70% wako 60 na nafasi ni 50 maana yake kuna kumi watabaki hawajachaguliwa ila wamefaulu ndo maana kulikuwa na shida ya waliofaulu kukosa nafas sababu uhitaj mkubwa kuliko shule zilizopo... zikipatikana bas inatokea second selection
so kama analalamika hakuchaguliwa inawezekana kuwa mstari ulipita katika idad ya waliohitajika na yeye hakuwemo.. kuhusu huyo mwalimu wake kumwambia haweza faulu sababu ya dini, may be it was just coincidence kuwa maneno yake yameakis kilichotokea
hayo ni mawazo yangu, nakaribisha kusahihishwa
Watoto wanasoma shuleni lakini kitaa/nyumbani, au kwingineko wanaambiwa mengine..Bahati mbaya historia zako hazitumiki mahali popote palipo rasmi (official). Historia rasmi inayotumika na inayofundishwa ni ya Mwalimu Nyerere (Mkristu Mkatoliki) kuongoza harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika, hao wengine wala huwa hawauliziwi
Huyu naona HAJUI hata harakati za waislam nchini.Kuna jamaa zangu mara nyingi husema wewe gudume si muislamu.. utakuwa mkristo au kafiri. mimi huwakubalia kwa kuwa ni mtizamo wao. kumekuwa na tatizo la waumini wa dini flani, watu wa kabila flani au asili flan(hasa sisi waafrika weusi) kuwa walalamishi. hii ni ishara ya udhaifu mkubwa sana. mimi nilikuwa nakuwa wa pili au watatu mitihani yote kuanzia darasa la 4 mpaka la saba. matokeo yalipokuja kutoka sikufanikiwa kuendelea kusoma kidato cha kwanza shule za serikali. na si mimi tu walikuwepo jamaa wengine wawili pia walikumbwa na mkasa huo. kila mwanafunzi alishangazwa na jambo hilo. sana.
Bahati nzuri mbaya zaidi aliyekuwa wa kwanza kwa mitihani mingi pale shuleni alikuwa ni dini ya kikristo.huyu jamaa naye alikosa nafasi ya kuingia kidato cha kwanza. huyu alikuwa ni "kichwa" hasa... nami ambaye nilikuwa nashika nafasi ya pili ya tatu nilikumbwa na hilo. sikunyong'onyea. nikaenda jiunga shule ya sekondari binafsi. leo hii nina Degree Mbili na wala sikuwah kulia lia... haya mambo hayahusiani na dini sema kama tumeshajiona wanyonge na watu wa kulia lia kila siku tunaonesha udhaifu na hii hali itasababisha sasa watu watuoneee kweli kweli maana tumeshatangaza udhaifu.
Waislam tuna shule gani ambazo tulianzisha ukilinganisha na wakristo? nyerere kama asinge taifisha shule nadhani kwa sasa hali yetu ingekuwa mbaya zaidi. tuangalie tu shule nyingi zinazofanya vizuri zinamilikiwa na akina nani? mbona kuna shule zinamilikiwa na wakristo na wanaofanya vizuri waislamu wapo? mbona huu ulalamishi wa kitoto unafikia hatua unatudhalilisha sasa. ustaadhi wangu kupata tu masters kaja kutangaza hapa katafuta sababu ya kutangazia kudai alikoseshwa kusoma na wakristo wakati wapo waislamu kadhaa wengi wamesoma shule za kikristo. mimi nimesoma shule ya mission ilikuwa wakichinja nguruwe wanapika jiko lingine ili kwa waislamu na wasabato wasibughudhiwe.. hi shule ilikuwa inaongozwa na maburuda. na aliyekuwa kaka mkuu wa shule alikuwa muislamu .ijumaa madarasa yalikuwa yanaisha saa tano na nusu. jamani kwa nini tunakuwa hivi?
Ni bora kuwa na dini yetu waafrika maana hizi dini zilizoletwa kwetu zimetujengea hali ya kuwa inferior sana. mimi ukiniita kafiri sawa. ukiniita mkristo sawa ukiiniita muislamu nisiye ujua uislamu tutaelimishana kama ni biblia au quran. ila huwa sikubaliani na upuuzi ,unafiki na mioyo dhaifu.
HUU NI UONGO MWEUPE... KWA VYOVYOTE VILE WAZEE WALITAKA WATOTO WAO WASOME ILA WASIALIBIWE IMANI ZAO.Dah! Pole mkuu! Lakini bado nadhani hakukuwa na ulazima wa kujishikisha vitu unavyoamini ni vya haramu. Waislamu wamesoma shule za kikristo tangu kabla ya ukoloni na hawakulazimishwa kubadili dini (naamini kwa kiasi fulani walishawishiwa, lakini siyo kulazimishwa). Nina wazee mtaani hapa wamesoma St Francis College Pugu ya zamani, na ni waislamu tangu zamani hadi leo. Cha ukweli kabisa ambacho hata wazee wangu mtaani wananiambia ni kwamba wazazi wao walikuwa hawapendi huo ushawishi, hasa ukizingatia kuwa wanaoshawishiwa ni watoto. Kupambana na hali hiyo, wazee wao walikuwa wanahakikisha mtoto amepata elimu ya kutosha ya madrasa ya kiislamu kabla hajajiunga shule hizo ili kumuongezea uimara wa kutoshawishika. Nina marafiki na majirani waislamu ambao watoto wao wanasoma shule za English medium za kikristo, wananiambia wanahakikisha kila siku mtoto akitoka shule jioni lazima aingie chuo apate maarifa ya kiislamu ili asiyumbe (japo nina uhakika shule za kikristo za siku hizi huwa hawashawishi mtu yeyote kubadili dini).
Nadhani ni utaratibu mzuri kujitahidi kuhakikisha mwanao anafuata misingi bora ya dini yako, si tu kujikinga dhidi ya ushawishi wa watu wa dini nyingine, bali zaidi kujikinga dhidi ya maovu. Maovu hayana dini. Waovu wote hawafuati dini zao (ndio maana wanafanya maovu), kwa hiyo tunapaswa kupambana na maovu hata au niseme hasa yanapotendwa na walewale wanaojinasibu kuwa ni waumini wenzetu wa dini tunazofuata.
HIZI NI PROPAGANDA ZA WAMISHONARI KUWA WALIKOMBOA WATUMWA ZANZIBAR..Hapana, hii ya jaji na wakristo wengine hasa waanglikana wa Zanzibar ni tofauti sana. Hawa babu wa babu zao waligombolewa pale soko la watumwa kwa kununuliwa na wamishenari kutoka kwa waarabu waliokuwa wanauza watumwa. Wengine waliachiwa huru utumwani wakatunzwa na kusaidiwa na hao wamishenari, ndipo walipobatizwa lakini wakatunza pia na majina yao ya awali.
Niwakumbushe tu kuwa majina mengi ya watumwa hayakuwa majina yao halisi, walipewa tu na slavemasters kama sisi wengine tunavyowapa ng'ombe wetu majina. Asilimia kubwa ya hawa watumwa hawakuwa na hizi dini za kigeni walipokamatwa. Walikuwa na majina yao ya kiyao, kinyamwezi, kimakonde nk, lakini mabosi waliamua kuwapa majina ambayo ni rahisi kwao mabosi kukumbuka, wakawakatia tu majina Ali, Juma, Omari, almuradi majina rahisi. Hata hao wamarekani weusi mnaosikia wana majina ya kizungu, hayo hayakuwa majina yao, walikatiwa majina na wazungu kwa sababu wazungu walishindwa kutamka majina ya kibantu na pia wangeshindwa kuyakumbuka. Surnames nyingi za black Americans ni majina ya owners wao au ya mitaa au mashamba au biashara walikotumika (utasikia watu weusi wanaitwa Baker, Tailor, Rivers, Mason, Blackwell etc)
KWANI ULIAMBIWA FISADI HUIBA HELA YOTE KWA MKUPUO???Hii habari ya namba ni uongo mtupu. Nimefanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1981, tulitumia namba siyo majina. Waziri wa Elimu wakati huo alikuwa Mama Tabitha Siwale kama sijasahau. Nilifanya mtihani wa form four mwaka 1985, waziri wa elimu alikuwa Jackson Makweta, na tulitumia namba za mitihani, siyo majina. Cheti changu cha Form 4 kimesainiwa na A. Modesti na N.A. Kuhanga. Kighoma Malima alikuja kuwa waziri wa elimu baadae, na wala siye aliyeasisi mfumo wa namba za mtihani.
KWANI NINI???....Hii habari ya namba ni uongo mtupu. Nimefanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1981, tulitumia namba siyo majina. Waziri wa Elimu wakati huo alikuwa Mama Tabitha Siwale kama sijasahau. Nilifanya mtihani wa form four mwaka 1985, waziri wa elimu alikuwa Jackson Makweta, na tulitumia namba za mitihani, siyo majina. Cheti changu cha Form 4 kimesainiwa na A. Modesti na N.A. Kuhanga. Kighoma Malima alikuja kuwa waziri wa elimu baadae, na wala siye aliyeasisi mfumo wa namba za mtihani.
UMEPOTEA WEWE.. UNADHANI MIMI NNA INFERIOLITY COMPLEX.. NA VIPI DR. MOHAMED SAID???Hii dini ina inferiority complex nashukuru sipo huko
Tatizo mnalalamika sana ,mngekuwa kama Gugume mngekuwa poa.Ebu sasa Kazeni buti kielimu.Tunaokaa wilaya ya Temeke tunaona udhaifu mkubwa toka level ya familia hadi kaya.Badilikeni ulalamishi hauleti ufumbuzi.Mshike elimu asiende zake.
Nyiokunda,
Uislam ungekuwa una hiyo ''complex,'' uhuru wa Tanganyika ungechelewa sana.
Soma historia ya Tanganyika uangalie ni watu gani walipambana na Wajerumani
kwa silaha na Waingereza kwa mbinu za siasa.
Unaijua historia ya Kleist Sykes katika African Association (1929 - 1949) au ya
mtoto wake Abdulwahid Sykes katika TAA/TANU (1950 - 1961)?
Umesoma historia ya Hassan Suleiman na Ali Juma Ponda (1945 - 1955)?
Unaijua historia ya Abdulrauf Songea Mbano katika Vita Vya Maji Maji 1905 - 1907)?
Unaijua historia ya Sheikh Hassan bin Ameir katika siasa za kupigania uhuru
(1940 - 1961) na baada ya uhuru akaweka jiwe la msingi kujenga Chuo Kikuu
mwaka wa 1968?
Unaijua historia Sheikh Yusuf Badi wa Lindi katika kupambana na propaganda za
Kanisa Southern Province lilipokuwa linawatisha waumini wake wasijiunge na TANU
kupigania uhuru?
Unaijua historia ya Bi. Sharifa bint Mzee?
Uaijua historia ya Salum Mpunga na Yusuf Chembera?
Ushamsikia Haruna Taratibu katika historia ya uhuru wa Tanganyika?
Nani mwenye ''mentality,'' ya kukubali ''inferiority?''
Hakika si hao niliokutajia na wako wengi sikuwataja wake kwa waume.
Je unawajua hao hapo chini ni akina nani na ulikuwa mwaka gani na walikuwa wapi
na nini kilikuwa kinawahangaisha wapo steshehi ya treni Dodoma.
Unajuwa walikuwa wanakwenda wapi na kutafuta nini?
Au kwa kuwa historia yao imefutwa ndiyo unadhani unaweza ukaja hapa na kejeli?:
Kushoto ni Idd Faiz Mafungo, Sheikh Mohamed Ramia, Baba
wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Abdu Kandoro na Haruna
Taratibu 1955.
Madrid...QUOTE="Madrid boy, post: 26215387, member: 434686"]Mo mimi mwenyewe baba yangu ni mkristo jina lake lilikatwa akapewa mtu mwingine tunaliwekaje hilo kwenye historia
Hiyo kitu cha kawaida ,kila zama zina muda wake .UMEPOTEA WEWE.. UNADHANI MIMI NNA INFERIOLITY COMPLEX.. NA VIPI DR. MOHAMED SAID???
MWENZIO KAFANYA UTAFITI.. NA UZURI HAKUNA ALOJITOJEZA HADHARANI KUMPINGA.
WAISLAM WANGEKUWA NA INFERIOLITY COMPLEX WANGETAWALA SPAIN MIAKA 700,AU KUITAWALA NUSU ULAYA???
mwaka gani?Astaghfirullah! Ulianza darasa la kwanza ukiwa na umri wa miaka 11 tena jijini Dar es Salaam! Nikiwa na umri wa miaka 11 nilikuwa niko darasa la 6 tena kijijini! Ngoja nikae kimya.
SASA NDO ZAMA ZA UISLAM KUWA NA KUWA NA NGUVU ZINAVOANZA SASA.Hiyo kitu cha kawaida ,kila zama zina muda wake .