PreGE2025 Shamira: Ni jukumu la UVCCM kuwalinda viongozi wetu wa Chama

PreGE2025 Shamira: Ni jukumu la UVCCM kuwalinda viongozi wetu wa Chama

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
843
Reaction score
1,024
NI JUKUMU LA UVCCM KUWALINDA VIONGOZI WETU WA CHAMA - SHAMIRA

Mjumbe wa Baraza Kuu (UVCCM) Taifa Ndg Shamira Mshangama amesema vijana wa CCM wana jukumu la kulinda viongozi wanaotokana na Chama cha Mapinduzi kwa kuhakikisha wanaendelea kushika nafasi ambapo kama Mbunge au diwani alikuwa ni kutoka CCM ataendela kubaki wa Chama hicho katika uchaguzi unaofuata

Shamira Mshangama ameyasema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji mkoa wa Songwe ikiwa ni muendelezo wa Ziara yake ya kuimarisha uhai wa Jumuiya ya Vijana wa CCM katika Mikoa, wilaya, Matawi na Shina kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025 ambapo amesema vijana wana jukumu la kuhakikisha kazi za Viongozi ikiwemo miradi mbalimbali inayotekelezwa inafahamika kwa wananchi

Amesema kupitia Kutangaza miradi inayotekelezwa kutasaidia kupata kura za Kishindo ambapo ametoa rai kwa vijana wote nchini kuendelea kuyasema yanayofanywa na Rais Dkt Samia katika kuwaletea wananchi Maendeleo
 
Back
Top Bottom