Shambulio la wabunge na TBC1 reporting

TBC ni ya wale wale..mitambo yenyewe imenunuliwa kwa style zilezile za rada,ndege ya rais etc. Wafanyakaz nao wanaharufu ile ile iliozoeleka..wake chonjo 2015 wote wanapoteza ajira. V
 
TBC kazi kwei kwei station nyingine wanaonyesha updates za uchaguzi wao wako na taarabu asubuhi na mapemaaaa!!kingine sijawahi ona taarifa ya habari yenye speed kali kama ya TBC1...ni hatari utafikiri mtangazaji anawahi ICU
 
Mkurugenzi wa TBC huchaguliwa na rais kwa kutumia vigezo anavyovijua yeye. kwa hali hiyo tutegemee nini? Katiba mpya tujitokeze kudai madaraka ya rais yapunguzwe,
 
Tbccm walishapoteza mwelekeo siku mwingi hakuna sababu kupoteza muda kuwajadili.
 
Hamna cha kulalamika. Huu ni wakati wa CHADEMA kufanya fund raising, ili kufungua kituo chetu cha habari.

La sivyo, unyanyasaji huu utaendelea. And its advantage kwa CCM. Hata wakifanya maovu hakuna mtu atayejua. Either wachache walioshuhudia hilo jambo
 
Mungu atasimama upande wetu daima, cha msingi tutende yote ktk haki.
 
Mkuu uko sahihi kabisa. Hilo linawezekana kama wataamua kufanya hivyo.
 
Kosa kubwa sana kwetu ilikuwa ni kuingia katika siasa za vyama vingi kwa kutumia katiba ya kuwekewa viraka. Lawama nyingi ninamtupia Mrema kwa vile mwaka 1995 ndiye aliyekuwa msitari wa mbele kudai kuwa atashinda tu chini ya katiba hiyo. Katiba hiyo ndiyo inayosababisha polisi na vyombo vyote vya umma vidhani kuwa viko pale kwa maslahi ya CCM tu.,
 
jamani awa magamba wameshindwa wanataka kutuondolea majembe yetu cdm imefunikwa na damu ya yesu so wanakazi ya ziada.
 

Hatushangai kwani sasa hivi CCM na vyombo vyake wana uwa watu wanaona ni jambo la kawaida. Kumbuka juzi juzi kwenye wilaya moja kule Morogoro, polisi wame uwa raia wema kwa kuwapiga risasi live, watu wakiwa wanashuhudia lakini mteuliwa wa Rais, Mkuu wa wilaya anasema "...hiyo nia ajali ya kawaida, kama ajali za mabasi zinavyo uwa...!"

Hii ina maana CCM ni janga, ni maafa, ni ajali na kuchagua CCM ni sawa na kupanda basi bovu linalokwenda kuuwa watu!
 

Mkuu bila ya kujali itikadi za chama, hivi inaingia akili kweli kwamba Mbunge anaweza akakatwa MAPANGA na Serikali yetu tukufu ikaona hilo ni jambo la kawaida KWELI? Mimi sikuwahi kuangalia TBC kwa hiyo siwezi kutoa maoni katika hilo.

Mimi nataka kulikumbusha jeshi la POLISI kwamba mambo ya RWANDA yalianza kidogo kidogo mwishowe likaja kuwa janga la kitaifa, Watanzania tusije kujidanganya kwamba hili aliwezi kutokea HAPA, tukumbuke hatuishi kwenye kisiwa.
 

Chonka Mwabagambila! kasinge waitu!
 
Kwa kweli habari ya shambulio la wabunge wa CDM kule Mwanza na Baadhi ya Wafuasi wa CDM kule Kiwila ni habari nzito. Sikutegemea vyombo vya dola kuwa kimya kiasi hiki au bado wameelekeza nguvu zao Arumeru?.........Mwema hebu chukua hatua za kuwanasa wahalifu waliotenda uovu huu au kama huwezi kufanya hivyo kemea tu
 
What a waste. Nashangaa imekuja automatic, huwa singalii hii TV. Sijui kwa nini.
 
Mimi binafsi TBC1 huwa naangaliga ze komedi tu basi, vipindi vingine hata sijui huwa vikoje, my wife na watoto wenyewe huwa wanaangalia chereko, ningependa na watanzania wengine nao waige mfano huu.
 
Hivi TBC walikua wanawaonesha watanzania kampeni za CDM kweli manake mie kila siku nilikua naona za CCM
 
nimekuwa naangalia tbc mara nyingi,jana wameniboa pia nakubiliana na aliyesema chadema iwe na v2o vyake itasaidia,mi nawashangaa sana wale watumishi wakoje,anyway we need a way out ila itv walionyesha vizuri
 

ccm inajua siku zake zimefikia kiama chake..........................lakini tatizo hawatatoka hadi wamng'oe mtu meno...............kuweni waangalifu sana hizi saa za majeruhi........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…