Shambulio la wabunge na TBC1 reporting

Shambulio la wabunge na TBC1 reporting

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,948
Reaction score
74,431
Taarifa ya TBC1 kuhusu kukatwa mapanga na mashoka kwa Mbunge wa Ilemela na yule wa Ukerewe imetuacha na maswali mengi. Tukio hilo ni kubwa na la aina yake kutokea katika nchi hii tokea tupate uhuru. Inakuwaje TV ya taifa waripoti swala hili kama tukio la kawaida lisilo na uzito wowote katika jamii? Au kwa vile ni wabunge waupinzani? Nchi inayojitapa kuwa ya amani na utulivu na wabunge wanapigwa mapanga na mashoka tunaenda wapi? Hoja jee kituo cha TV cha taifa kinapo dharau jambo kama hili maana yake nini katika mustakabali wa Taifa?
 
Mkuu hiyo Tbc ni ya magamba but movement 4 change ndiyo itakayoamua hatima yao hao magamba tbc.
 
nadhani wananchi watakapoanza kulipa kisasi ndio watapata cha kuandika!
 
Mshana anashindwa kujua TBC inatazamwa na watu wa itikadi mbalimbali wakiwemo wana CCM.Tunashindwa kuelewa kwa nini TBC1 inaongozwa kwa misingi ya CCM?
Basi tunawaomba TBC1 wabadilishe rangi na waweke rangi ya kijani na njano ili tujue kabisa kama ni kituo cha CCM
 
Waacheni wafanye mchezo, watakuja kujibu siku moja kwa sababu historia huwa haipotei, na pia wakumbuke kuwa hata Rwanda mambo yalianza hivi hivi.
 
Kama hawafahamu, mwenendo wa TV hii unachangia sana kwa wananchi kukatishwa imani na serikali yao (chama tawala). Hata wale wenye ufahamu mdogo wameshaelewa kuwa hii TV ni kwa ajili ya propaganda kwa chama tawala. Wabunge ni viongozi wa kitaifa, sasa tunapobagua itikadi dhidi ya wabunge wanaotuwakilisha wananchi wote kitaifa ni kutenganisha Taifa letu pia.
 
Ingekuwa ni wabunge wa CCM wangesema wamekatwa mapanga na wafuasi wa CHADEMA!
 
hii inatisha hata Ghadafi alikuwa na TV ya chama chake kwa ajili ya kuficha uovu wake.
 
Na pia wananchi waelewe kwamba Tbc ni ya wote wasio na vyama, hata wale wenzetu ambao wanasumbuliwa na magonjwa kama akili,walemavu,wafungwa,watoto,watu wazima na wengi ambao wana matatizo tofauti ni jambo la kila mmoja wetu kuelimisha jamii juu ya nini maana ya serikali maake mie nimegundua hiki kikundi flani cha watu kuanzia Rais na mawaziri na chama chao cha Magamba wanaona wao ndio serikali na pia ndio maana hata hawa wazembe watangazaji wa TBC hawaonyeshi moja kwa moja kama ni TV ya Taifa ili chaguzi zikifika waweza kuwahaada watu especialy wale wa vijijini kuwa oooh tuko na hivi na vile na wapinzani hawana hata Tv na hili ndio tatizo la nchi yetu kwani kule vijijini hata hawafahamu kwa nini wanapiga kura kuchagua viongozi maake wao wanawapa kura Magamba then wanawatosa baada ya miaka 5 wanawaona tena hata hivyo pia hawafahamu kwa nini wamekuja tena then wanawahada then wakijijini wanawapa tena maisha duuh wajinga ndio waliwao
 
Taarifa ya TBC1 kuhusu kukatwa mapanga na mashoka kwa Mbunge wa Ilemela na yule wa Ukerewe imetuacha na maswali mengi. Tukio hilo ni kubwa na la aina yake kutokea katika nchi hii tokea tupate uhuru. Inakuwaje TV ya taifa waripoti swala hili kama tukio la kawaida lisilo na uzito wowote katika jamii? Au kwa vile ni wabunge waupinzani? Nchi inayojitapa kuwa ya amani na utulivu na wabunge wanapigwa mapanga na mashoka tunaenda wapi? Hoja jee kituo cha TV cha taifa kinapo dharau jambo kama hili maana yake nini katika mustakabali wa Taifa?

Sifa kubwa ya wafuasi wa CHADEMA ni kulalamika hata pasipo na sababu ya kulalamika! Hivi ingekuwa wewe ndio muhisika pale TBC1, unge-include nini ili ionekane umeipa uzito habari hiyo?! Ukiangalia, taarifa za tukio lile limechukua takribani tatu.....Highness Kiwia amehojiwa na wala hakukatizwa alichotaka kuongea! Zitto Kabwe amehojiwa na ameyasema aliyokusia kuyasema bila kukatizwa. RPC nae amehojiwa na amesema bila kukatizwa! Wametoa picha za pale Bugando Hospital hadi Muhimbili! Nini cha ziada ambacho ungependa kionekane kwenye taarifa hiyo?! Ulitaka kuwe na live coverage?!
 
Waheshimiwa mkae mkijua kuwa huyo Mshana anaogopa kile kilichomkumba Tido. Ukurugenzi mtamu bwana...! We kama unaona hupati UKWELI NA UHAKIKA achana na TBC kama mie nilivyofanya baada ya kuona inaninyima raha ambazo nilikuwa nikizipata kipindi cha Tido Mhando.
 
hakika hapa ndipo wamedhihirisha wazi jinsi gani wnavyotafuna kodi zetu bila faida.....
sio sahihi kabisa kwa kutolipa uzito suala hili...angekuwa mbunge wa CCM ungesikia kauli kuanzia IGP, CHAGONJA, WAZIRI WA MAMBO YA NDANI.
TUTAFIKA TU IPO SIKU....TIME WILL TELL:A S shade:
 
Hata mi nimeona. ilivyoripotiwa ni kama ya kawaida sana mshana anakaribia kustaafu nini? coz kama anajua anatakiwa kuwepo kazini after 2015 huu us.ng. angeacha. CDM FUNGUENI TV!
 
Back
Top Bottom