Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
-
- #41
NYEMO CHILONGANI
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269
Sehemu ya Tisa.
HISTORIA YA MTU WA PILI KATI YA WALE WATANO ILIYOMFANYA KUWA NDANI YA NDEGE HIYO.
Mtu wa Pili Ndani ya Ndege.
“Guys, tell me what the hell is going on,” (jamani niambieni kitu gani kinaendelea) alisikika mwanaume mmoja aliyeitwa Sam Scott kutoka katika ofisi ya ndani kabisa katika jengo la makao makuu ya Shirika la Kijasusi nchini Marekani, CIA (Central Intelligence Agency) yaliyokuwa Langley, Virginia, McLean, Virginia nchini Marekani.
“The president calls the press,” (rais amewaita waandishi wa habari) alisema mwanaume mwingine kwenye simu.
“I want to get the feedback as soon as possible,” (nataka kupata kinachoendelea haraka iwezekanavyo) alisema Scott na kukata simu.
Dunia nzima ilikuwa bize kusikilizia kile kilichokuwa kikiendelea nchini Iraq. Watu walitega masikio yao, walihitaji kujua sababu ya rais wa nchi hiyo, Sharif Hamis kuwaita waandishi wa habari na kutaka kuzungumza nao.
Kila mmoja alimfahamu rais huyo, alikuwa miongoni mwa marais viburi waliowahi kutokea hapa duniani. Alikuwa mtu aliyependa fujo ambaye alitawala kibabe nchini mwake.
Watu hawakumpenda kwa sababu alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa ambaye alikuwa na uwezo wa kufanya kitu chochote kile, wakati wowote pasipo kuogopa chochote.
Marekani walijitahidi kumuwekea vikwazo rais huyo, hakujali, kitu alichokijua ni kwamba alikusanya pesa nyingi kutokana na visima vya mafuta vilivyokuwa nchini mwake.
Nchi iliingiza pesa nyingi kupitia mafuta, ilijiendesha kama ilivyotakiwa kuwa kwa sababu tu biashara hiyo ilikuwa na pesa, aliziunganisha nchi nyingi na kuziuzia mafuta hayo ambayo yalimfanya kupata pesa nyingi.
Hakujali kuhusu Marekani, walimwambia wangeweza kuilipua nchi yake lakini hakutaka kujali, kwake, kelele zao zilikuwa ni sawa na muziki uliopigwa mbele ya mbuzi ili acheze lakini hakufanya hivyo.
Siku zikaendelea, baada ya Urusi kuona kulikuwa na maslahi makubwa nchini Iraq, rais wa nchi hiyo, Bwana Petrov Ludovick akampigia simu Rais Hamis na kumwambia kwamba hakutakiwa kuogopa kwa sababu alikuwa upande wake, kama kungekuwa na mtu yeyote ambaye angembabaisha basi angemsaidia kupambana na adui huyo.
Kwa Hamis akakenua, hakuamini kama angepata msaada kutoka kwa nchi kubwa kama Urusi, kitendo cha Rais Ludovick kusema angemtetea kwenye kila hatua, kwake ikaonekana kuwa ushindi mkubwa, akaongeza kiburi zaidi.
Alichokuwa akikiangalia Ludovick si kumlinda tu mwanaume huyo bali alihitaji kuingia kwenye biashara ya mafuta na nchi hiyo, aliamini kwamba Marekani alihitaji sana kupata mafuta kutoka nchini humo kibabe, yeye hakutaka kufanya hivyo na ndiyo maana kitu cha kwanza kabisa ambacho alihitaji kukipata ni kuchukua nafasi ya kufanya biashara na Iraq kwa kutengeneza urafiki.
Urafiki huo haukuwa siri, Marekani wakajua kwamba Urusi aliingilia kati, kulikuwa na mipango mingi ambayo nchi hiyo ilipanga, waligundua kwamba rais Ludovick aliahidi kumlinda Hamis, hata kama kungekuwa na wabaya walihitaji kupambana naye, mtu wa kwanza kabisa ambaye angejitokeza angekuwa Urusi.
Hilo liliwaumiza vichwa Wamarekani, walishindwa kujua nini cha kufanya. Urusi ilikuwa nchi kubwa na yenye silaha kubwa za kijeshi lakini kubwa zaidi ni kwamba walikuwa karibu na Marekani.
Kama ambavyo Marekani alivyokuwa mbabe, hata Urusi alikuwa hivyohivyo, hawakuwahi kupatana na kila siku walikuwa wakiangaliana kama maadui, yaani ni kama kila mmoja alikuwa akimsubiri mwenzake amchokoze.
Baada ya siku nyingi kupita hatimaye Rais Hamis akawaita waandishi wa habari na kutaka kuzungumza nao kitu, kila mtu alihitaji kusikia ni kitu gani kingezungumzwa mahali hapo mbele ya waandishi wa habari.
Waandishi hao walifika ikulu, waliweka kamera zao, waliujua ubabe wake, walijua kabisa kama siku hiyo mwanaume huyo alihitaji kuzungumza kitu cha kuigusa dunia kwa sababu tu hakuwa akipatana na mataifa mengi nje ya himaya ya Waarabu.
Baada ya dakika kadhaa, rais huyo akafika mbele ya waandishi wa habari. Alivalia kanzu nyeupe, iliyong’ara huku akiwa na kilemba kichwani mwake, kwa kumwangalia harakaharaka ilikuwa ni rahisi kusema mtu huyo alikuwa mtakatifu, mwenye moyo mzuri na wa kujishusha kama Mtume Muhammad kumbe haikuwa hivyo, alikuwa mwanaume aliyeishi katika dunia yake ya kibabe aliyependa kila mtu duniani amuogope.
Akakaa kwenye kiti chake, kabla ya kuzungumza kitu chochote kile, akaachia tabasamu pana, akachukua maji na kuanza kunywa, alihitaji kuzungumza kitu ambacho alijua kabisa dunia ingeshtuka na kuona hakukuwa na amani tena.
Hakutaka kupoteza muda wa waaandishi wa habari, akaanza kuzungumza kile kitu kilichomfanya kuwaita waandishi wa habari, aliwaambia kwamba alikuwa na mabomu ya nyuklia saba ambayo yalitengenezwa na watu wake, alikuwa na silaha nzito ambazo kila mtu alitakiwa kumuogopa.
Kila mtu aliyesikia hivyo, akashtuka, hapakuwa na mtu aliyeamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa na mabomu ya nyuklia, Marekani wenyewe kwenye stoo ya mabomu yao kipindi hicho walikuwa na mabomu matatu tu ambayo walikuwa wakiringia nayo, cha ajabu Rais Hamis alikuwa na mabomu saba, alionekana kuwa mtu tishio.
Haraka sana Rais Ludovick wa Marekani akaitisha kikao ikulu na kutaka kuzungumza na viongozi wa juu wa CIA. Alihitaji kuwaambia kile kilichokuwa kimetokea, walitakiwa kujipanga na kuhakikisha wanashinda kila kitu kilichokuwa mbele yao.
Simu ikapigwa na ndani ya nusu saa watu hao walikuwa ikulu na kufanya kikao hicho kidogo. Walizungumza mambo mengi ikiwemo lile la kuwamaliza watu waliokuwa wametengeneza mabomu hayo lakini kitu kikubwa zaidi kilikuwa ni kuhakikisha wanapata formula ambayo wataalamu wa Rais Hamis waliitumia kutengeneza mabomu hayo.
“Tuhakikisheni tunafanikiwa katika hilo, sawa?” alisema Rais Ludovick.
“Sawa.”
Wakaondoka, aliwaachia kazi ya kuhakikisha hilo linafanyika haraka pasipo kugundulika. Ili hilo lifanikiwe ilikuwa ni lazima kumtuma mtu kwenda nchini Iraq ambapo huko angefanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanafanikiwa katika hilo.
Hawakutakiwa kumtuma jasusi wa Kizungu kwa kuwa walijua ingekuwa ni rahisi kugundulika, mtu ambaye alitakiwa kwenda huko ni jasusi mweusi ambaye angejifanya kama mfanyabiashara kutoka barani Afrika, ila baada ya kufika huko angefanya kila liwezekanalo kuhakikisha anagundua kila kitu kilichokuwa kikiendelea pamoja na kupata formula hiyo.
Walichokifanya ni kumchukua jasusi aliyeitwa kwa jina la Kennedy Edward ila kwenye kazi hiyo alitakiwa atumie jina la Ibrahim Munir ambaye angejifanya kuwa mfanyabiashara wa mafuta aliyekuwa na kampuni yake nchini Kenya.
Kabla ya yote, kitu cha kwanza walichokifanya ni kumtengenezea hati za kusafiria ambazo zilionyesha alikuwa akitokea nchini Kenya, hawakuishia hapo bali wakatengeneza tovuti yake binafsi ambayo ilionyesha shughuli mbalimbali za kijamii alizokuwa akizifanya nchini Kenya huku kukiwa na picha za kutengenezwa.
Kwa kuwa walikuwa na uhitaji wa kukamilisha kazi yao ilikuwa ni lazima Kennedy asafirishwe kuelekea nchini Kenya ambapo huko angetembelea vituo vya watoto yatima.
Hilo halikuwa tatizo kabisa lakini pia alitakiwa kubadilisha muonekano wake, haraka sana sura ya bandia ikaletwa na kuvalishwa, kila kitu ambacho kilikuwa kikienda kufanyika katika nchi za Kiarabu kilitakiwa kuwa siri kubwa, hakutakiwa mtu yeyote kufahamu kama alitumwa kwenda nchini humo kwa kazi maalumu.
Ilikuwa ni lazima kazi ifanyike, picha zipigwe huko Kenya na hatimaye kuingizwa kwenye tovuti hiyo na kwa sababu walikuwa siriazi na kazi hiyo, wakamtengenezea ukurasa wake wikipedia ambapo humo kulikuwa na stori yake ya uongo kuhusu maisha yake na mpaka alipoanza kufanya biashara ya mafuta huku akiwa ametokea katika familia ya kimasikini.
Mbali na yote hayo, pia walimtaka kupiga picha nyingi akiwa na kanzu, ilikuwa ni lazima aonekane kama alikuwa Muislamu hivyo alitakiwa kuuvaa uhusika na kupelekewa ustadhi ambaye alikuwa na kazi ya kumfundisha kuswali na kufanya mambo mengine katika dini hiyo.
Alikuwa makini kwa kila kitu, kichwa chake kilikuwa na uwezo mkubwa wa kukariri kila kitu alichokuwa akifundishwa, baada ya mwezi mmoja na kuonekana alikuwa tayari kwa kila kitu, akasafirishwa mpaka Dubai huku hati zake zote za kusafiria zikionekana kama alikuwa raia wa Kenya na kuanza kuelekea nchini Iraq.
Kabla ya kufika huko, tayari Wamarekani waliwasiliana na watu wao juu ya mtu huyo, waliwaambia watangaze kwamba mfanyabiashara mkubwa kutoka nchini Kenya alikuwa akienda nchini Iraq kufanya utalii wa kuzunguka sehemu mbalimbali ambazo mitume ya zamani ilikuwa imepitia.
Watu walitakiwa kujua ujio wake, si hilo tu bali pia watu walitakiwa kufahamu kwamba mtu ambaye alikuwa akija alikuwa bilionea mkubwa ambapo akaunti yake ilisoma kuwa na kiasi cha dola bilioni thelathini ambazo zilikuwa ni zaidi ya trilioni sitini, pesa hizo zote zilikuwa hewa lakini hilo hakukuwa na mtu aliyekuwa akilifahamu zaidi yake na watu waliokuwa wamemtuma.
Matangazo yakaanza kutolewa sehemu mbalimbali, kitendo cha bilionea kutoka Kenya kutangazwa kwamba alikuwa akienda nchini humo kutembelea sehemu mbalimbali za makumbusho na hata kutoa misaada, kila mmoja alichanganyikiwa, alikuwa Mwafrika lakini Waarabu hawakutaka kujali kuhusu ngozi, walichokuwa wakikijali ni kuona nchi yao ikinufaika na ujio wa mwanaume huyo.
Kila kona kulikuwa na stori kuhusu yeye, hakuwa amefika nchini humo lakini wale watu ambao walitumiwa kufikisha habari nchini humo walifanya kazi kwa uaminifu mkubwa mno kiasi kwamba ndani ya siku mbili tu, tayari alikuwa mwanaume maarufu sana.
Wale ambao hawakuwa wakimfahamu walikwenda kwenye tovuti mbalimbali na kulitafuta jina lake. Hawakupata tabu kumpata, ni ndani ya dakika chache tu walimuona akiwa sehemu mbalimbali Afrika huku akionekana kuwasaidia watu wengi waliokuwa kwenye matatizo.
Kwa jinsi alivyokuwa akijitoa, kila mmoja alifurahia, alionekana kuwa mwanaume mwenye roho nzuri ambaye alitamani kuona kila mtu akipata kile kidogo alichokuwanacho.
Uso wake ulikuwa wa huruma sana, alionekana kama malaika ambaye alitumwa duniani kwa ajili ya kuwasaidia watu waliokuwa wakiteseka kwa njaa kila siku.
Katika nakala zake alizobeba, aliandikiwa kwamba alitakiwa kufikia katika Hoteli ya Sultani Alwaqidr iliyokuwa pembezoni na Mji wa Baghdad.
Katika hoteli hiyo kulikuwa na msichana aliyeitwa kwa jina la Nurat ambaye alitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha msichana huyo anakuwa na ukaribu naye kwa sababu baba wa msichana huyo aliyeitwa Shabir Kuwad alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa matunda ndani ya jiji hilo.
“Sijaelewa, lengo hapa ni nini?” aliuliza Kennedy ambaye alijulikana kwa jina la Ibrahim Munir.
“Tunahitaji utengeneze ukaribu naye, umpende, umjali lakini mwisho wa siku tunataka uende mpaka nyumbani kwao, huko, tengeneza ukaribu na baba yake ambaye ni muhimu sana kwetu,” alisema mwanaume kwenye simu.
“Halafu?”
“Kwanza fanya hivyo, tutakwambia kazi kubwa ya baba yake. Hakikisha kwanza unaanza kumteka kimapenzi Nurat, halafu baada ya hapo tutakwambia ni kitu gani unatakiwa kufanya. Nakutumia picha ya Nurat ili isiwe vigumu kumpata,” alisema mwanaume huyo na kumtumia picha ya msichana huyo.
“Sawa. Nimemuona, nitakamilisha kila kitu na formula tutaipata tu,” alisema Kennedy na kisha kuzima simu ambayo ilikuwa ikitumia huduma ya wireless ndani ya ndege ile.
Je, nini kitaendelea kwa jamaa huyu wa pili?
Je, nini kitaepelekea kuingia ndani ya ndege ile?
Tukutane Alhamisi
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269
Sehemu ya Tisa.
HISTORIA YA MTU WA PILI KATI YA WALE WATANO ILIYOMFANYA KUWA NDANI YA NDEGE HIYO.
Mtu wa Pili Ndani ya Ndege.
“Guys, tell me what the hell is going on,” (jamani niambieni kitu gani kinaendelea) alisikika mwanaume mmoja aliyeitwa Sam Scott kutoka katika ofisi ya ndani kabisa katika jengo la makao makuu ya Shirika la Kijasusi nchini Marekani, CIA (Central Intelligence Agency) yaliyokuwa Langley, Virginia, McLean, Virginia nchini Marekani.
“The president calls the press,” (rais amewaita waandishi wa habari) alisema mwanaume mwingine kwenye simu.
“I want to get the feedback as soon as possible,” (nataka kupata kinachoendelea haraka iwezekanavyo) alisema Scott na kukata simu.
Dunia nzima ilikuwa bize kusikilizia kile kilichokuwa kikiendelea nchini Iraq. Watu walitega masikio yao, walihitaji kujua sababu ya rais wa nchi hiyo, Sharif Hamis kuwaita waandishi wa habari na kutaka kuzungumza nao.
Kila mmoja alimfahamu rais huyo, alikuwa miongoni mwa marais viburi waliowahi kutokea hapa duniani. Alikuwa mtu aliyependa fujo ambaye alitawala kibabe nchini mwake.
Watu hawakumpenda kwa sababu alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa ambaye alikuwa na uwezo wa kufanya kitu chochote kile, wakati wowote pasipo kuogopa chochote.
Marekani walijitahidi kumuwekea vikwazo rais huyo, hakujali, kitu alichokijua ni kwamba alikusanya pesa nyingi kutokana na visima vya mafuta vilivyokuwa nchini mwake.
Nchi iliingiza pesa nyingi kupitia mafuta, ilijiendesha kama ilivyotakiwa kuwa kwa sababu tu biashara hiyo ilikuwa na pesa, aliziunganisha nchi nyingi na kuziuzia mafuta hayo ambayo yalimfanya kupata pesa nyingi.
Hakujali kuhusu Marekani, walimwambia wangeweza kuilipua nchi yake lakini hakutaka kujali, kwake, kelele zao zilikuwa ni sawa na muziki uliopigwa mbele ya mbuzi ili acheze lakini hakufanya hivyo.
Siku zikaendelea, baada ya Urusi kuona kulikuwa na maslahi makubwa nchini Iraq, rais wa nchi hiyo, Bwana Petrov Ludovick akampigia simu Rais Hamis na kumwambia kwamba hakutakiwa kuogopa kwa sababu alikuwa upande wake, kama kungekuwa na mtu yeyote ambaye angembabaisha basi angemsaidia kupambana na adui huyo.
Kwa Hamis akakenua, hakuamini kama angepata msaada kutoka kwa nchi kubwa kama Urusi, kitendo cha Rais Ludovick kusema angemtetea kwenye kila hatua, kwake ikaonekana kuwa ushindi mkubwa, akaongeza kiburi zaidi.
Alichokuwa akikiangalia Ludovick si kumlinda tu mwanaume huyo bali alihitaji kuingia kwenye biashara ya mafuta na nchi hiyo, aliamini kwamba Marekani alihitaji sana kupata mafuta kutoka nchini humo kibabe, yeye hakutaka kufanya hivyo na ndiyo maana kitu cha kwanza kabisa ambacho alihitaji kukipata ni kuchukua nafasi ya kufanya biashara na Iraq kwa kutengeneza urafiki.
Urafiki huo haukuwa siri, Marekani wakajua kwamba Urusi aliingilia kati, kulikuwa na mipango mingi ambayo nchi hiyo ilipanga, waligundua kwamba rais Ludovick aliahidi kumlinda Hamis, hata kama kungekuwa na wabaya walihitaji kupambana naye, mtu wa kwanza kabisa ambaye angejitokeza angekuwa Urusi.
Hilo liliwaumiza vichwa Wamarekani, walishindwa kujua nini cha kufanya. Urusi ilikuwa nchi kubwa na yenye silaha kubwa za kijeshi lakini kubwa zaidi ni kwamba walikuwa karibu na Marekani.
Kama ambavyo Marekani alivyokuwa mbabe, hata Urusi alikuwa hivyohivyo, hawakuwahi kupatana na kila siku walikuwa wakiangaliana kama maadui, yaani ni kama kila mmoja alikuwa akimsubiri mwenzake amchokoze.
Baada ya siku nyingi kupita hatimaye Rais Hamis akawaita waandishi wa habari na kutaka kuzungumza nao kitu, kila mtu alihitaji kusikia ni kitu gani kingezungumzwa mahali hapo mbele ya waandishi wa habari.
Waandishi hao walifika ikulu, waliweka kamera zao, waliujua ubabe wake, walijua kabisa kama siku hiyo mwanaume huyo alihitaji kuzungumza kitu cha kuigusa dunia kwa sababu tu hakuwa akipatana na mataifa mengi nje ya himaya ya Waarabu.
Baada ya dakika kadhaa, rais huyo akafika mbele ya waandishi wa habari. Alivalia kanzu nyeupe, iliyong’ara huku akiwa na kilemba kichwani mwake, kwa kumwangalia harakaharaka ilikuwa ni rahisi kusema mtu huyo alikuwa mtakatifu, mwenye moyo mzuri na wa kujishusha kama Mtume Muhammad kumbe haikuwa hivyo, alikuwa mwanaume aliyeishi katika dunia yake ya kibabe aliyependa kila mtu duniani amuogope.
Akakaa kwenye kiti chake, kabla ya kuzungumza kitu chochote kile, akaachia tabasamu pana, akachukua maji na kuanza kunywa, alihitaji kuzungumza kitu ambacho alijua kabisa dunia ingeshtuka na kuona hakukuwa na amani tena.
Hakutaka kupoteza muda wa waaandishi wa habari, akaanza kuzungumza kile kitu kilichomfanya kuwaita waandishi wa habari, aliwaambia kwamba alikuwa na mabomu ya nyuklia saba ambayo yalitengenezwa na watu wake, alikuwa na silaha nzito ambazo kila mtu alitakiwa kumuogopa.
Kila mtu aliyesikia hivyo, akashtuka, hapakuwa na mtu aliyeamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa na mabomu ya nyuklia, Marekani wenyewe kwenye stoo ya mabomu yao kipindi hicho walikuwa na mabomu matatu tu ambayo walikuwa wakiringia nayo, cha ajabu Rais Hamis alikuwa na mabomu saba, alionekana kuwa mtu tishio.
Haraka sana Rais Ludovick wa Marekani akaitisha kikao ikulu na kutaka kuzungumza na viongozi wa juu wa CIA. Alihitaji kuwaambia kile kilichokuwa kimetokea, walitakiwa kujipanga na kuhakikisha wanashinda kila kitu kilichokuwa mbele yao.
Simu ikapigwa na ndani ya nusu saa watu hao walikuwa ikulu na kufanya kikao hicho kidogo. Walizungumza mambo mengi ikiwemo lile la kuwamaliza watu waliokuwa wametengeneza mabomu hayo lakini kitu kikubwa zaidi kilikuwa ni kuhakikisha wanapata formula ambayo wataalamu wa Rais Hamis waliitumia kutengeneza mabomu hayo.
“Tuhakikisheni tunafanikiwa katika hilo, sawa?” alisema Rais Ludovick.
“Sawa.”
Wakaondoka, aliwaachia kazi ya kuhakikisha hilo linafanyika haraka pasipo kugundulika. Ili hilo lifanikiwe ilikuwa ni lazima kumtuma mtu kwenda nchini Iraq ambapo huko angefanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanafanikiwa katika hilo.
Hawakutakiwa kumtuma jasusi wa Kizungu kwa kuwa walijua ingekuwa ni rahisi kugundulika, mtu ambaye alitakiwa kwenda huko ni jasusi mweusi ambaye angejifanya kama mfanyabiashara kutoka barani Afrika, ila baada ya kufika huko angefanya kila liwezekanalo kuhakikisha anagundua kila kitu kilichokuwa kikiendelea pamoja na kupata formula hiyo.
Walichokifanya ni kumchukua jasusi aliyeitwa kwa jina la Kennedy Edward ila kwenye kazi hiyo alitakiwa atumie jina la Ibrahim Munir ambaye angejifanya kuwa mfanyabiashara wa mafuta aliyekuwa na kampuni yake nchini Kenya.
Kabla ya yote, kitu cha kwanza walichokifanya ni kumtengenezea hati za kusafiria ambazo zilionyesha alikuwa akitokea nchini Kenya, hawakuishia hapo bali wakatengeneza tovuti yake binafsi ambayo ilionyesha shughuli mbalimbali za kijamii alizokuwa akizifanya nchini Kenya huku kukiwa na picha za kutengenezwa.
Kwa kuwa walikuwa na uhitaji wa kukamilisha kazi yao ilikuwa ni lazima Kennedy asafirishwe kuelekea nchini Kenya ambapo huko angetembelea vituo vya watoto yatima.
Hilo halikuwa tatizo kabisa lakini pia alitakiwa kubadilisha muonekano wake, haraka sana sura ya bandia ikaletwa na kuvalishwa, kila kitu ambacho kilikuwa kikienda kufanyika katika nchi za Kiarabu kilitakiwa kuwa siri kubwa, hakutakiwa mtu yeyote kufahamu kama alitumwa kwenda nchini humo kwa kazi maalumu.
Ilikuwa ni lazima kazi ifanyike, picha zipigwe huko Kenya na hatimaye kuingizwa kwenye tovuti hiyo na kwa sababu walikuwa siriazi na kazi hiyo, wakamtengenezea ukurasa wake wikipedia ambapo humo kulikuwa na stori yake ya uongo kuhusu maisha yake na mpaka alipoanza kufanya biashara ya mafuta huku akiwa ametokea katika familia ya kimasikini.
Mbali na yote hayo, pia walimtaka kupiga picha nyingi akiwa na kanzu, ilikuwa ni lazima aonekane kama alikuwa Muislamu hivyo alitakiwa kuuvaa uhusika na kupelekewa ustadhi ambaye alikuwa na kazi ya kumfundisha kuswali na kufanya mambo mengine katika dini hiyo.
Alikuwa makini kwa kila kitu, kichwa chake kilikuwa na uwezo mkubwa wa kukariri kila kitu alichokuwa akifundishwa, baada ya mwezi mmoja na kuonekana alikuwa tayari kwa kila kitu, akasafirishwa mpaka Dubai huku hati zake zote za kusafiria zikionekana kama alikuwa raia wa Kenya na kuanza kuelekea nchini Iraq.
Kabla ya kufika huko, tayari Wamarekani waliwasiliana na watu wao juu ya mtu huyo, waliwaambia watangaze kwamba mfanyabiashara mkubwa kutoka nchini Kenya alikuwa akienda nchini Iraq kufanya utalii wa kuzunguka sehemu mbalimbali ambazo mitume ya zamani ilikuwa imepitia.
Watu walitakiwa kujua ujio wake, si hilo tu bali pia watu walitakiwa kufahamu kwamba mtu ambaye alikuwa akija alikuwa bilionea mkubwa ambapo akaunti yake ilisoma kuwa na kiasi cha dola bilioni thelathini ambazo zilikuwa ni zaidi ya trilioni sitini, pesa hizo zote zilikuwa hewa lakini hilo hakukuwa na mtu aliyekuwa akilifahamu zaidi yake na watu waliokuwa wamemtuma.
Matangazo yakaanza kutolewa sehemu mbalimbali, kitendo cha bilionea kutoka Kenya kutangazwa kwamba alikuwa akienda nchini humo kutembelea sehemu mbalimbali za makumbusho na hata kutoa misaada, kila mmoja alichanganyikiwa, alikuwa Mwafrika lakini Waarabu hawakutaka kujali kuhusu ngozi, walichokuwa wakikijali ni kuona nchi yao ikinufaika na ujio wa mwanaume huyo.
Kila kona kulikuwa na stori kuhusu yeye, hakuwa amefika nchini humo lakini wale watu ambao walitumiwa kufikisha habari nchini humo walifanya kazi kwa uaminifu mkubwa mno kiasi kwamba ndani ya siku mbili tu, tayari alikuwa mwanaume maarufu sana.
Wale ambao hawakuwa wakimfahamu walikwenda kwenye tovuti mbalimbali na kulitafuta jina lake. Hawakupata tabu kumpata, ni ndani ya dakika chache tu walimuona akiwa sehemu mbalimbali Afrika huku akionekana kuwasaidia watu wengi waliokuwa kwenye matatizo.
Kwa jinsi alivyokuwa akijitoa, kila mmoja alifurahia, alionekana kuwa mwanaume mwenye roho nzuri ambaye alitamani kuona kila mtu akipata kile kidogo alichokuwanacho.
Uso wake ulikuwa wa huruma sana, alionekana kama malaika ambaye alitumwa duniani kwa ajili ya kuwasaidia watu waliokuwa wakiteseka kwa njaa kila siku.
Katika nakala zake alizobeba, aliandikiwa kwamba alitakiwa kufikia katika Hoteli ya Sultani Alwaqidr iliyokuwa pembezoni na Mji wa Baghdad.
Katika hoteli hiyo kulikuwa na msichana aliyeitwa kwa jina la Nurat ambaye alitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha msichana huyo anakuwa na ukaribu naye kwa sababu baba wa msichana huyo aliyeitwa Shabir Kuwad alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa matunda ndani ya jiji hilo.
“Sijaelewa, lengo hapa ni nini?” aliuliza Kennedy ambaye alijulikana kwa jina la Ibrahim Munir.
“Tunahitaji utengeneze ukaribu naye, umpende, umjali lakini mwisho wa siku tunataka uende mpaka nyumbani kwao, huko, tengeneza ukaribu na baba yake ambaye ni muhimu sana kwetu,” alisema mwanaume kwenye simu.
“Halafu?”
“Kwanza fanya hivyo, tutakwambia kazi kubwa ya baba yake. Hakikisha kwanza unaanza kumteka kimapenzi Nurat, halafu baada ya hapo tutakwambia ni kitu gani unatakiwa kufanya. Nakutumia picha ya Nurat ili isiwe vigumu kumpata,” alisema mwanaume huyo na kumtumia picha ya msichana huyo.
“Sawa. Nimemuona, nitakamilisha kila kitu na formula tutaipata tu,” alisema Kennedy na kisha kuzima simu ambayo ilikuwa ikitumia huduma ya wireless ndani ya ndege ile.
Je, nini kitaendelea kwa jamaa huyu wa pili?
Je, nini kitaepelekea kuingia ndani ya ndege ile?
Tukutane Alhamisi