MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,698
- 7,883
Majaji wawili kutoka Uganda na Namibia ni miongoni mwa makamishna sita watakaochunguza waliohusika na makosa ya jinai na ukiukwaji wa sheria uliotokea kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzindua rasmi tume hiyo Ijumaa.
Tume hiyo, iliyopewa muda wa miezi mitano kukamilisha kazi yake, inaongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Shabani Ally Lila, huku Rais Samia akisema muda huo unaweza kuongezwa endapo kutakuwa na sababu za msingi.
"Kama kutakuwa na ombi la kuongezewa muda, tutaliangalia baadaye," alisema Rais Samia wakati wa uzinduzi uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.
Majaji wa nje walioteuliwa ni Petrus Tileinge Damaseb wa Namibia na Cheborion Barishaki wa Uganda.