Shairi: Nilipomuona Simba

Shairi: Nilipomuona Simba

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
1)nilitembea porini,nilipo kwenda kuwinda,kwenye mbuga yenye nyoka.
Moyoni ninaamini,hakuna cha kunishinda,nnge swala pia nyoka.
Podo yangu mgongoni,na mshale ulopinda,haraka nikashituka.
Nilipo mi msituni,tena namuona simba,atembea akiimba.
2)sauti ilo makini,tasema tu wakiponda,wao chanzo haribika.
Wana mali majumbani,waliiba kikandanda,msone wacheka cheka.
Wanaroho za shetani,moyoni wana vidonda,karibia watatoka

Nilipo mi msituni,tena namuona simba,atembea akiimba

SHAIRI:NILIPOMUONA SIMBA..
MTUNZI:Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0655519736
 
)Mkonini nashika chaki,utao
nauandika.
Siyo kama mi sitaki,mloto unasomeka.
Na vaa vazi la kaki,ukwapi
unazinduka.
Mtamu usi na dhiki,kama pindu
kaumbika.
Darasa la mafahali,makomando
jemedari.
2)tuwaache halaiki,kikwamba
kikisifika.
Kisishika mamluki,kwa vina
visivyonuka.
Tasdisa si falaki,ulogwe ukalogeka.
Mandhuma kama laki,msuko
ukipangika.
Darasa la mafahali,makomandi
jemedari.
3)mloto kama mkuki,mleo hautazika.
Mkarara huchomoki,mwandamo
ukilipuka.
Kibwagizo chenye keki,ubeti
ukichezeka.
Takhmisa huandiki,kisa kili imechoka.
Darasa la mafahali,makomando
jemedari.
4)ukumi tungo ya haki,kamwe
hitofurahika
Wote wala mishikaki,mafisadi
wang'atuka.
Mavue kumaliziki,tungo nzuri
tengezeka.
Wawe asili ya nyuki,katujalia rabuka.
Darasa la mafahali,makomando
jemedari.
5)tenzi nzuri zihakiki,ukawafi
ukishika.
Sama bila ya mikiki,haiwezi kufutika.
Kibwagizo si fataki,eti boma kulipuka.
Talthitha huzinduki,soma uje furahika.
Darasa la mafahali,makomando
jemedari.
6)kwa bahari pasifiki,inkisari
punguzika.
Tabdila wako rafiki,mandhuma si
dhihaka.
Ukaraguni iliki,na shairi linalika.
Guni vue zi lukuki,kichwani
zitochanika.
Darasa la mafahali,makomando
jemedari
Shairi=DARASA LA MAFAHALI.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0655519736.
 
huo ndo utamu wa kiswahili.
hapa labda aje Nyani Ngabu na Kiranga wao wataelewa zaidi.
wengine siye kiswahili cha kichaga mweeehhhh..........imekula kwetu. snowhite njoo usome ushairi huku.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom