Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 2,439
- 6,691
Wakuu,
Huyu shahidi anasema mara tu baada ya kuangalia video ya Jambo TV kuhusu kauli ya Lisu kuwa atakinukisha, alifuatwa na Polisi na kukamatwa na kisha akapelekwa kwa RCO ambapo alipewa kosa la kutaka kuanzisha fujo.
Does this make sense?
=======================
Wakili: Tarehe 03/04/2025 kuna nini kilitokea?
Shahidi wa kificho : hiyo tarehe majira ya jioni nilikuwa kijiwe cha kwa morombo Arusha. Tulikuwa hapo kijiweni na tunafanya mazungumzo ya kawaida.
Wakili: Ikawaje?
Shahidi wa kificho : Kuna mwenzetu akasema hamjasikia Chadema wamesema watazuia Uchaguzi wa Mwaka huu. Wamesema watakinukisha mbaya. Alikuwa anatuelezea huyo mtu.
Wakili: kingine ni nini?
Shahidi wa kificho : Akasema kuwa Polisi wanaiba kura hata ukienda Mahakamani hautapata haki.
Wakili: Kikaendelea baada ya mtu huyo kusema?
Shahidi wa kificho : Akasema pia Majaji ni vibaraka wa CCM, akasema pia mwaka 2024 tume ya Uchaguzi ilipewa maelekezo ya kukata wajumbe wa Chadema. Tukiwa tunaendelea na hayo mazungumzo nilipata hamasa kupitia hayo maneno niliyosikia akisema yule Bajaji mwenzangu.
Wakili: Sasa weka vizuri, wewe ulifanya nini?
Shahidi wa kificho : Niliingia kwenye mtandao wa youtube na mimi niweze kujionea hayo maneno. Nilitumia simu yangu na kuingia channel inaitwa Jambo. Simu ya janja.
Wakili: Nini kiliendelea?
Shahidi wa kificho : Nikafungua channel ya Jambo na kukuta yale maneno kama nilivyoambiwa hapo kijiweni.
Wakili: Nini kikaendelea?
Shahidi wa kificho : Baada ya dakika chache kuna watu wakaja wakajitambulisha kama wao ni maaskari na baadae watu walikimbia tukakamatwa mimi na P4.
Wakili: kilichoendelea hapo?
Shahidi wa kificho : Tukapelekwa kituo cha Polisi Murieti. Tulikaa kama Dakika 45 tukapelekwa kituo cha Polisi Central Mjini.
Wakili: baada ya kuwa umepelekwa Central ikawaje?
Shahidi wa kificho : Tukaingizwa Ofisi ya RCO nikaambiwa nashitakiwa kwa kosa la kutaka kufanya fujo, niliandikwa maelezo na kuingizwa Mahabusu na asubuhi yake ndugu zangu walinifuata nikazaminiwa na kupewa tarehe za kuwa naenda kuripoti kwenye hicho kituo cha Polisi.
Wakili: Nini kilifuata?
Shahidi wa kificho : Nikawa naripoti kwa mujibu mpangilio wa hiyo ratiba na ilipofika Tar. 17/04 2025 baada ya kufika kuripoti kama kawaida, nikaambiwa naandikwa maelezo upya.
Huyu shahidi anasema mara tu baada ya kuangalia video ya Jambo TV kuhusu kauli ya Lisu kuwa atakinukisha, alifuatwa na Polisi na kukamatwa na kisha akapelekwa kwa RCO ambapo alipewa kosa la kutaka kuanzisha fujo.
Does this make sense?
=======================
Wakili: Tarehe 03/04/2025 kuna nini kilitokea?
Shahidi wa kificho : hiyo tarehe majira ya jioni nilikuwa kijiwe cha kwa morombo Arusha. Tulikuwa hapo kijiweni na tunafanya mazungumzo ya kawaida.
Wakili: Ikawaje?
Shahidi wa kificho : Kuna mwenzetu akasema hamjasikia Chadema wamesema watazuia Uchaguzi wa Mwaka huu. Wamesema watakinukisha mbaya. Alikuwa anatuelezea huyo mtu.
Wakili: kingine ni nini?
Shahidi wa kificho : Akasema kuwa Polisi wanaiba kura hata ukienda Mahakamani hautapata haki.
Wakili: Kikaendelea baada ya mtu huyo kusema?
Shahidi wa kificho : Akasema pia Majaji ni vibaraka wa CCM, akasema pia mwaka 2024 tume ya Uchaguzi ilipewa maelekezo ya kukata wajumbe wa Chadema. Tukiwa tunaendelea na hayo mazungumzo nilipata hamasa kupitia hayo maneno niliyosikia akisema yule Bajaji mwenzangu.
Wakili: Sasa weka vizuri, wewe ulifanya nini?
Shahidi wa kificho : Niliingia kwenye mtandao wa youtube na mimi niweze kujionea hayo maneno. Nilitumia simu yangu na kuingia channel inaitwa Jambo. Simu ya janja.
Wakili: Nini kiliendelea?
Shahidi wa kificho : Nikafungua channel ya Jambo na kukuta yale maneno kama nilivyoambiwa hapo kijiweni.
Wakili: Nini kikaendelea?
Shahidi wa kificho : Baada ya dakika chache kuna watu wakaja wakajitambulisha kama wao ni maaskari na baadae watu walikimbia tukakamatwa mimi na P4.
Wakili: kilichoendelea hapo?
Shahidi wa kificho : Tukapelekwa kituo cha Polisi Murieti. Tulikaa kama Dakika 45 tukapelekwa kituo cha Polisi Central Mjini.
Wakili: baada ya kuwa umepelekwa Central ikawaje?
Shahidi wa kificho : Tukaingizwa Ofisi ya RCO nikaambiwa nashitakiwa kwa kosa la kutaka kufanya fujo, niliandikwa maelezo na kuingizwa Mahabusu na asubuhi yake ndugu zangu walinifuata nikazaminiwa na kupewa tarehe za kuwa naenda kuripoti kwenye hicho kituo cha Polisi.
Wakili: Nini kilifuata?
Shahidi wa kificho : Nikawa naripoti kwa mujibu mpangilio wa hiyo ratiba na ilipofika Tar. 17/04 2025 baada ya kufika kuripoti kama kawaida, nikaambiwa naandikwa maelezo upya.