dolevaby
JF-Expert Member
- Aug 25, 2013
- 12,955
- 9,527
Je nyakati tofauti haziwezi kumfanya mtu kuwa na mitizamo tofauti? Najiuliza tu.
Kama kabadili mcmamo anatakiwa Aseme,,,!
Je nyakati tofauti haziwezi kumfanya mtu kuwa na mitizamo tofauti? Najiuliza tu.
Uko very wrong!Extremely wrong!Mie ni CCM, na kabla ya hii thread fuatilia thread zangu nyingine!Kuhusu kitabu huna haja hata ya kuuliza kama mjomba wangu au bibi anayo hiyo PhD!Umri unaniruhusu kutokuwa nayo,ila for sure nitaipata ambayo nina uwezo kuitetea popote!Taifa kwanza u-chama baadae!Wanafiki wapika majungu hamjambo, endelee kuleta mada za kinafiki hapa ili muweze kuganga njaa. Unaposema PHD ya Dk.mwakyembe ni feki baba yako au wewe unayo, acheni unafiki wa kinjaa njaa, Dk.Mwakyembe ni kichwa.Unafiki wenu hauna maana. Kwanza lzm mtumie akili, Dk.Mwakyembe hayasema lolote kuhusu maelezo ya mnafiki wa Chadema LISSU kwa hiyo mnamhukumu Mwakyembe tu kabla yeye hayajibu kitu. Wajinga kweli. Bahati mbaya mnaochangia humu wote asilimi 98 ni mi-Chadema.
Huna Hoja, kaa kimya!Nani kakuambia mie nahusika na Saccoss za mtei!Taifa kwanza!ukweli unauma sana, ni sawa na wewe kuitwa MSUKULE WA MZEE MTEI. kazi unayo
Kipuuzi ndo wapi mkuu!Huna hoja kaa kimya!Hii mada ni ya kipuuzi
Amefanya nini; tufahamisheni tujue.
Tatizo ni kuwa kumnyangaya mtu digrii kunaendana pia na kumwadhibisha mwalimu aliyemsimamia na kutoa mapendekezo kwenye senate kuwa mtu huyo apoewe digrii hiyo. Digirii ya Ph.D hutolewa na chuo kwa mapendekezo ya msimamizi wa mwanafunzi husika; huyo ndiye anayeweza kutoa mapendekezo tena kwa chuo kuwaambia kuwa amepata taarifa mpya zinazooneysha kuwa Mheshimiwa hakustahili rights na privileges za digrii hiyo.
Ni ajabu mtu anapotofautiana na utafiti wake wa kitaaluma uliompatia PHD mara baada ya kuipata hiyo PHD. Ni vigumu kuelewa jambo hili. Dr. Mwakyembe atuambie ama aliiba utafiti huo ama alifanyiwa na mtu mwingine. Tafadhali chuo kilichompatia PHd ni kipi watende haki. Sio bure.
Kichuguu kinataka kusema kama huyo mwalimu aliyesimamia na hatimaye kupendekeza mwanafunzi atunukiwe digrii husika amekwisha kufa, basi hakuna njia nyingine yeyote ya kusawajisha makosa ya aina ya mwakyembe!!!!!!
kama ndivyo basi mfumo huu hauna auto-equilibrium formation.
Wasomi wanashirikiana kuiangamiza dunia yetu. Wataalam wanajitahidi kuitengeneza.
Tafiti ngapi haziendani na uhalisia?? His paper was just an ideal and some time it is very difficult to put into practice. Maana yake ni kwamba siyo kila kitu kinachoandikwa kwenye makaratasi kinaweza kutekelezeka katika mfumo wa maisha ya watu. Usipaniki brother!
njaa noma,polonium 210 bado ipo kwenye ubongo wa mwakyembe..
Kutokana na nukuu zinazoendelea kutolewa na wachambuzi mbalimbali (Hapa namuongelea Lissu) katika mchakato wa katiba mpya, imethibitisha pasipo shaka kuwa Mh. Dr. Mwakyembe anakikana kile alichokiandika miaka ya Tisini ili kupata udaktari wa falsafa (PhD).
Katika kitabu chake alinukuliwa akisema kuwa muundo wa muungano wa Tanzania ni shirikisho pasipo na shaka, na kuthibitisha kuwa migogoro itamalizwa kwa kuwa na serikali tatu! Ni kwa hoja zake hizo aliweza kutunukiwa shahada ya uzamivu (PhD). Sasa kwa kuwa anazikana hoja hizo maana yake ni kuwa alipotosha watu katika utafiti wake!
Aidha aliegemea upande ambao alikuwa anautaka (bias) au aliamua kufuata wengine walisemaje!Sasa kwa kuwa hata yeye hauamini utafiti wake je sio haki yake kuondolewa udaktari wake!?
Prof. Shivji nae ameyakana maandiko yake ya miaka ya 90, ambayo mengine aliyatumia kupanda cheo mpaka kuwa profesor, je nae sio haki yake ashushwe cheo hicho?
Nawasilisha.
Je nyakati tofauti haziwezi kumfanya mtu kuwa na mitizamo tofauti? Najiuliza tu.
Lyimo Mkuu wasomi wanaligharimu sana hili Taifa