Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,320
Aisee jana ilibidi nisherehekee na Valuu 2, pale baba aliponipigia mwenyewe na kusema 'yaani sasa sitaki tena kusikia CCM, hata mama yako amesema kura yake ni kwa Slaa. Nilijisikiliza mara 2 kama ninayosikia ni halisi, maana huyu mzee wangu aliyekuwa kada wa CCM, alikuwa haambiliki siku za mwanzo, na nilikuwa nimeshakata tamaa. Nilipomuuliza nini kimekubadilisha, anaseme amesikitishwa sana na kupanda gafla bei za vitu hasa mafuta ya kula. "Yaani tangu aje Slaa hapa, sijui alileta uchawi gani?, hakuna mtu anataka kusikia CCM, zaidi ya hawa matajiri wenye magari" alimaliza mzee wangu...