SGR imeibua kero kwa wananchi inakopita

samakiurembo

JF-Expert Member
Dec 8, 2021
445
684
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu .

Ujenzi una nia njema kabisa nasi tunapongeza kama wananchi ila changamoto umekuja kutenganisha miundombinu ya kibiashara kijamii kielimu na muingiliano wa kila siku wa watu

Ujenzi wa reli hii umeenda kutenga watu waliokuwa wanaingiliana kila siku katika maeneo hayo niliyotajwa hivyo imepelekea usumbufu kero na kuongezeka kwa gharama kusiko kwa lazima

Makundi yanayoathirika ni

Wafanyabiashara baadhi ya maeneo yaliyotengwa kama masoko au maduka yalikuwa sehemu muhimu ya watu kupata mahitaji yao lakini reli imeenda kuweka uzio na umbali mrefu kulifikia soko au duka hiki ni kilio kikubwa cha wananchi

Kundi la pili watoto wadogo wa shule na wakina mama ambao wanalazimika kwenda umbali mrefu ili kufuata kivuko kilichotengwa kwa mfano eneo la Banana Ukonga Dar es Salaam watoto wadogo inawalazimu watembee umbali mrefu mpaka Majumba Sita na kurudi tena Banana ili wafike shuleni na ni eneo lenye shule zaidi ya sita na zipo eneo la jeshi na wengi wa wanafunzi wanatokea upande uliozibwa wa raia.

Ndani ya week mbili baada ya njia za muda mrefu kufungwa maduka yameanza kufungwa kwa kukosa wateja gharama usafiri zimepanda kwani kwenda kununua dawa ya kikohozi itakulazimu ujumlishe na elfu mbili ya pikpiki

Lengo la kuandika uzi huu ni kujaribu kupata nafasi ya kuwafikia wahusika kwa urahisi kwa JamiiForums ni mtandao mkubwa unaosomwa na wengi

Mapendekezo kuwe na route ya gari kuanzia Pugu kupitia upande wa pili wa reli Hadi Banana ama kuwe na vivuko kama cha Buguruni au Manzese kwa wapita kwa miguu au kuwe na geti kwa raia kupita kwa muda fulani tu kisha geti kufungwa maana wanaoteseka ni wakina mama wanaenda masokoni kuanzia usiku na watoto wanaowahi mashuleni alfajiri.

Nb kilio ni kikubwa wananchi wanateseka
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu...
pointi hii
 
Pointi imewasilishwa kisomi kabisa, serikali ilione hili hata kwa kuweka automatic gates ambazo zitazuia watu pale tu treni inapotaka kupita, au waweke daraja kama la manzese.
 
Una Point Kubwa Sana na yenye Mashiko. Nimependezwa na Mapendekezo tofauti uliyoyatoa, wasiwasi wangu ni wenye kutoa maamuzi kwa maslahi ya wengi watalichukuliaje hili?

Ahsante, Naomba kuunga mkono hoja.👍🤝🙏
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu .

Ujenzi una nia njema kabisa nasi tunapongeza kama wananchi ila changamoto umekuja kutenganisha miundombinu ya kibiashara kijamii kielimu na muingiliano wa kila siku wa watu

Ujenzi wa reli hii umeenda kutenga watu waliokuwa wanaingiliana kila siku katika maeneo hayo niliyotajwa hivyo imepelekea usumbufu kero na kuongezeka kwa gharama kusiko kwa lazima

Makundi yanayoathirika ni

Wafanyabiashara baadhi ya maeneo yaliyotengwa kama masoko au maduka yalikuwa sehemu muhimu ya watu kupata mahitaji yao lakini reli imeenda kuweka uzio na umbali mrefu kulifikia soko au duka hiki ni kilio kikubwa cha wananchi

Kundi la pili watoto wadogo wa shule na wakina mama ambao wanalazimika kwenda umbali mrefu ili kufuata kivuko kilichotengwa kwa mfano eneo la Banana Ukonga Dar es Salaam watoto wadogo inawalazimu watembee umbali mrefu mpaka Majumba Sita na kurudi tena Banana ili wafike shuleni na ni eneo lenye shule zaidi ya sita na zipo eneo la jeshi na wengi wa wanafunzi wanatokea upande uliozibwa wa raia.

Ndani ya week mbili baada ya njia za muda mrefu kufungwa maduka yameanza kufungwa kwa kukosa wateja gharama usafiri zimepanda kwani kwenda kununua dawa ya kikohozi itakulazimu ujumlishe na elfu mbili ya pikpiki

Lengo la kuandika uzi huu ni kujaribu kupata nafasi ya kuwafikia wahusika kwa urahisi kwa JamiiForums ni mtandao mkubwa unaosomwa na wengi

Mapendekezo kuwe na route ya gari kuanzia Pugu kupitia upande wa pili wa reli Hadi Banana ama kuwe na vivuko kama cha Buguruni au Manzese kwa wapita kwa miguu au kuwe na geti kwa raia kupita kwa muda fulani tu kisha geti kufungwa maana wanaoteseka ni wakina mama wanaenda masokoni kuanzia usiku na watoto wanaowahi mashuleni alfajiri.

Nb kilio ni kikubwa wananchi wanateseka
"No problems, No opportunities". Kuna mzee mmoja ameandika hayo maneno kwenye uzi wa ke hapa JF, nakubaliana nayo. Anamaanisha ikiwa hakuna matatizo hakuna fursa, hizo changamoto zote ukizitama kwa mtazamo chanya, zote zinazaa fursa kwa namna moja au nyengine. Tuzitumie fursa hizo, tusikae tunalalamika tu.
 
"No problems, No opportunities". Kuna mzee mmoja ameandika hayo maneno kwenye uzi wa ke hapa JF, nakubaliana nayo. Anamaanisha ikiwa hakuna matatizo hakuna fursa, hizo changamoto zote ukizitama kwa mtazamo chanya, zote zinazaa fursa kwa namna moja au nyengine. Tuzitumie fursa hizo, tusikae tunalalamika tu.
Toa mifano ya baadhi hizo fursa.
 
Toa mifano ya baadhi hizo fursa.
Kufungua maduka mapya kuendana na njia mpya.

Kuhamisha vituo vya daladala kuwa pande zote mbili.

Kuhamishia watoto kwenye shule zisizowalazimu kuvuka reli kila siku.

Tuache malalamiko mitandaoni sababu,hapo walipo kuna Diwani,Mbunge na mpaka uongozi wa wilaya kwa kuanzia.

Maana ya treni ya umeme ni spidi 160KPH.

Sasa bila uzio mnatarajia nini?

Au reli ndio ipishe watu?

Watu wajifunze kuishi kuendana na wakati na mazingira husika.

Tuache kulalamika sababu tu,Duka lako limekosa biashara baada ya uzio kuwekwa.
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu ....
Maduka yamefungwa kwa kukosa wateja! Inamaana huko wanunuzi wanaishi upande mmoja na maduka yako upande mwingine! Kwa uongo huu sijui utasaidiwaje.
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu...
Reli ni kama mpaka, wa huku ni wa huku na wa kule ni wa kule.

Hamieni kuliko na ahueni.
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu ...
Maendeleo yana gharama boss, maadam hiyo Sgr itakuwa na faida kwenu na kwa taifa, basi hizo changamoto ndio gharama mlizolipia ili nchi ifaidike.

Poleni na tafuteni namna nyingine ya kuzoea hayo, maana hiyo reli haiwezi kuhamishwa.
 
"No problems, No opportunities". Kuna mzee mmoja ameandika hayo maneno kwenye uzi wa ke hapa JF, nakubaliana nayo. Anamaanisha ikiwa hakuna matatizo hakuna fursa, hizo changamoto zote ukizitama kwa mtazamo chanya, zote zinazaa fursa kwa namna moja au nyengine. Tuzitumie fursa hizo, tusikae tunalalamika tu.
Ni kweli mkuu, kama hakuna tatizo, hakuna fursa!, maduka mapya, madaraja mapya n.k zote fursa
 
Habari za usiku huu wanaJamiiForums natumai wote ni wazima wa afya.

Bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye hoja ya msing juu ya ujenzi wa reli ya kisasa iliyojengwa na serikali yetu tukufu .

Ujenzi una nia njema kabisa nasi tunapongeza kama wananchi ila changamoto umekuja kutenganisha miundombinu ya kibiashara kijamii kielimu na muingiliano wa kila siku wa watu

Ujenzi wa reli hii umeenda kutenga watu waliokuwa wanaingiliana kila siku katika maeneo hayo niliyotajwa hivyo imepelekea usumbufu kero na kuongezeka kwa gharama kusiko kwa lazima

Makundi yanayoathirika ni

Wafanyabiashara baadhi ya maeneo yaliyotengwa kama masoko au maduka yalikuwa sehemu muhimu ya watu kupata mahitaji yao lakini reli imeenda kuweka uzio na umbali mrefu kulifikia soko au duka hiki ni kilio kikubwa cha wananchi

Kundi la pili watoto wadogo wa shule na wakina mama ambao wanalazimika kwenda umbali mrefu ili kufuata kivuko kilichotengwa kwa mfano eneo la Banana Ukonga Dar es Salaam watoto wadogo inawalazimu watembee umbali mrefu mpaka Majumba Sita na kurudi tena Banana ili wafike shuleni na ni eneo lenye shule zaidi ya sita na zipo eneo la jeshi na wengi wa wanafunzi wanatokea upande uliozibwa wa raia.

Ndani ya week mbili baada ya njia za muda mrefu kufungwa maduka yameanza kufungwa kwa kukosa wateja gharama usafiri zimepanda kwani kwenda kununua dawa ya kikohozi itakulazimu ujumlishe na elfu mbili ya pikpiki

Lengo la kuandika uzi huu ni kujaribu kupata nafasi ya kuwafikia wahusika kwa urahisi kwa JamiiForums ni mtandao mkubwa unaosomwa na wengi

Mapendekezo kuwe na route ya gari kuanzia Pugu kupitia upande wa pili wa reli Hadi Banana ama kuwe na vivuko kama cha Buguruni au Manzese kwa wapita kwa miguu au kuwe na geti kwa raia kupita kwa muda fulani tu kisha geti kufungwa maana wanaoteseka ni wakina mama wanaenda masokoni kuanzia usiku na watoto wanaowahi mashuleni alfajiri.

Nb kilio ni kikubwa wananchi wanateseka
Naunga mkono hoja yako mkuu.Hili ni kero sana
 
Back
Top Bottom