Seriously nimekata tamaa ya maisha.

Seriously nimekata tamaa ya maisha.

ranjan

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2013
Posts
338
Reaction score
288
habari za jioni wanajamvi.naombeni maombi yenu nimeachishwa kazi bila kosa, yaani nimekata tamaa na maisha,ukizingatia ilivyo kazi kupata kazi,najiuliza cjui nimemkosea nini mungu,najiona sina bahati katika dunia hii.
 
Unaelimu gani?,kazi ilikuwa ni ipi?kampuni gani?kabila gani?
 
Pole ndugu yangu ila kumbuka kwenye maisha kuna challenges kibao hio ni mojawapo kwahio usikate tamaa! Hayo ni majaribu Tu!!!
 
Kwanini umeachishwa kazi?
Mkataba wako unasemaje?

Usikate tamaa mkuu, kukata tamaa ni makosa makubwa sana katika maisha ya mwadamu yeyoteyule.
Kumbuka kila kitu hutokea kwasababu.

Nakumbuka nilipitia misuko suko kama yako, nilipo maliza chuo nikapata ajira ndani ya miezi minne wakanizingua nikaa bench karibia mie sita nikaja kupata sehemu ambayo mshahara wake ulikua mara mbili ya ule wa awali..... so hizo ni changamoto tu katika maisha ya binadamu.

Na hivyo ni vitu ambavyo vinaweza kukufanya kua mkomavu haswaa
 
pole sana kazi gan ulikua unafanya? je hukua unajiwekea kiasi kidogo cha pesa ili ujiajiri?
 
The Best Is Yet To Come..!!Be Patient..!!God Never Take Something Good From U Without Replacing With The Best Ones....!!
 
Kwanza wewe ulishakata tamaa. Nakuambia badilika kimawazo. Hukuzaliwa kwenye hiyo ofisi, kufukuzwa bila kosa kuna sheria yake na wewe utapata kazi nyingine bado umri wako mdogo. Kwani ulijua utaipata hiyo kazi???
 
Ndugu yangu hebu fikiria kwamba hiyo kampuni ingekufa au boss ingekufa, je ndio ungekua mwisho wa maisha yako? Amini Mungu yupo na fikiria kuwa riziki hupanda na kushuka.
 
we kweli boyaa
una haki ya kujua sababu ya kuachiwa kazi
kama wasipo kupa sababu nenda kafungue kesii mahakamani
uwadai fidia
mtoto wa kiume unalilia eti huna bahati
 
Pole mkuu' mapito tu hayo!! ila tuambie sababu za kukuachisha lakini pia walifuta taratibu gani kukufukuza? maana naona kama dili lakukupa mahela hilo' sema hujajua tu.
 
Usife moyo ndugu yangu,shukuru mungu umejiunga jf,haya ni maisha tu,tembelea sana jukwaa la business and economic forum kuna vitu vingi vizuri zaidi,nijulishe upo mkoa gani.
 
Jamaa mbona hasemi alikuwa anafanya kazi, ameachishwa kwa misingi ipi. . . .mbona ameleta kilio chake hadharani lakn hataki kujibu queries
 
Pole sana, riziki yako ipo sehemu nyingine usikate tamaa....
 
habari za jioni wanajamvi.naombeni maombi yenu nimeachishwa kazi bila kosa, yaani nimekata tamaa na maisha,ukizingatia ilivyo kazi kupata kazi,najiuliza cjui nimemkosea nini mungu,najiona sina bahati katika dunia hii.
Mkuu nakuo0mba usikate tamaa

Hujui Mungu amekuandikia nini, inawezekana kakuepusha na majanga makuu lakini huwezi jua na inawezekana wewe kuondoka hapo ndio kufungua milango mingine ya mafanikio.

Always mshukuru Mungu kwa kila litakalokutokea maishani na ninaamini iko siku utarudi hapa jukwaani kutuambia kuwa neema imefunguliwa kwenye maisha yako
 
Kuna vyama vya wafanyakazi unashtaki huko lesi onapelekwa mahakamani, ukishind unarudishwa kazini na vompany inapigwa fine ambayo utapewa wewe.
 
wamechana vyeti vyako?

kama bado unavyo vyeti, chukulia kama hapo tulikua tuna volunteer hafu tujipange upya broh.
Mungu hamtupi mja wake.
 
Mkuu nakuo0mba usikate tamaa

Hujui Mungu amekuandikia nini, inawezekana kakuepusha na majanga makuu lakini huwezi jua na inawezekana wewe kuondoka hapo ndio kufungua milango mingine ya mafanikio.

Always mshukuru Mungu kwa kila litakalokutokea maishani na ninaamini iko siku utarudi hapa jukwaani kutuambia kuwa neema imefunguliwa kwenye maisha yako

ukweli mtupu kaka Lukosi. Mungu amjaze nguvu kujana wetu.
 
Jamaa mbona hasemi alikuwa anafanya kazi, ameachishwa kwa misingi ipi. . . .mbona ameleta kilio chake hadharani lakn hataki kujibu queries

Kwa ajira za Tz zlivo kazi kupata, ebu tumfariji kwanza. Kesho atatujibu.
 
Back
Top Bottom