fiksiman
JF-Expert Member
- May 17, 2008
- 402
- 104
Ndio hadi sasa serikali kadhaa zikiwemo za Afrika Mashariki (Tanzania na Uganda) pamoja na Afrika Kusini zimeonyesha kumgwaya Rais wa Sudan Omar Ali Bashir ambaye anatuhumiwa na mahakama kuu ya kimataifa kwa uhalifu dhidi ya binadamu nchini mwake. Akijibu swali la Mbunge wa Viti maalum kutoka Chadema, Mhe. Halima Mdee, naibu waziri wa mambo ya nje, aliweka wazi kuwa Serikali ya Tanzania haitamkamata Rais huyo wa sudan endapo atakuja nchini.
Pia Waziri mmoja pale Uganda aligoma kujibu swali kutoka kwa mwandishi wa BBC swahili alipotaka kujua kama Serikali ya Uganda itamkamata Bashir kama ataingia nchini humo. Waziri huyo alimtupia Mwanasheria Mkuu wa Serikali akidai yeye ndo mwenye wajibu wa kuamua. Hata hivyo baadae aliwaomba waandishi wasubiri mpaka atapofika ndipo itajulikana kama atakamatwa au laa. Uganda ni miongoni mwa mwanachama katika Baraza la Amani la Umoja wa Mataifa.
Afrika kusini nayo ilionuyesha kumgwaya Rais huyo baada ya kumwalika kwenye shughuli za Kuapishwa kwa Rais Jacob Zuma na baadae kumshauri asihudhurie hafla hiyo ili kuepusha mgongana na jumuya ya kimataifa. Yote tisa, kumi ni pale Umoja wa Afrika ulipotoa tamko la kugoma kushirikiana na Mahakama hiyo katika suala la kumkamata Rais huyo kwa kigezo cha kudai kuwa mara nyingi nchi za Afrika hazipewi kipaumbele katika masuala yao hivyo hawaoni kwanini watoe ushirikiano inapotokea wengine wanawahitaji.
Pamoja na masuala yote hakuna kiongozi hata mmoja aliyesimama na kukanusha tuhuma alizipewa Rais Bashir ingawa wameonekana kumkingia kifua kama walivyofanya kwa Komredi Mugabe. Je hii inatoa tafsiri gani kwa wachambuzi wa masuala ya siasa za Afrika?
Pia Waziri mmoja pale Uganda aligoma kujibu swali kutoka kwa mwandishi wa BBC swahili alipotaka kujua kama Serikali ya Uganda itamkamata Bashir kama ataingia nchini humo. Waziri huyo alimtupia Mwanasheria Mkuu wa Serikali akidai yeye ndo mwenye wajibu wa kuamua. Hata hivyo baadae aliwaomba waandishi wasubiri mpaka atapofika ndipo itajulikana kama atakamatwa au laa. Uganda ni miongoni mwa mwanachama katika Baraza la Amani la Umoja wa Mataifa.
Afrika kusini nayo ilionuyesha kumgwaya Rais huyo baada ya kumwalika kwenye shughuli za Kuapishwa kwa Rais Jacob Zuma na baadae kumshauri asihudhurie hafla hiyo ili kuepusha mgongana na jumuya ya kimataifa. Yote tisa, kumi ni pale Umoja wa Afrika ulipotoa tamko la kugoma kushirikiana na Mahakama hiyo katika suala la kumkamata Rais huyo kwa kigezo cha kudai kuwa mara nyingi nchi za Afrika hazipewi kipaumbele katika masuala yao hivyo hawaoni kwanini watoe ushirikiano inapotokea wengine wanawahitaji.
Pamoja na masuala yote hakuna kiongozi hata mmoja aliyesimama na kukanusha tuhuma alizipewa Rais Bashir ingawa wameonekana kumkingia kifua kama walivyofanya kwa Komredi Mugabe. Je hii inatoa tafsiri gani kwa wachambuzi wa masuala ya siasa za Afrika?