Serikali yatuma chopa kuokoa watu waliozungukwa na vimelea vya kipindupindu

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,739
32,874
image.jpeg


Helicopter ya Jeshi la Polisi imetua Mkoani Iringa ili kuwaokoa watu waliozungukwa na maji ya mafuriko yenye vimelea vya Ugonjwa wa kipindupindu katika Tarafa ya Pawaga kwenye vijiji vya Mboliboli,Kimande na Usolanga.

Itakumbukwa hili ni jimbo la Isimani kwa Mbunge na Waziri wa Ardhi ndugu William Lukuvi.

Eneo hili ni maarufu sana kwa ulimaji wa mpunga ktk ukanda wa eneo la Bonde la mto Ruaha.

Serikali ameamuru kufungwa kwa vilabu vya pombe na utengenezaji wa aina yoyote ya Pombe za kienyeji,hali ni mbaya sbb watu wanakunywa maji yenye kinyesi yanayotoka kwenye majaruba ya mpunga.
 
Back
Top Bottom