fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Serikali yatua rasmi
Fidelis Butahe
SERIKALI imesema haiwezi kutoa fedha za kusaidia uendeshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na badala yake, inatafuta mwekezaji wa kuliendesha shirika hilo.
Pia, imesema mkakati ulipo sasa ni kupunguza wafanyakazi 153 wa shirika hilo na kutafuta Dola 700,000 za Kimarekani kwa ajili ya kulipia matengenezo ndege moja iliyopelekwa Afrika Kusini. kwa matengenezo.
Msimamo huo ulitangazwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo, baada ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, kumtaka aeleze mikakati ya serikali katika ukusanyaji wa mapato na uboreshaji wa shirika hilo.
Kamati hiyo ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Zainab Vullu, pamoja na mambo mengine, ilisema moja ya sababu za kuzorota kwa shirika hilo ni Bodi na Menejimenti ya ATCL na kuitaka serikali iivunje bodi hiyo.
Akijibu hoja hiyo, Chambo alisema kwa sasa hali ya ATCL ni mbaya na kwamba hiyo inatokana na kuwa na ndege tatu, moja ikiwa ya kukodi.Kwa mujibu wa katibu mkuu, ni ndege mbili tu kati hizo ndizo zinazomilikiwa na shirika.
"Hivi sasa anatafutwa mbia wa kuendesha ATCL, ila serikali haiwezi kutoa tena fedha kwa ATCL, mkakati ulipo ni huo wa kutafuta mbia na kupunguza wafanyakazi," alisema Chambo,
Alisema serikali pia sasa iko katika mchakato wa kutazama utendaji kazi wa Menejimenti na Bodi ya ATCL na kwamba ikijiridhisha, itachukua hatua stahiki.
Mbali na ATCL wabunge hao pia walitaka kupata ufafanuzi kuhusu mkataba wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) ambayo serikali ina hisa ya asilimia 49 wakati Kampuni ya Rites ya India, ikiwa na asilimia 51 ya hisa.
Akitoa ufafanuzi suala hilo, Chambo alisema serikali ipo katika hatua za mwisho za kununua hisa zote za Rites ili kampuni hiyo iongozwe na Watanzania na kwamba nguvu kubwa itawekwa katika uwekezaji ili kuboresha zaidi usafiri wa reli ya kati.
Pamoja na majibu hayo wajumbe,waliokenaka kutoridhishwa na Mbunge wa Nkasi, Ali Mohammed Kessy (CCM), aliwataka wabunge wenzake wasimbane Chambo kwa kuwa hivi sasa siasa zimeingilia utendaji wa serikali.
"Hapa makatibu wakuu mnawaonea bure, unajua siasa zimekuwa zikiwekwa mbele zaidi kuliko utendaji, kila kitu siasa tu, siasa tu, umefikia wakati wa kuweka fedha mbele siasa nyuma, alisema Kessy.
Fidelis Butahe
SERIKALI imesema haiwezi kutoa fedha za kusaidia uendeshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na badala yake, inatafuta mwekezaji wa kuliendesha shirika hilo.
Pia, imesema mkakati ulipo sasa ni kupunguza wafanyakazi 153 wa shirika hilo na kutafuta Dola 700,000 za Kimarekani kwa ajili ya kulipia matengenezo ndege moja iliyopelekwa Afrika Kusini. kwa matengenezo.
Msimamo huo ulitangazwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo, baada ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, kumtaka aeleze mikakati ya serikali katika ukusanyaji wa mapato na uboreshaji wa shirika hilo.
Kamati hiyo ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Zainab Vullu, pamoja na mambo mengine, ilisema moja ya sababu za kuzorota kwa shirika hilo ni Bodi na Menejimenti ya ATCL na kuitaka serikali iivunje bodi hiyo.
Akijibu hoja hiyo, Chambo alisema kwa sasa hali ya ATCL ni mbaya na kwamba hiyo inatokana na kuwa na ndege tatu, moja ikiwa ya kukodi.Kwa mujibu wa katibu mkuu, ni ndege mbili tu kati hizo ndizo zinazomilikiwa na shirika.
"Hivi sasa anatafutwa mbia wa kuendesha ATCL, ila serikali haiwezi kutoa tena fedha kwa ATCL, mkakati ulipo ni huo wa kutafuta mbia na kupunguza wafanyakazi," alisema Chambo,
Alisema serikali pia sasa iko katika mchakato wa kutazama utendaji kazi wa Menejimenti na Bodi ya ATCL na kwamba ikijiridhisha, itachukua hatua stahiki.
Mbali na ATCL wabunge hao pia walitaka kupata ufafanuzi kuhusu mkataba wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) ambayo serikali ina hisa ya asilimia 49 wakati Kampuni ya Rites ya India, ikiwa na asilimia 51 ya hisa.
Akitoa ufafanuzi suala hilo, Chambo alisema serikali ipo katika hatua za mwisho za kununua hisa zote za Rites ili kampuni hiyo iongozwe na Watanzania na kwamba nguvu kubwa itawekwa katika uwekezaji ili kuboresha zaidi usafiri wa reli ya kati.
Pamoja na majibu hayo wajumbe,waliokenaka kutoridhishwa na Mbunge wa Nkasi, Ali Mohammed Kessy (CCM), aliwataka wabunge wenzake wasimbane Chambo kwa kuwa hivi sasa siasa zimeingilia utendaji wa serikali.
"Hapa makatibu wakuu mnawaonea bure, unajua siasa zimekuwa zikiwekwa mbele zaidi kuliko utendaji, kila kitu siasa tu, siasa tu, umefikia wakati wa kuweka fedha mbele siasa nyuma, alisema Kessy.