Serikali yatangaza Matokeo ya Mtihani Darasa la 7

RUCCI

JF-Expert Member
Oct 6, 2011
1,701
1,714
1.jpg


Baraza la Mitihani la Taifa limetangaza matokeo ya kumaliza elimu ya msingi (PSLE) ambayo yameonyesha ongezeko la ufaulu kwa asilimia 2.

Akitangaza matokeo hayo leo (Alhamisi), Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema jumla wa watahiniwa 555,291 kati ya 789,479 waliofanya mtihani huo wamefaulu.

Amesema idadi hiyo ni sawa na asilimia 70.3 ya ufaulu tofauti na ufaulu wa mwaka jana ambao ulikuwa ni asilimia 67.8

"Hivyo kuna ongezeko la ufaulu kwa asilimia 2.52," amesema Dk Msonde.

Shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema ya mkoani Shinyanga.

Tembelea Hapa=> Link ya Kwanza

Tembelea Hapa=> Link ya Pili

Habari hii imetumika kwenye Kipindi cha JamiiLeo kinachorushwa kila siku jioni katika Channel ya JamiiForums kwenye mtandao wa YouTube.


Kuona kipindi hicho angalia video ifuatayo, acha maoni yako na kisha Subscribe kwenye Channel ya JamiiForums.


 
Wameongezeka wanajua kusoma na kuandika au ni nafasi tu zipo nyingi sekondari.
 
Elimu yetu bana... cha kushangaza ni kwamba wenye hela zao hawakusubiri hata hayo matokeo, watoto wao wameshapata shule siku nyingi.. watoto wa walalahoi ndio wanasubiria kuchaguliwa kwenda shule za kata

Natamani hali irudi kama enzi zetu, shule za serikali ndio zilikua heshima kusoma
 
Back
Top Bottom