Slogan ya "Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania" ilikuwa ni kwa ajili ya kukamilisha malengo ya kwnda kukalia kiti. Kuna taarifa kupitia vyombo vya habari zilielezea kuwa utafiti unaonyesha asilimia 42 ya watoto hapa nchini wamedumaa hawakui. Kutokua vizuri ni kukosa lishe bora. Lishe bora ni sehemu ya "Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania" Kupanda kwa bei ya vyakula hapa nchini ni UZEMBE wa makusudi wa watendaji wa serikali wakati ndiyo hao hao wanaofanya utafiti. Bila shaka utafiti wanaoufanya ni kwa ajili ya kupanda ngazi zao za elimu kutoka digrii ya pili kwenda PhD, lakini tujiulize kwanini UNAUA WATU KWA MAKUSUDI KWA AJILI YA VYEO? Si busara kupanga bei ya SEMBE Peke yake, pangeni bei ya chakula kwa ujumla wananchi wanakufa. Kukosa milo kwa siku kunaongeza UHALIFU, FAMILIA KUHITILAFIANA, KWA UJUMLA NI TISHIO KWA USALAMA WA FAMILIA NA NCHI. Kupatikana kwa chakula cha kutosha huongeza watu kuzaana, utulivu, amani na maelewano. KWA MANTIKI HII SERIKALI INAHUSIKA KWA MAMBO MENGI SANA YA MAISHA YA WATU.
"MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAYAPO"