Serikali yapokea msaada wa kibajeti Sh. 490 bilioni kutoka Umoja wa Ulaya zitakazotolewa kwa miaka 4

PRODA LTD

JF-Expert Member
Oct 20, 2016
1,005
1,333
EU YAISAIDIA TANZANIA: Serikali yapokea msaada wa kibajeti wa Sh490 bilioni kutoka Umoja wa Ulaya zitakazotolewa kwa miaka 4 kuanzia 2017/2018.

======

Umoja wa ulaya kuipa Tanzania Shilingi billion 490 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Fedha.jpg

Umoja wa ulaya umeingia mkataba na serikali ya Tanzania ya kuipatia misaada wa fedha za miradi ya maendeleo kiasi cha shilingi bilioni 490 kwa kipindi cha miaka minne baada ya kuridhishwa mipango wa serikali ya awamu ya tano.

Akizungumza baada kusaini makubaliano hayo, katibu mkuu wizara ya fedha na mipango bwana Dotto James amesema umoja huo utakuwa unatoan shilingi bilioni 120 kila mwaka wa fedha kuanzia mwaka huu wa fedha wa 2017/18,fedha ambazo zitaelekezwa katika miradi ya vipaumbele ikiwemo kilimo,viwanda na afya.

Mkuu wa ujumbe wa umoja wa ulaya nchini na nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki, Bwana Roeland van de Geer amesema licha kuwepo kwa changamoto mbalimbali umoja wa ulaya unahistoria ya muda mrefu na Tanzania, ambapo amesisitiza fedha hizo za msaada zilielekeze katika sekta za kimkakati ikiwemo kilimo na viwanda kwa lengo la kufikia azma ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo 2020.

Chanzo: ITV
 
Hapo ndio uthibitisho kuwa wahisani wameisusa hii awamu ya mungu mtu,tangu awali bajeti yetu ilikuwa ikipewa msaada wa 40% na nchi wahisani wa bajeti,walianzaga kujiondoa mmoja mmoja,leo tunapewa billion 100 kwa mwaka na mazwazwa ya CCM yatasema maendeleo makubwa na raisi anafanya kazi!!
 
Yaani ukiongeza kwenye escrow 183 B unapata hiyo tutakayo powe aiseee!!!

Mbaya zaidi ni ahadi na bado ni 100B kwa mwaka!

Safi sana, namba zitasomwa hadi tukifikia namba za kichina akili lazima zifanye kazi sawasawa!
 
Kupewa misaada sio jambo la kujivunia ni aibu. Waziri wa fedha anayejivunia na kutamka kwa mbwembwe tunapopata misaada iwe Grants au mikopo hafai kuwa waziri wa wizara hiyo!!!
 
Baada ya Tanzania kuonesha kutokuwa tayari kusaini mkataba wa EPA, sasa Umoja wa Ulaya umebuni mbinu mpya ya kumlainisha Rais na Serikali kwa ujumla, sasa Umoja huo umeamua kutoa " Msaada wa Sh. Bilioni 490" kwa kipindi cha miaka 4 ijayo.

Kumbukeni huu ni msaada na si mkopo, sasa serikali imeukubali, na umoja wa ulaya wanajipanga kwa sasa kuja tena rasmi nchini kumshawishi Rais na Serikali ili watie saini mkataba huo wa EPA, kama Tanzania itakuwa bado kichwa ngumu, basi, Umoja huo wa Ulaya utatishia kuufuta huo msaada wa Bilioni 490 kwa kipindi cha miaka 4 kuanzia mwaka huu, ndio maana UMOJA wa ULAYA wamekaa na kutafakari kwa kina na kuona kuwa huo uitwe " MSAADA" ili uweze kufutwa kirahisi ikiwa mambo yao hayatakubaliwa na Tanzania.

Jana, UMOJA wa ULAYA ulisema kuwa, wana Imani kuwa Tanzania, Burundi na Uganda zitatia saini mkataba huo.
 
Siku hizi billioni 490 kwa nchi kama Tanzania is a peanut tena kwa miaka minne.
 
Ki pesa chenyewe kidogo halafu wanatoa kwa mafungu!!! Hivi wanatuonaje?
 
Habari kama hzi huwezi kuwaona buku 7 lumumba fc .....wanafanya kuchungulia tu!

Ova
 
Back
Top Bottom