Kennedy
Platinum Member
- Dec 28, 2011
- 59,109
- 69,563
Leo Bunge kwa Moyo mmoja imeridhia suala la ajira za Kada kama Dereva,Mhudumu na nyingine zinazofanana na hizo kutangazwa na Halmashauri husika pia Usaili kufanyika huko huko kwenye Halmashauri badala ya Sekretarieti ya Ajira. Isipokuwa Kada kama Afisa Kilimo, Mifugo, Misitu, Uvuvi na zinazofanana na hizo Sekretarieti ya Ajira itaendelea kutangaza na kuwafanyia Usaili kama ifanyavyo sasa. Baadhi ya Wabunge wamesema kwa upande mmoja ilikuwa ni kero mtu atoke Songe, Kagera Mbeya na sehemu nyingine kwenda Dar kwa Usaili.