Nakuunga mkono hundred percent ndugu yangu, usanii mkubwa sana wanafanya hawa ndugu zetu wakatoliki. Nina mtoto Bendel Memorial, ada ni shilingi 550,000 tu iliyoandikwa kwenye form. Lakini jumla ya pesa unazotakiwa kulipa, kwa mfano mimi binti yangu yuko form six. Anatakiwa kulipiwa shs 2,250,000!!! Na haijaishia hapo, kapewa na fomu ya kuchangisha yaani mzazi nichangishe kwa marafiki zangu!
Huwezi kuamini eti joho la kuvaa siku ya mahafari ya mtoto anaemaliza form six linalipiwa 100,000! Jamani huu sio wizi kweli!? Sawa ada iwepo na hawezi kuwa 550,000 lakini basi michango ifutwe iwekwe tu kwenye ada. Ada pamoja na michango tulikuwa tunalipa 1600,000.00 kwa term leo imepanda hadi 2,250,000( Plus michango) na wakati huo huo serikali ilitangaza ada zisipande!
Kwa hili serikali ilifanyie kazi, na kwa nini hiyo pesa tuliyolipa term iliyopita isiendelee tu na ki ukweli inatosha kabisa, 1600,000 kwa term ni reasonable na kama walikuwa na mpango wa kupandisha wangetutumia ujumbe toka wakati watoto wanenda kuanza term waliyomaliza ili tujipange. Kiukweli wakatoliki ni wababe sana katika shule zao. Serikali ilifanyie kazi hili ili tulipe ada kama term iliyopita kwa sababu hatukupewa notisi mapema. Mtoto kafunga tarehe 19/12 na anatakiwa 16/01/2016 hilo ongezeko mzazi atoe wapi au wanafikiri tunaziiba wapi, hata mishahara inayoweza kuongezeka kwa ghafla hivyo ni ya wapi?