Serikali yaonya Shule binafsi kuhusu michango

Makini

Senior Member
Dec 23, 2014
154
59
Serikali imeonya wadau wa elimu wanaoendelea kutoza ada ya kujiandikisha na michango mingine kuacha mara moja kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Naibu waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Eng. Stella Manyanya, amesema wakuu wote wa Wilaya na Wakurugenzi wa Miji na Manispaa watahusika katika kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha kuwa agizo la Rais linatekelezwa. Rais Magufuli aliagiza kufutwa kwa michango yote shule ya msingi na Sekondari.

Manyanya pia amewasihi Watanzania kushirikiana na utawala kwa kuripoti aina yoyote ya ukiukwaji wa agizo hilo.

Kuhusu ada elekezi, Kamishna wa Elimu, Prof. Eustella Bhalalusesa amesema Serikali itakuwa na kikao na wamiliki wa shule ili kujadiliana ni kiwango gani kitakachofaa na kisichowaumiza wananchi.

Wakati hayo yakiendelea, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya juu, Jonathan S. Mbwamba, ameendelea kusisitiza kuwa wanafunzi wote waliokidhi vigezo vya kupata mikopo watapatiwa mikopo hiyo. Idadi ya wanafunzi wanaopata mikopo imeongezeka kutoka 13,582 hadi 53,032.
 
Nafikiri sasa mtaelewa alichokuwa anasema Kaunga jana..

Watu wanatakiwa kufatilia ili jambo kwa karibu si ku ngoja mpaka watu walalamike na huu ni udhaifu mkubwa wa kamishina wa elimu!

Yani baada ya kuona malalamiko jana ndio tunaona leo wanaibuka na matamko ...watu wanataka kuona mnafatilia kuhakikisha watu hawakiuki maagizo ya serikali!

Ni aibu kuona watu wana kiuka maagizo ya serikali na huku watendaji wamekaa tuu maofisi bila kifatilia utekelezaji mpaka waone malalamiko ndio wastuke!
Hakika watumishi wengi ni mizigo kabisa...
 
Last edited by a moderator:
Elimu ni sawa na biashara nyingine yeyote huwezi kunilazimisha kutoza ada wanayotaka watu wa serikalini. Huwezi kuniamria shule ya kupekeka mtoto wangu na pesa nilipayo ni jasho langu kama naona maumivu nitapeleka mtoto magufuli schools. Waache wenye hela waanzishe elite schools nasi tutapeleka watoto. Hatuwezi kuendesha nchi kwa matamko wakati kuna sheria.
 
Elimu ni sawa na biashara nyingine yeyote huwezi kunilazimisha kutoza ada wanayotaka watu wa serikalini. Huwezi kuniamria shule ya kupekeka mtoto wangu na pesa nilipayo ni jasho langu kama naona maumivu nitapeleka mtoto magufuli schools. Waache wenye hela waanzishe elite schools nasi tutapeleka watoto. Hatuwezi kuendesha nchi kwa matamko wakati kuna sheria.

Kwani suala la ada elekezi ni tamko tu mtu kaamka nalo. Mbona kuna miongozo ipo siku nyingi, tatizo ni usimamizi ulikuwa mbovu au haukuwepo kabisa, kila mtu alikuwa anajifanyia lwake. Nchi haiwezi kuendeshwa kiholela tu bila kufuata taratibu na miongozo tuliyojiwekea. Hata hizo biashara nyingine uzisemazo hazifanywi kiholela. Mnatakiwa kutii sheria mkuu, Vinginevyo funga shule.
 
Jamani hili la shule mbona kama halijatiliwa mkazo na Serikali. Hivi inakuwaje mtoto anasoma day Primary School eti anatakiwa alipe 4 millioni. Sasa hizo pesa mtu anazitoa wapi??? Kwa kweli shule binafsi zimekuwa na Tozo la juu bila sababu. Nimeshangaa pamoja na agizo la Rais bado wazazi wanatakiwakulipa milioni 4. Kwa mshahara upi? Hiyo Millioni 4 unakuta eti unalazimishwa uniform kila mwaka, vitabu,chakula n.k. Sikatai kwamba bei elekezi ya 150,000 inastahili ila hiyo pesa kwa wakati huu ni ngumu ukizingatia hata mishahara yenyewe. Hizi shule zinaweza kuwa kichocheo cha watu kuwa wezi tunaomba ada elekezi itolewe haraka kama hiyo ya 150,000/= imeonekana ni ndogo sana basi hata 800,000/= kwa mwaka kwa wale wanaotoa chakula na 500,000 bila chakula lakini siyo milioni 4. Tunaomba namba za kutoa malalamiko zitolewe ili wananchi waweze kutoa maoni.
 
Nina watoto wawili mmoja anasoma Precious Blood Sec School na mwingine anasoma Henry Gogarty Sec zote zinamilikiwa na kanisa Catholic ukweli ni kwamba ada na michango mbali mbali ni tishio la kiuchumi kwa wazazi waliopeleka watoto shule hizo.Afadhali Henry Gogarty ada ya mwanzo inaumiza kama michango ya majengo,sijui ada ya maji ya moto lakini Precious Blood kama mzazi hauko vyema nakushauri usimpeleke mtoto pale.

Kwanza kero ya michango ni kubwa kupita maelezo

Pili mwanao usipofikisha wastani wa 86 akifika form 3 uongozi wa shule unakuita mzazi na kukutaarifu mwanao atasoma lakini atajiandikisha katika kituo kingine ili aweze kufanya mthani wa form 4 nia ni kulinda jina la shule.Fikiria mzazi umelipa ada miaka 3 michango ya kufa mtu uongozi wa shule unakutaarifu mwanao atafute kituo au shule nyngine ya kumalizia kidato cha nne.

Serekali imeziachia sana taasisi za dini kujiamulia watakavyo hasa suala la michango mbali mbali.Mfano michango ya majengo ya nini wakati wazazi si wamiliki wa hizo shule,form za wanafunzi wakati wa kujiunga na hizo shule zimefanywa mradi mkubwa.Nakumbuka wakati nampeleka mwanangu mwaka jana wanafunzi waliofanya mtihani kituo cha Arusha walifikia idadi ya 2,768 x 20,000/= ambayo ni sawa na tsh 55,360,000/= idadi iliyotakiwa ni wanafunzi 100 tu huu ni wizi wa mchana kweupe unaofanywa na hizi shule.Bado kulikuwa na kituo cha Kilimanjaro,Dar na Mwanza haya ni mapato makubwa sana yasiyotozwa kodi.Kitendo cha kutoa fomu nyingi sana wakati unajua idadi ya wanafunzi utakayo chukua ni ndogo sana ni sanaa ya ukwapuaji wa fedha za waTanzania bila kujali ugumu wa maisha unaowakabili.Mwanaunzi akichaguliwa mzazi utatakiwa kulipa ada na micngo mbali mbali kiasi cha Tsh 1,700,000/= halafu mwezi wa July ada ya kumalizia isiyopungua 1,000,000/= ukikataa mwanao atakwenda shule za kata ambazo hazina waalimu wa kutosha,motisha ya waalimu,vifaa na maabara hakuna akimaliza kidato cha nne atakuwa mzigo kama mawaziri mzigo wa Kikwete.

Kwakuwa taasisi za dini zina shule nzuri,ifike wakati serekali ikazipatia ruzuku kwakuwa watoto wanaosoma ni watanzania na hizo shule zikaelekezwa kutoza ada za kawaida ambazo hata watoto wa maskini wataweza kumudu.Kinachotokea sasa ni watoto wa watu wenye uwezo tu ndio wenye kuweza kumudu gharama kubwa na watoto wa maskini kuwekwa kando.Ikiwa shule zitapatiwa ruzuku mfano mishahara ya waalimu na wazazi wakati changia gharama nyingine ada inaweza kushuka hadi tsh 500,000/= kwa mwaka ambayo waTanzania wengi wataweza kumudu.
 
Jamani hili la shule mbona kama halijatiliwa mkazo na Serikali. Hivi inakuwaje mtoto anasoma day Primary School eti anatakiwa alipe 4 millioni. Sasa hizo pesa mtu anazitoa wapi??? Kwa kweli shule binafsi zimekuwa na Tozo la juu bila sababu. Nimeshangaa pamoja na agizo la Rais bado wazazi wanatakiwakulipa milioni 4. Kwa mshahara upi? Hiyo Millioni 4 unakuta eti unalazimishwa uniform kila mwaka, vitabu,chakula n.k. Sikatai kwamba bei elekezi ya 150,000 inastahili ila hiyo pesa kwa wakati huu ni ngumu ukizingatia hata mishahara yenyewe. Hizi shule zinaweza kuwa kichocheo cha watu kuwa wezi tunaomba ada elekezi itolewe haraka kama hiyo ya 150,000/= imeonekana ni ndogo sana basi hata 800,000/= kwa mwaka kwa wale wanaotoa chakula na 500,000 bila chakula lakini siyo milioni 4. Tunaomba namba za kutoa malalamiko zitolewe ili wananchi waweze kutoa maoni.

ya nini kuhangaika kulipa hela nyingi hivyo wakati uwezo wako ni mdogo? Mpeleke mtoto wako shule ya serikali hakuna ada wala michango; Ni elimu bure.
 
hivi tumelazimishwa kuwapeleka huko wanapotoza hizo hela kubwa??? shule za bei chee zipo nyingi tu
 
Elimu ni sawa na biashara nyingine yeyote huwezi kunilazimisha kutoza ada wanayotaka watu wa serikalini. Huwezi kuniamria shule ya kupekeka mtoto wangu na pesa nilipayo ni jasho langu kama naona maumivu nitapeleka mtoto magufuli schools. Waache wenye hela waanzishe elite schools nasi tutapeleka watoto. Hatuwezi kuendesha nchi kwa matamko wakati kuna sheria.
Uhuru bila mipaka ni wendawazimu-kila mtu akiwa huru kujipangia alitakalo(mfano ada aitakayo)itakuwa vurugu.Afterall sheria hizi za vidhibiti ada zilikuwepo ni usimamizi tu ulilega,usidhani watu wamekurupuka.Ukiachiwa ufanye utakalo kwa sababu tu unapesa mwisho utataka kununua coco beach ili ujenge shule ya chekechea na kuweka ada pasua kichwa.Hatuhitaji kuwa na taifa la kuabudu wenye pesa bali tunahitaji taifa la watu wanaofata sheria na taratibu za nchi bila kujali financial status zao.
 
Elimu ni sawa na biashara nyingine yeyote huwezi kunilazimisha kutoza ada wanayotaka watu wa serikalini. Huwezi kuniamria shule ya kupekeka mtoto wangu na pesa nilipayo ni jasho langu kama naona maumivu nitapeleka mtoto magufuli schools. Waache wenye hela waanzishe elite schools nasi tutapeleka watoto. Hatuwezi kuendesha nchi kwa matamko wakati kuna sheria.

Na ndiyo maana Serikali inakuja pia mpango maalumu kwamba ni lazima pia basi wewe mwenye shule ulipe kodi kama biashara nyingine zote, kwa maana kinachotokea sasa hivi ni kwamba wenye shule wanafanya kama ulivyosema wewe biashara lkn Kodi ya Serikali hawalipi kwa maana hapo mwanzo serikali ilikuwa inatambua kwamba Shule ni Huduma kwa Jamii na hivyo kutokulipa kodi!
 
ivi kama wew kipato ni kidogo kwan ni lazim umpelek mtoto shule ya ghari??? pelk mtoto ambapo unaweza mudu..tuache mambo ambayo hatuyawezi....wenye shule watafunga shule n majengo bora wafugie nguruwe na c kuwapangia ada
 
Mbona wao waeonesha harusi TBC wakati ni channel ya kitaifa waache na wao c biashara kama biashara zingine. Mtu akikubaliana na bei anapeleka mwanae bana
 
Hapana hakuna aliyetulazimisha lakini kama mzazi mara nyingi utapigana sana kuhakikisha mwanao anapata kilicho bora.Mimi naishi Njiro karibu na shule ya Naura sec naona jinsi wanafunzi wanavyopata shida ya usafiri asubuhi na jioni ukiwa na binti yako unayemjali na kumpenda kwa moyo wako wote kamwe hautopenda kumwona akining'inia kwenye dala dala,akichewa shule,akikosa mwelekeo mzuri wa masomo,akirejea nyumbani hakuna alichojifunza,akipachikwa mimba na madereva au makonda wa dala dala na nk.

Ni wajibu wa serekali kuweka mazingira mazuri ya elimu kwa wananchi wake bahati mbaya watawala wetu hasa awamu za 3 na 4 zilishindwa likatokea ombwe la elimu taasisi za dini zikachukua jukumu la kuziba ombwe hilo ambalo ni faida kwa taifa.

Ndugu yangu waTanzania wanashindwa kushindana katika soko la ajira ya EAC si kwa bahati mbaya ni kwasababu serekali yetu hajawekeza vyakutosha katika sekta ya elimu nchi nyingine zimetambua udhaifu wetu ndio maana zinataka soko la ajira lifunguliwe.Nadhani serekali ya Dr Magufuli inaweza kusaidiana na taasisi za dini katika sekta ya elimu kama serekali inavyofanya katika sekta ya afya.Jambo hili linawezekana kabisa wala si geni.

hivi tumelazimishwa kuwapeleka huko wanapotoza hizo hela kubwa???
 
Naona wanashtuka walalahoi kuamka na kupeleka watoto wao shule zilizobora ili tusiendelee kutawaliwa na familia zao tu.Hata watoto wapewe nafasi.Kama wangekuwa na nia nzuri wangeboresha shule zetu zote za serikali na mishahara na marupurupu ya walimu.

Leo serikali unaona sawa tukichangia majengo yao ambayo serikali ilipaswa kuyajenga lakini wanaona tabu tukichangangia kwenye shule za private.
Waende wakapasue majipu kwenye Tamisemi kwanza
 
Nina watoto wawili mmoja anasoma Precious Blood Sec School na mwingine anasoma Henry Gogarty Sec zote zinamilikiwa na kanisa Catholic ukweli ni kwamba ada na michango mbali mbali ni tishio la kiuchumi kwa wazazi waliopeleka watoto shule hizo.Afadhali Henry Gogarty ada ya mwanzo inaumiza kama michango ya majengo,sijui ada ya maji ya moto lakini Precious Blood kama mzazi hauko vyema nakushauri usimpeleke mtoto pale.

Kwanza kero ya michango ni kubwa kupita maelezo

Pili mwanao usipofikisha wastani wa 86 akifika form 3 uongozi wa shule unakuita mzazi na kukutaarifu mwanao atasoma lakini atajiandikisha katika kituo kingine ili aweze kufanya mthani wa form 4 nia ni kulinda jina la shule.Fikiria mzazi umelipa ada miaka 3 michango ya kufa mtu uongozi wa shule unakutaarifu mwanao atafute kituo au shule nyngine ya kumalizia kidato cha nne.

Serekali imeziachia sana taasisi za dini kujiamulia watakavyo hasa suala la michango mbali mbali.Mfano michango ya majengo ya nini wakati wazazi si wamiliki wa hizo shule,form za wanafunzi wakati wa kujiunga na hizo shule zimefanywa mradi mkubwa.Nakumbuka wakati nampeleka mwanangu mwaka jana wanafunzi waliofanya mtihani kituo cha Arusha walifikia idadi ya 2,768 x 20,000/= ambayo ni sawa na tsh 55,360,000/= idadi iliyotakiwa ni wanafunzi 100 tu huu ni wizi wa mchana kweupe unaofanywa na hizi shule.Bado kulikuwa na kituo cha Kilimanjaro,Dar na Mwanza haya ni mapato makubwa sana yasiyotozwa kodi.Kitendo cha kutoa fomu nyingi sana wakati unajua idadi ya wanafunzi utakayo chukua ni ndogo sana ni sanaa ya ukwapuaji wa fedha za waTanzania bila kujali ugumu wa maisha unaowakabili.Mwanaunzi akichaguliwa mzazi utatakiwa kulipa ada na micngo mbali mbali kiasi cha Tsh 1,700,000/= halafu mwezi wa July ada ya kumalizia isiyopungua 1,000,000/= ukikataa mwanao atakwenda shule za kata ambazo hazina waalimu wa kutosha,motisha ya waalimu,vifaa na maabara hakuna akimaliza kidato cha nne atakuwa mzigo kama mawaziri mzigo wa Kikwete.

Kwakuwa taasisi za dini zina shule nzuri,ifike wakati serekali ikazipatia ruzuku kwakuwa watoto wanaosoma ni watanzania na hizo shule zikaelekezwa kutoza ada za kawaida ambazo hata watoto wa maskini wataweza kumudu.Kinachotokea sasa ni watoto wa watu wenye uwezo tu ndio wenye kuweza kumudu gharama kubwa na watoto wa maskini kuwekwa kando.Ikiwa shule zitapatiwa ruzuku mfano mishahara ya waalimu na wazazi wakati changia gharama nyingine ada inaweza kushuka hadi tsh 500,000/= kwa mwaka ambayo waTanzania wengi wataweza kumudu.

Nakuunga mkono hundred percent ndugu yangu, usanii mkubwa sana wanafanya hawa ndugu zetu wakatoliki. Nina mtoto Bendel Memorial, ada ni shilingi 550,000 tu iliyoandikwa kwenye form. Lakini jumla ya pesa unazotakiwa kulipa, kwa mfano mimi binti yangu yuko form six. Anatakiwa kulipiwa shs 2,250,000!!! Na haijaishia hapo, kapewa na fomu ya kuchangisha yaani mzazi nichangishe kwa marafiki zangu!
Huwezi kuamini eti joho la kuvaa siku ya mahafari ya mtoto anaemaliza form six linalipiwa 100,000! Jamani huu sio wizi kweli!? Sawa ada iwepo na hawezi kuwa 550,000 lakini basi michango ifutwe iwekwe tu kwenye ada. Ada pamoja na michango tulikuwa tunalipa 1600,000.00 kwa term leo imepanda hadi 2,250,000( Plus michango) na wakati huo huo serikali ilitangaza ada zisipande!
Kwa hili serikali ilifanyie kazi, na kwa nini hiyo pesa tuliyolipa term iliyopita isiendelee tu na ki ukweli inatosha kabisa, 1600,000 kwa term ni reasonable na kama walikuwa na mpango wa kupandisha wangetutumia ujumbe toka wakati watoto wanenda kuanza term waliyomaliza ili tujipange. Kiukweli wakatoliki ni wababe sana katika shule zao. Serikali ilifanyie kazi hili ili tulipe ada kama term iliyopita kwa sababu hatukupewa notisi mapema. Mtoto kafunga tarehe 19/12 na anatakiwa 16/01/2016 hilo ongezeko mzazi atoe wapi au wanafikiri tunaziiba wapi, hata mishahara inayoweza kuongezeka kwa ghafla hivyo ni ya wapi?
 
Ada elekizi ni lazima. Ndiyo maana kuna board za kuratibu bei za bidhaa mbalimbali.
 
Jamani hili la shule mbona kama halijatiliwa mkazo na Serikali. Hivi inakuwaje mtoto anasoma day Primary School eti anatakiwa alipe 4 millioni. Sasa hizo pesa mtu anazitoa wapi??? Kwa kweli shule binafsi zimekuwa na Tozo la juu bila sababu. Nimeshangaa pamoja na agizo la Rais bado wazazi wanatakiwakulipa milioni 4. Kwa mshahara upi? Hiyo Millioni 4 unakuta eti unalazimishwa uniform kila mwaka, vitabu,chakula n.k. Sikatai kwamba bei elekezi ya 150,000 inastahili ila hiyo pesa kwa wakati huu ni ngumu ukizingatia hata mishahara yenyewe. Hizi shule zinaweza kuwa kichocheo cha watu kuwa wezi tunaomba ada elekezi itolewe haraka kama hiyo ya 150,000/= imeonekana ni ndogo sana basi hata 800,000/= kwa mwaka kwa wale wanaotoa chakula na 500,000 bila chakula lakini siyo milioni 4. Tunaomba namba za kutoa malalamiko zitolewe ili wananchi waweze kutoa maoni.

Hivi hili suala la SHULE binafsi wazazi wanalazimishwa kupeleka watoto wao huko hata kama hawana uwezo? Si SHULE za serikali zipo?

Kuhusu ada elekezi, serikali isikurupuke kulazimisha wamiliki wa SHULE binafsi kushusha bei ya ada wanazotozwa wazazi badala yake serikali iboreshe SHULE zake kwa kuweka miundombinu rafiki kwa wanafunzi na walimu. Lakini pia waboreshe maslahi ya walimu. Ni hakika walimu wengi watatoka SHULE za private na kwenda SHULE za serikali bila hata kulazimishwa. Watakwenda kuomba kazi wenyewe. Hili pia litazifanya SHULE binafsi kufa the natural death
 
Elimu ni sawa na biashara nyingine yeyote huwezi kunilazimisha kutoza ada wanayotaka watu wa serikalini. Huwezi kuniamria shule ya kupekeka mtoto wangu na pesa nilipayo ni jasho langu kama naona maumivu nitapeleka mtoto magufuli schools. Waache wenye hela waanzishe elite schools nasi tutapeleka watoto. Hatuwezi kuendesha nchi kwa matamko wakati kuna sheria.

Nahisi unaishi kwenye ile himaya ya 'Wapumbavu'. Hakuna serikali ya aina hiyo Dunia hii.
btw. Wewe mwenyewe una elimu ya kiwango kipi? Ni ajabu kuona mtu wa JF anasema elimu ni biashara!
 
Back
Top Bottom