Serikali yabanwa kuhusu vurugu za wamachinga na Tabora

Losambo

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
2,612
864
WABUNGE wameitaka Serikali kutoa maelezo ya vurugu za Machinga zilizotokea mwishoni mwa wiki iliyopita mkoani Mbeya na hatua ya askari wa JKT kambi ya Masange, kuvamia Soko Kuu la Tabora, kuwapiga na kuwajeruhi wafanyabiashara. Ombi hilo lilitolewa jana asubuhi na Mbunge wa Mbozi Mashariki (CCM), Godfrey Zambi, muda mfupi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.
Kwa habari yote Serikali yabanwa vurugu za Mbeya
My take;
Ngoja tusubiri majibu ya serikali hii leo tuone nini itasema, je itagusa kiini cha tatizo au itaendeleza propaganda tena?
Nilishabandika post fulani kuhusiana na tatizo hili kwa ufupi, kiini cha tatizo la Wamachinga Mbeya na kwingineko ni ukosefu wa ajira. Hivyo nitafurahi kama serikali itajikita katika kutoa njia mbadala ilizojipanga za kuwaandalia mazingira mbadala yanayokidhi haja badala ya kukimbilia kuwafukuza kama mbwa tena kwa kutumia maguvu yaliyopitiliza
 
Kiini cha tatizo ni ukosevu wa Ajira kivipi wakati wanaopigwa ni watu waliojiajiri wenyewe. au umachinga sio kazi?
Umachinga ni sekta isiyo rasmi na ni imani yangu watu wengi wamejishikiza huko, sasa serikali kuwafukuza watu hao bila kuwapa ajira ramsi au kuwaelekeza wapi wafanye kazi zao kama awali ndiyo shida ilipo. Hebu fikiria mtu anapata 1000 au 2000 faida kwa siku, inamtosha kwa matumizi yake mwenyewe sasa leo ukimfukuza bila kumpa mbadala wa kupata 1000 au 2000 aliyokuwa akiipata ni lazima ata resist tu na ndivyo serikali yetu inavyofanya.
Sijui kama nipo clear mpaka hapo?
 
Umachinga ni sekta isiyo rasmi na ni imani yangu watu wengi wamejishikiza huko, sasa serikali kuwafukuza watu hao bila kuwapa ajira ramsi au kuwaelekeza wapi wafanye kazi zao kama awali ndiyo shida ilipo. Hebu fikiria mtu anapata 1000 au 2000 faida kwa siku, inamtosha kwa matumizi yake mwenyewe sasa leo ukimfukuza bila kumpa mbadala wa kupata 1000 au 2000 aliyokuwa akiipata ni lazima ata resist tu na ndivyo serikali yetu inavyofanya.
Sijui kama nipo clear mpaka hapo?

Umeeleweka mkuu.
 
Labda watanzania tujimwage barabarani kudai haki zetu, haki yamungu mafisadi hawatendi haki kwa raia
 
Kiini cha tatizo ni ukosevu wa Ajira kivipi wakati wanaopigwa ni watu waliojiajiri wenyewe. au umachinga sio kazi?

"Wanaopigwa"!!! Mkubwa hilo nalo si tatizo????? I think the Government should learn to treat the youth right!!! Or else!!....
 
Bila shaka serekare inafikiri hao wamachinga wametumiwa na CDM kufanya maandamano.
Hii sirikali sasa haina mbinu ingine dhidi ya ile ya kutisha raia kwa kuwaambia 'Tutawaua' mtaozea jela!
 
Back
Top Bottom