Serikali ya Ukawa ikiingia Mdarakani Hazina kweupe

Serikali ya Ukawa ikiingia Mdarakani Hazina kweupe

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,760
MiCCM inafanya kila mbinu kusudi kuweka wakati mgumu kwa serikali ya Ukawa ifikapo mwishoni mwa 2015 itapoingia madarakani na kuwa Serikali mbadala ,kama mtachunguza tokea kuanza kwa BMK hela za hazina zimekuwa zikitumika kwa kiwango kikubwa sana na cha kutisha tena bila huruma.

Sherehe za kukabidhiana maajabu zilizofanyika Dodoma ,zimetumia hela ambayo si ndogo ,kuna hela iliyobaki pale BMK haijulikani nani amekula au kutumia ,miccm wamekuwa wakifanya mikutano isiyo na tija kila kona hela wanayotumia unaweza kutegua inatoka wapi ,kufungua miradi hivi sasa kumekuwa ni jambo kubwa la kufanya sherehe za aina yake ikifuatiliwa na mikutano ,hiyo yote ina gharama na hela inatoka hazina.

Nini lengo la kufanya yote hayo kwa kutumia gharama kubwa ? CCM wanajua 2015 wanaondoka madarakani ,je atakaeingia madarakani aikute hazina kumenona ? Hapana wanafanya kila kitu alimuradi wanahakikisha hazina inakwangurwa na hakubaki kitu ,kwa maana hiyo atakaeingia madarakani atapata taabu sana kuendesha serikali ambayo hazina yake imekauka. watu watarise up na kuhoji maendeleo ,mwishowe ni kwa serikali hiyo kuanguka au kuangushwa.

UKAWA kuweni wenye kuweka rekodi mkiikuta hazina tupe kamata wote ,waweke lokapu mpaka kijulikane !
 
unashangaa hazina ! Mbona kuna watendaji wanajipanga kuondoka hata na computer za vichogo za ofisi ili kukomoa ukawa , lakini sisi hatujali , NI HERI KUANZA UPYA KULIKO KUENDELEA NA Uozo !
 
Ni mtanzania gani mwenye akiri anaweza akaipa nchi ukawa,kwanza viongozi wenu wamefikia ukomo wa kufikiri,elimu ya mwenyekiti wenu ni ndogo sana kuongoza Taifa kama hili,lugha tu inamsumbua sasa ataongoza watu gani?labda awe Raisi wa wanyama but kuongoza binadamu hawezi.
 
Ni mtanzania gani mwenye akiri anaweza akaipa nchi ukawa,kwanza viongozi wenu wamefikia ukomo wa kufikiri,elimu ya mwenyekiti wenu ni ndogo sana kuongoza Taifa kama hili,lugha tu inamsumbua sasa ataongoza watu gani?labda awe Raisi wa wanyama but kuongoza binadamu hawezi.

mkuu mgoroko...hata binadamu ni wanyama pia!...usipaniki moto wa ukawa ukuunguze.
 
Utakuwa moto wa kuni ambao unazimwa kwa maji,labda mbadilishe aina ya moto,kiukweli yule kijana Mbatia ni bonge la kiongozi na ana msimamo but hao wengine mhhh ni sheeeeda.
 
unashangaa hazina ! Mbona kuna watendaji wanajipanga kuondoka hata na computer za vichogo za ofisi ili kukomoa ukawa , lakini sisi hatujali , NI HERI KUANZA UPYA KULIKO KUENDELEA NA Uozo !

Mkuu umenikumbusha Waziri Masha baada ya kugalagazwa na Wenje Nyamagana alienda ofisi ya mbunge na kuondoa hata vitasa alivyoweka kwa kutumia fedha za "mfuko wa jimbo" akiamini ni vyake binafsi.ndivyo walivyo hawa Fisiem
 
Unaota wewe labda ukawa ni kitu gan? Unajua hii nchi ina misingi yake haiwezekan watu wakaamua kuunda kaumoja kao basi tuwakabidhi nchi, kwanza walioungana wenyewe wanakinzana halaf tuwape nchi ...hebu kalale usitupotezee muda yapo mambo ya msingi ya kujadili na sio huo umoja wa kihuni
 
Hela yote ya hazina wameikwapua throughout ESCREW ,sasa wanapuliza SOS kukopa ,matajiri msiwe mazezeta ukikopesha ndio imetoka ,jamaa hawarudi tena serikalini na UKAWA hawatahusika kwa tajiri yeyote atakaeikopesha CCM wachilia mbali nchi za nje na IMF ,UKAWA lazima watoe onyo na mapema ,kwa yeyote yule atakaeikopesha serikali hii inayoelekea kaburini basi ataenda kuidai huko makaburini.
 
Hela yote ya hazina wameikwapua throughout ESCREW ,sasa wanapuliza SOS kukopa ,matajiri msiwe mazezeta ukikopesha ndio imetoka ,jamaa hawarudi tena serikalini na UKAWA hawatahusika kwa tajiri yeyote atakaeikopesha CCM wachilia mbali nchi za nje na IMF ,UKAWA lazima watoe onyo na mapema ,kwa yeyote yule atakaeikopesha serikali hii inayoelekea kaburini basi ataenda kuidai huko makaburini.

Mkiwaonya wasitukopeshe tutatumia njia hii.
ImageUploadedByJamiiForums1419716092.013699.jpg
 
utawala wa mashetani ccm unaenda kuanguka rasmi 2015
 
Back
Top Bottom