Serikali ya Rais Magufuli na Corona

Serikali ya Rais Magufuli na Corona

Swelana

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2016
Posts
430
Reaction score
1,273
Wandugu

Kuna jambo linanitatiza kila siku,naombeni niwaulize mnisaidie.

Rais Magufuli kila apatapo nafasi ya kuzungumza huwa anajisifu kuwa Corona Tanzania imeisha na haipo kabisa na pia kuulezea umma kuwa hana haja ya kuvaa barakoa kwa sababu hakuna Corona.

Hata Leo amelizungumza hilo akitolea mfano kwamba walipokusanyika wote Leo hakuna aliyevaa barakoa na hakuna haja.

Sote tunajua asemacho Rais ni lazima kifuatwe na wote na kinatekelezwa Kwa vitendo.

Ajabu ni kuwa mtu binafsi ukienda baadhi ya ofisi za serikali na zisizo za serikali hurusiwi kuingia bila barakoa,je hizi ofisi zina mdharau raisi?

Watoto wa shule wamefungua shule baada ya ya Rais kutangaza kuwa corona imeisha,lkn wizara ya elimu imetoa mwongozo wa baadhi ya wanafunzi lazima kuvaa barakoa,je wizara imemdharau raisi?

Au tunaweza kusema kuwa corona IPO lakini raisi ni muongo anayehadaa umma?binafsi nashindwa kuelewa,kwani raisi hana uhakika na asemacho?na kama ana uhakika Kwa nini anapuuzwa?

Kila Mara amekuwa akisema Mungu ametusaidia Tanzania,kwani Mungu anaweza ondoa corona Tanzania pekee,?Kwa nini jina la MUNGU analitumia hovyo kila Mara? Ina maana Tanzania ndio tunamwabudu Mungu tofauti na nchi zingine?na huu ujinga umewaingia wajinga wengi hasa kwenye haya makanisa ya wasaka sadaka,utakuta mtu anajigamba kuwa sisi Tanzania tuna MUNGU na corona hatupati na kuna watu wameaminishwa kabisa corona hakuna.

Asanteni,
Swelana.!
 
atoto wa shule wamefungua shule baada ya ya raisi kutangaza kuwa corona imeisha,lkn wizara ya elimu imetoa mwongozo wa baadhi ya wanafunzi lazima kuvaa barakoa,je wizara imemdharau raisi?
Nchi yalaana hii bora iangamie uumbaji mwingine utokee.

 
Za kuambiwa changanya na za kwako.Corona haijaisha ila imepungua
 
Jibu umeliandika hapa.

"Au tunaweza kusema kuwa corona IPO lakini raisi ni muongo anayehadaa umma?".
 
“Kwenye corona tumeweza, hapa tumekutana hatujavaa chochote, unaambiwa usimsogelee Mtu hadi Mita moja, Mkeo au Mumeo utaacha kumsogelea?, mtapataje Mtoto bila kusogeleana, ni mambo ya ajabu,ndio maana tukasema sisi tutaendelea kusogeleana, Mungu anatulinda”-JPM baada ya kurudisha fomu ya kugombea Urais leo Dodoma
#MillardAyoUPDATES
 
Wandugu

Kuna jambo linanitatiza kila siku,naombeni niwaulize mnisaidie.

Rais Magufuli kila apatapo nafasi ya kuzungumza huwa anajisifu kuwa Corona Tanzania imeisha na haipo kabisa na pia kuulezea umma kuwa hana haja ya kuvaa barakoa kwa sababu hakuna Corona.

Hata Leo amelizungumza hilo akitolea mfano kwamba walipokusanyika wote Leo hakuna aliyevaa barakoa na hakuna haja.

Sote tunajua asemacho Rais ni lazima kifuatwe na wote na kinatekelezwa Kwa vitendo.

Ajabu ni kuwa mtu binafsi ukienda baadhi ya ofisi za serikali na zisizo za serikali hurusiwi kuingia bila barakoa,je hizi ofisi zina mdharau raisi?

Watoto wa shule wamefungua shule baada ya ya Rais kutangaza kuwa corona imeisha,lkn wizara ya elimu imetoa mwongozo wa baadhi ya wanafunzi lazima kuvaa barakoa,je wizara imemdharau raisi?

Au tunaweza kusema kuwa corona IPO lakini raisi ni muongo anayehadaa umma?binafsi nashindwa kuelewa,kwani raisi hana uhakika na asemacho?na kama ana uhakika Kwa nini anapuuzwa?

Kila Mara amekuwa akisema Mungu ametusaidia Tanzania,kwani Mungu anaweza ondoa corona Tanzania pekee,?Kwa nini jina la MUNGU analitumia hovyo kila Mara? Ina maana Tanzania ndio tunamwabudu Mungu tofauti na nchi zingine?na huu ujinga umewaingia wajinga wengi hasa kwenye haya makanisa ya wasaka sadaka,utakuta mtu anajigamba kuwa sisi Tanzania tuna MUNGU na corona hatupati na kuna watu wameaminishwa kabisa corona hakuna.

Asanteni,
Swelana.!
'Sote tunajua asemacho Rais ni lazima kifuatwe na wote na kinatekelezwa Kwa vitendo'
Si lazima, na kama ujuavyo,vyote anajikosha akijua hatakosa watakaomtetea kwa nguvu zote kuwa ugonjwa hakuna. Sasa kama wewe mwananchi unajiona sawa na rais ambaye kawekewa uzio wa binadamu wenzake na nyuma ya pazia humsogelei bila ya kupimwa korona, usivae barakoa wala kuosha mikono .
Wenzetu wa Brazil wanaojitambua uwiano wa madaraka, mahakama imeamuru, kila wakati rais wao akiwa katika kadamnasi bila barakoa, atalipa $ 300. Maana rais wao kama wetu, mpotoshaji mkubwa wakati maisha ya walalahoi yanapotea.
 
Wandugu

Kuna jambo linanitatiza kila siku,naombeni niwaulize mnisaidie.

Rais Magufuli kila apatapo nafasi ya kuzungumza huwa anajisifu kuwa Corona Tanzania imeisha na haipo kabisa na pia kuulezea umma kuwa hana haja ya kuvaa barakoa kwa sababu hakuna Corona.

Hata Leo amelizungumza hilo akitolea mfano kwamba walipokusanyika wote Leo hakuna aliyevaa barakoa na hakuna haja.

Sote tunajua asemacho Rais ni lazima kifuatwe na wote na kinatekelezwa Kwa vitendo.

Ajabu ni kuwa mtu binafsi ukienda baadhi ya ofisi za serikali na zisizo za serikali hurusiwi kuingia bila barakoa,je hizi ofisi zina mdharau raisi?

Watoto wa shule wamefungua shule baada ya ya Rais kutangaza kuwa corona imeisha,lkn wizara ya elimu imetoa mwongozo wa baadhi ya wanafunzi lazima kuvaa barakoa,je wizara imemdharau raisi?

Au tunaweza kusema kuwa corona IPO lakini raisi ni muongo anayehadaa umma?binafsi nashindwa kuelewa,kwani raisi hana uhakika na asemacho?na kama ana uhakika Kwa nini anapuuzwa?

Kila Mara amekuwa akisema Mungu ametusaidia Tanzania,kwani Mungu anaweza ondoa corona Tanzania pekee,?Kwa nini jina la MUNGU analitumia hovyo kila Mara? Ina maana Tanzania ndio tunamwabudu Mungu tofauti na nchi zingine?na huu ujinga umewaingia wajinga wengi hasa kwenye haya makanisa ya wasaka sadaka,utakuta mtu anajigamba kuwa sisi Tanzania tuna MUNGU na corona hatupati na kuna watu wameaminishwa kabisa corona hakuna.

Asanteni,
Swelana.!
Ndugu ukisikia utawala wa kidikteta ndio unakuwaga hivyo. Hakuna kuhoji, kila kitu kinalazimishwa na haki ni suala tu la kiongozi atakavyoamka siku hiyo. Tuupinge udikteta kwa nguvu zetu zote.
 
Back
Top Bottom