Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yakana kufunga mipaka

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Ninacho shangazwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hawa Mawaziri wake, kila mmoja kuja na matamshi yake huku serikali ikikana huku waziri wa utalii kupiga marufuku ndege yoyote kuja .

Waziri wa afya Hamad Rashid nae amekuwa akitoa matamko yake pamoja na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar,kukana kuzuiya usafiri wa ndani na nje.
IMG_0547.JPG




Wakati huo huo, wanasema wanaokuja lazima wakae karantini siku 14 kwa gharama zao? Mgeni gani atakae kuja akae karantini kwa siku hizo kwa gharama yake ? Pia hata sisi wazenji tutarudi vipi nyumbani kwa vitisho kwa gharama za karantini?

Kama mnazuia usafiri zuiyeni tu moja kwa moja Lkn sio kutoa vitisho vya karantini, huko ni kwenda kuambukizana, huku tuliko nchi za kigeni tupo karantini majumbani, si ruhusa kwenda hata hospital, unless una tatizo la kupumua.

Sisi kama wazenji watanzania tuna haki ya kurudi nyumbani, kama nchi nyengine zinavyo chukua hatua kuchukua raia wake.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh...!. Juzi nilimsikia Waziri wao wa Afya akitangaza kufunga mipaka ya kimataifa, kumbe hawana mpaka. Mipaka ni ya JMT.
Ni full kujikanyagakanyanga, nilisema, sikusema..
P
 
Ninacho shangwazwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hawa Mawaziri wake, kila mmoja kuja na matamshi yake huku serikali ikikana huku waziri wa utalii kupiga marufuku ndege yoyote kuja .

Waziri wa afya Hamad Rashid nae amekuwa akitoa matamko yake pamoja na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar,kukana kuzuiya usafiri wa ndani na nje.View attachment 1400156



Wakati huo huo, wanasema wanaokuja lazima wakae karantini siku 14 kwa gharama zao? Mgeni gani atakae kuja akae karantini kwa siku hizo kwa gharama yake ? Pia hata sisi wazenji tutarudi vipi nyumbani kwa vitisho kwa gharama za karantini?

Kama mnazuia usafiri zuiyeni tu moja kwa moja Lkn sio kutoa vitisho vya karantini, huko ni kwenda kuambukizana, huku tuliko nchi za kigeni tupo karantini majumbani, si ruhusa kwenda hata hospital, unless una tatizo la kupumua.

Sisi kama wazenji watanzania tuna haki ya kurudi nyumbani, kama nchi nyengine zinavyo chukua hatua kuchukua raia wake.



Sent using Jamii Forums mobile app
Wakumbuke kuna Waziri katamka hadharani mwisho wa kwenda Zanzibar ni March 28, 2020!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid amesema Watanzania walioko nje ya nchi baada ya Jumamosi watasalia waliko.

Bw Rashid amesisitiza kwamba taifa hilo halijafunga mipaka yake.

Waziri aliongeza kusema kuwa waliorudi 130 wapo karantini na baadhi yao hawaonyeshi uzalendo.

Video : Millard Ayo
 
Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid amesema Watanzania walioko nje ya nchi baada ya Jumamosi watasalia waliko.

Bw Rashid amesisitiza kwamba taifa hilo halijafunga mipaka yake.

Waziri aliongeza kusema kuwa waliorudi 130 wapo karantini na baadhi yao hawaonyeshi uzalendo.

Video : Millard Ayo
Najua viongozi wetu wanafanya haya kwa nia njema ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Corona,lakin naona SMZ wanachofanya si haki.kwa mfano tarehe 24 mwez huu nilikwenda kuwapokea wagen wangu wapatao 11 AAKIA,nikakuta uwanjan pale wamewazuia wanataka wakae carantine siku 14,kisa tamko la SMZ la tarehe 23 mwezi la kuwa abiria wote wakiingia ZNZ wakae carantine but kwenye kesi ya hawa marafiki zangu wenyewe waliingia Tanzania kupitia KIA tarehe 14 mwezi huu ,wakapitia Ngorongoro nk baadae wanaamua kuja ZNZ wanaambiwa wakae carantine,wagen walikataa ikabidi wageuke waende DAR,hata Bandarin pia nasikia kesi Kama hii ya wagen wangu zipo nyingi
 
Umejazwa ujinga mwingi na siasa uchwara ,mwishowe umeshindwa kuchuja ujinga wa kuchukua na wa kuacha hivyo ubongo wako kuwaza " negative ". Hilo ni tatizo la kisaikolojia, muone mtaalamu kabla hali haijawa mbaya.
 
Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid amesema Watanzania walioko nje ya nchi baada ya Jumamosi watasalia waliko.

Bw Rashid amesisitiza kwamba taifa hilo halijafunga mipaka yake.

Waziri aliongeza kusema kuwa waliorudi 130 wapo karantini na baadhi yao hawaonyeshi uzalendo.

Video : Millard Ayo
WanZanzibar wana akili kuliko bara. Iweje wazidiwe kete Kwenye Muungano? Wamekaliwa kimabavu.
Hili jambo lanshangaza sana yakhe.
Ushajua nnachokisema ee?
 
Nimesoma habari iliyopo kwenye mtandao wa BBC wamemnukuu Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid, kuwa Watanzania waliopo nje ya nchi wametakiwa kurejea nyumbani kabla ya Jumamosi.

Hapo ndio ninapojiuliza wanaotakiwa kurejea nyumbani ni Wazanzibar au Watanzania?
 
Nilicho kiona mimi kuna mkanyagano baina ya mawaziri wa bara na Zanzibar, kwa mfano waziri wa utalii mwanzo alitamka kuwa wamezuiya ndege, wakati huo huo Tanzania tanganyika kazi kama kawaida, wizara ya anga ndio wenye wajibu wa kuzuia usafiri, Zanzibar ilipata wapi mamlaka? Baadae smz ikalazimika kutoa tamko la kukanusha.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh...!. Juzi nilimsikia Waziri wao wa Afya akitangaza kufunga mipaka ya kimataifa, kumbe hawana mpaka. Mipaka ni ya JMT.
Ni full kujikanyagakanyanga, nilisema, sikusema..
P
Mkuu hii kauli sijaitarajia kutoka kwako. Waandishi wanatakiwa kuchunguza (to verify) kila wanachokiandika. Ikiwa waziri alisema ndege hazitoingia Zanzibar lazima reporting yake iwe hivyohivyo. Wewe unajua, kama anavyojua waziri, kwamba suala la mipaka ni mamlaka ya Jamhuri. Tunapaswa kusema yaliyosema na sio kutasiri (to interpret).
 
Back
Top Bottom