Serikali ya Magufuli ni nini? Ni nani?

Serikali ya Magufuli ni nini? Ni nani?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,154
Reaction score
137,162
Let’s talk about it!

Serikali ya Magufuli ni nini? Ni nani?

Kuna kila aina ya ‘excuses’ ambazo Rais Samia anapewa na baadhi ya watu.

Watu hawa wanadai kuwa Rais wetu huyu anahujumiwa na watu waliokuwepo kwenye serikali ya Magufuli.

Sasa labda ni mimi tu ambaye ndo sielewi. Hivyo nataka/ naomba nieleweshwe.

Hiyo serikali ya Magufuli ni nini? Ni mashine? Ni watu? Ni mbuzi? Ni nguchiro?

Nijuavyo mimi hiyo serikali ya Magufuli ilimhusisha Magufuli mwenyewe pamoja na Samia.

Samia naye ni sehemu muhimu kabisa ya hiyo serikali ya Magufuli.

Rais Samia kuivunja serikali ya Magufuli ni kujivunja na yeye mwenyewe maana hatenganishiki na Magufuli.

Hatenganishiki kwa sababu waligombea wote mwaka 2015 na kugombea tena mwaka 2020.

Samia angeweza kabisa kuamua kutogombea tena baada ya kumaliza muhula wake wa kwanza kama makamu wa Magufuli.

Lakini aliamua kugombea tena na huyo huyo Magufuli mwaka 2020.

Sasa mtu huyo anajitengaje na serikali ya Magufuli?

Help me make sense of this ‘vunja serikali ya Magufuli’ nonsense’.
 
Ni watu wajinga tu kwa katiba tuliyonayo yaani rais hawezi kusema anakwamishwa

Labda aseme anajikwamisha


Yani Gwajima au Ndungai aikwamishe serikali?

Kwa lipi? Kuropoka? Samia ni weak ana mtu anayemkwamisha.
 
Haujawahi kusikia watu wanamlaumu Nyerere hadi leo kwa mambo ambayo wamekua na nafasi ya kuyarekebisha?

Hii naona ni kisingizio tu, mbaya zaidi hata yeye mwenyewe Mama alikiri hadharani kwamba yeye na JPM ni kitu kile kile, hapo alieleweka japo baadhi ya mambo aliyoyafanya yalipingana na kauli yake.

Kwenye hiyo inayoitwa serikali ya JPM wote walikuwepo na walishika nafasi za juu ikapelekea wakamate uskani wa nchi. Unaposema kuondoa uongozi wa JPM sijajua unataka usimike upinzani na ufumue kuanzia chama tawala au ni kubadili watu wote waliopo madarakani?

Nimeona hata TL amesema kweli jemedari na ukatili wake lakini hakuwahi kuwabambikia watu kesi za ugaidi. Nikasema kweli siasa na ukahaba tofauti ni bidhaa tu, lakini siasa ni zaidi ya ukahaba. Usimwamini mwanasiasa yeyote.

Acha tusubirie wajuvi waje kutupa darasa mkuu.
 
Hatuna serikali ya magufuli bali serikali ya jamhuri ya muungano wa TZ.

Tuna Awamu za uongozi ngazi ya rais katika jamhuri ya muungano wa TZ.

Awamu ya 5 ndio ya Magufuli ,sasa ni Awamu ya 6.

Kuna viongozi walikuwepo awamu zilizopita na bado wanaendelea na wengine hawaendelei.

Mh SSH sasa hayupo awamu ya magufuli ,alishaondoka ,enzi za magufuli yeye alikuwa VP.
 
Tuliambiwa Samia anaongozwa kutoka Msoga!

Lakini lawama bado anapewa Magufuli.
Magufuli kashakufa

Yaani uache kufanya mambo yako na uanze kumsingizia marehemu?

Ndio kama watu wanamlaumu Nyerere eti alishindwa kuacha ameweka katiba mpya.

Mtu kaacha kutawala 1985 na kafa 1999 miaka zaidi ya 20 hayupo je waliopo wameshindwa nini kuleta katiba mpya?

Wewe upo sasa Fanya sio kuanza kuwalaumu watu ambao hawapo kwa ubovu wako.
 
Tuliambiwa Samia anaongozwa kutoka Msoga!

Lakini lawama bado anapewa Magufuli.
A paradox. Wanataka wamtetee lakini wanashindwa. Mabaya yote yaende kwa yule aliyeondoka...mazuri yabaki kwake
 
Ni kikundi fulani cha wasukuma wengi na wageni kutoka upande wa kushoto mwa kigoma
 
Kuna watu bado hawataki kukubali nchi kwa sasa ipo chini ya Samia, na kama kuna zuri au baya basi ni la Samia.
 
Back
Top Bottom