Serikali ya Rais Jakaya Kikwete imeelemewa. Imelea matatizo, imeshindwa kuchukua maamuzi stahiki kwa wakati, sasa imeshikwa kila Upande. Ukiachilia suala la Mtwara linalofukuta, sasa suala la Udini linaisumbua, waliruhusu watu wa madhehebu kutukanana, Sheikh aliyepo kwenye hii picha na Mkanda aliotoa hakuchukuliwa hatua, na sasa gazeti hili limeandika habari ya uchochezi, pengine serikali inaogopa kulichukulia hatua kwa kuwa ni la kidini. Inaogopa haikumchukulia hatua huyo anayetajwa kuwa muuaji, lakini pia hata gazeti lenyewe naona limeandika kwa kuwa linajua lipo katika mrengo fulani ili lichukuliwe hatua ni lazima ianzie kwa sheikh. Tulishauri kwa busara, ikaonekana ni mambo ya kupita. Sasa maji ya shingo. Rais aache kufanya utani nchi yetu inaelekea pabaya. Na Kwa mfano gazeti hili na habari iliyopo haina tofuti na ile iliyosababisha MwanaHalisi kufungiwa, lakini serikali imekaa kimya...... Haina msimamo.. .........Nini hatima ya nchi yetu? Mbona mambo haya yanakuja kama utani lakini yanafumbiwa macho?