Chademakwanza
JF-Expert Member
- Jun 11, 2014
- 6,346
- 1,872
Ule mgogoro wa ardhi uliokuwa ukiwahusisha wananchi na kiwanda cha Cement cha wazo hatimaye umekwisha rasmi.
Na hii imetokana na juhudi binafsi zilizofanywa na mbunge matata Halima Mdee kwa kushirikiana na madiwani makini.
Wa chadema Janeth Rithe, Deus Mtiro na Esther Samany ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa wakilaumu serikali kwa kuendelea kumkumbatia mwekezaji wa kiwanda hicho bila kuwajali wananchi ambao ni watanzania.
Hatimaye leo saa 7:00 mchana waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi pamoja na naibu wake walifika eneo la Chasimba wakiwa sambamba na timu nzima ya wizara hiyo iliyoongozwa na katibu mkuu wa wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi na hatimaye wamekubali kuwa wananchi wa chasimba,chachui na chatembo wataendelea kuwepo hapo maisha yao yote.
Hongera Halima Mdee, Janeth Rithe, Samanya waziri kwa kusikia kilio cha wananchi
Na hii imetokana na juhudi binafsi zilizofanywa na mbunge matata Halima Mdee kwa kushirikiana na madiwani makini.
Wa chadema Janeth Rithe, Deus Mtiro na Esther Samany ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa wakilaumu serikali kwa kuendelea kumkumbatia mwekezaji wa kiwanda hicho bila kuwajali wananchi ambao ni watanzania.
Hatimaye leo saa 7:00 mchana waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi pamoja na naibu wake walifika eneo la Chasimba wakiwa sambamba na timu nzima ya wizara hiyo iliyoongozwa na katibu mkuu wa wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi na hatimaye wamekubali kuwa wananchi wa chasimba,chachui na chatembo wataendelea kuwepo hapo maisha yao yote.
Hongera Halima Mdee, Janeth Rithe, Samanya waziri kwa kusikia kilio cha wananchi