Serikali ya CCM yakata tena mishahara ya walimu

Serikali ya CCM yakata tena mishahara ya walimu

YUDITHA

Senior Member
Joined
May 5, 2013
Posts
154
Reaction score
28
Serikali imekata mishahara ya walimu ktk viwango tofauti tofauti bila kutoa sababu za msingi za makato hayo.
Ikumbukwe kuwa mshahara ni haki ya mtumishi.

Kwa kitendo hicho serikali ya inajidhirisha ni kinara wa wizi. Kuna watu wamekatwa elfi 60,wengine 25 na wengine 14 huu ni wizi wa waziwazi. Wasiporejesha mshahara wangu natangaza wazi naiburuza serikali mahakani.

Ikiwa wamekata ktk ujenzi wa maabara, waniambie kodi ninayolipa kila mwezi zaidi ya 68 elfu inaenda wapi?

Je, wabunge waliocheza kitolondo bungeni wamekatwa shilingi ngapi?
 
YUDITHA

Pole sana hii inauma sana. Mimi kama muajiriwa na mlipa kodi inaniuma sana kwa ushenzi kama huu wa serikali ya kihuni. Haiwezekani kwa kodi zote tunazolipa ukate mshahara wa mwalimu eti kwa kuwa Rais ametoa amri ya kujenga maabara kwa kila sekondari. ni wizi na uhuni wa wazi wazi. hilo ni jukumu la serikali, nimekwenda shmbani weekend naambiwa na mwenyekiti wa kijiji eti nichangie maabara.

Tena wenye mashamba eti watapewa barua na kuamriwa kulipa kiasi atakachopanga mkurugenzi. nimemwambia akinifuata tena nitamchapa makofi. Nimeshilipia maabara nyingi sana kwa kodi ninayokatwa sichangii tena mabaradhuli hawa wale hela ya jasho langu.

Walimu huu ni mtihani kwenu, ninyi ndio mmekuwa wasaliti wa kubwa, sasa acha tuwaone mkitumika kuichangia CCM.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana ndugu hiyo ndo sura hali ya ccm hizo wanazohubiri majukwani ni zuga. We ushaona wapi nusu ya serikali wapo nje ya nchi kwa wakati mmoja?raisi yupo na delegation yake vietnam na waziri mkuu na delegation yake wapo oman.
 
Nchi ishauzwa! WaTZ wenyewe hatujielewi na mafisadi wanatumia mwanya huo huo wa Amani yetu idumu...
 
Ayaaaaaaaaaaaaaa! kwa hili jamani walim tusikubali, kwanza jamaa alishasema kura zetu haziongezi chochote kwake, tuamken jaman najua wanaharakati na wapenda haki watatuunga mkono,kwa hili nko tayari kutoka jicho, jaman wanaharakati njooon mtusaidie juu ya hili swala na wapenda haki wote tuungane pamoja kuliangusha dubwana ccm, msifikili walim wote tuyaaunga mkono haya mainterahamwe yametunyanyasa vya kutosha,kura zutu hawazipati ng'oo! labda za walim mazuzu pamoja na mafisad wenzao.
 

Kutokana na issue inayoendelea MSD,madaktari na manesi wajiandae kukatwa kwa ajili ya dawa.

Wanajeshi nao wakae mkao wa kula maana tunahitaji jeshi la kisasa.

Hivi haya yanafanyika mpaka nchi jirani ya Zanzibar au huko maabara zinatosha?

Tungekuwa na upinzani wa kweli nchi hii then hii ingekuwa karata yao kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa lakini walivyo vilaza watang'ang'ania vitu ambavyo havimuathiri raia wa kawaida moja kwa moja mfano serikali tatu.
 
Ninamshukuru Muumba mbingu na nchi kwa sababu haya yanatokea wakati huu karibia na chaguzi zenye turufu kwa mwananchi mnyonge wa nchi hii. Huyo ni Mungu wetu anatuasa kufanya maamuzi magumu, kumbukeni kwa wale wasomaji wa biblia Mungu alipoona wana wa Israel wanaanza kusita kuondoka Misri kama mpango wake ulivyokuwa akawaongezea suluba kutoka kwa Farao yule mpya aliyekuwa hamjui Yusufu wala Musa. Yote ilikuwa ni kuwaandaa wana wa Israel kuanza safari waliyoiona ngumu.
Ndipo sasa Mungu wetu kwa upendo mkubwa kabisa anatuandaa kwa ukombozi kutoka kwenye makucha ya mafisadi wakisaidiwa na CCM. Wee Mwalimu inuka sasa, wee mfanyakazi inuka sasa na kuhakikisha unakuwa tayari na halali kupiga kura kuanzia serikali za mitaa hadi uchaguzi Mkuu mwakani. Kumbukeni uandikishaji wa daftari la uchguzi wa serikali za mitaa unaweza kuanza wakati wowote na tunalazimika kufuatilia kwa viongozi wa serikali za mitaa kwani hawakawii kuendesha zoezi kinyemela.
Yatupasa kushikamana na kumjua mtesi wetu ili tumpelekee ujumbe kuanzia uchaguzi ujao. Kataa kuonewa e mwananchi.
 
Wakuu wa Wilaya nao wakatwe mishahara ya kujenga ofisi za wakuu wa wilaya katika wilaya mpya 19 pia wakuu wa Mikoa kujenga ofisi za mikoa mipya minne madaktari na manesi nao wakatwe kununulia dawa hapo angalau tutaona kuna kausawa isiwe waalimu peke yao kuchangia ujenzi wa miundombinu ya sekta yao
 
YUDITHA

Pole sana hii inauma sana. Mimi kama muajiriwa na mlipa kodi inaniuma sana kwa ushenzi kama huu wa serikali ya kihuni. Haiwezekani kwa kodi zote tunazolipa ukate mshahara wa mwalimu eti kwa kuwa Rais ametoa amri ya kujenga maabara kwa kila sekondari. ni wizi na uhuni wa wazi wazi. hilo ni jukumu la serikali, nimekwenda shmbani weekend naambiwa na mwenyekiti wa kijiji eti nichangie maabara.

Tena wenye mashamba eti watapewa barua na kuamriwa kulipa kiasi atakachopanga mkurugenzi. nimemwambia akinifuata tena nitamchapa makofi. Nimeshilipia maabara nyingi sana kwa kodi ninayokatwa sichangii tena mabaradhuli hawa wale hela ya jasho langu.

Walimu huu ni mtihani kwenu, ninyi ndio mmekuwa wasaliti wa kubwa, sasa acha tuwaone mkitumika kuichangia CCM.

Ndugu yangu hapo kwenye red umenena, mimi sijaelewa kabisa kwa mwalimu kukatwa mishahara yao ili wachangie ujenzi wa maabara, kwa kifupi huu mtindo siku zote umekuwepo na hakuna hata maelezo ya hao wahusika kuwadhibitishia walimu kuwa kweli pesa wanayokatwa inaenda huko, lakini kodi zinaenda wapi?, ndio maana tumasema Rais sio mfalme wa enzi zile za watu wa stone age iweje aamulishe kujenga maabara bila kuwa na pesa ya kujengea hizo maabara..................UPUUUUUUUUZI MTUPU.................WALIMU AMUKENI IONDOENI HII SERIKALI WA MAJAMBAZI.
 
Serikali imekata mishahara ya walimu ktk viwango tofauti tofauti bila kutoa sababu za msingi za makato hayo.
Ikumbukwe kuwa mshahara ni haki ya mtumishi.

Kwa kitendo hicho serikali ya inajidhirisha ni kinara wa wizi. Kuna watu wamekatwa elfi 60,wengine 25 na wengine 14 huu ni wizi wa waziwazi. Wasiporejesha mshahara wangu natangaza wazi naiburuza serikali mahakani.

Ikiwa wamekata ktk ujenzi wa maabara, waniambie kodi ninayolipa kila mwezi zaidi ya 68 elfu inaenda wapi?

Je, wabunge waliocheza kitolondo bungeni wamekatwa shilingi ngapi?

sisi halmashauri yetu ya nkasi - rukwa tumeambiwa wachangisha watakuja maeneo tunayoishi sasa mimi nasubiri waje wanikamate wanipeleke ndani then sitaki kudhaminiwa bali nataka nipelekwe mahakamani nikasomewe kifungu cha sheria ndipo nihukumiwe lakini hela ya maabara siko tayari kutoa.
 
lazima kila mtu achangie elimu hii ni msharagamba. ole wake mwanachi yeyote agome kuchangia maabara tutawafunga wote
 
YUDITHA

Walimu huu ni mtihani kwenu, ninyi ndio mmekuwa wasaliti wa kubwa, sasa acha tuwaone mkitumika kuichangia CCM.
Waalimu hamjawahi kujitambua na kutumia wingi wenu kuleta mabadiliko katika nchi hii. Mmekuwa mkitumika kuiba kura makabaki mnachekacheka tu. Mlidhani wakishaiba kura si lazima waibe na hela yenu?
Shame on you teachers maana mpaka leo kuna mwalimu anashabikia magamba, sijui ualimu hamkuupata kwa kuusomea? ni kama hamkustahili!
 
Hakuna kitu kama hicho. Acheni uzushi. Msitake kutumia matatizo ya walimu kwa manufaa ya kisiasa. Serikali ya ccm haiwezi kufanya hayo. Nitajie mwalimu angalau mmoja aliyekatwa mshahara wake
 
Waalimu hamjawahi kujitambua na kutumia wingi wenu kuleta mabadiliko katika nchi hii. Mmekuwa mkitumika kuiba kura makabaki mnachekacheka tu. Mlidhani wakishaiba kura si lazima waibe na hela yenu?
Shame on you teachers maana mpaka leo kuna mwalimu anashabikia magamba, sijui ualimu hamkuupata kwa kuusomea? ni kama hamkustahili!
Poleni sana Mkuu. Walimu wa Tanzania ni watu makini sana. Nyie ukawa hamuwezi kuwatumia kisiasa namna hiyo
 
Walimu endeleni kukipa kura chama cha mapinduzi. Kwani mapinduzi maana yake ni nini? Kama sio hayo mnayoyashuhudia kwa vitendo?
Kura ya maoni ya katiba yenu walimu na magamba ishapitishwa so muendelee kukithamini chama chenu la sivyo kitawanyima kusimamia uchakachuaji wa kura ya maoni na uchaguzi mkuu mwakani
 

Kutokana na issue inayoendelea MSD,madaktari na manesi wajiandae kukatwa kwa ajili ya dawa.

Wanajeshi nao wakae mkao wa kula maana tunahitaji jeshi la kisasa.

Hivi haya yanafanyika mpaka nchi jirani ya Zanzibar au huko maabara zinatosha?

Tungekuwa na upinzani wa kweli nchi hii then hii ingekuwa karata yao kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa lakini walivyo vilaza watang'ang'ania vitu ambavyo havimuathiri raia wa kawaida moja kwa moja mfano serikali tatu.


Upinzani wakweli unaoutaka niule utakaoludisha hela uliyokatwa na Ccm au?waliwaambia muanze migomo mlifanyanini zaidi yakuingia shimoni? Wakiitisha maandamano huwa mnatokea?.Mimi nasema tena acha wawakate tena ikiwezekana wachue zote labda mtaamka!
 
Acheni wawakate na ikiwezekana wasiwalipe kabisa maana Waalimu ndio mnaidekesha CCM
 
Back
Top Bottom