Serikali vs Malipo ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii

Serikali vs Malipo ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii

Toosweet

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2012
Posts
2,140
Reaction score
1,982
Heshima Kwenu,

Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ametoa taarifa kuwa serikali imelipa deni la zaidi ya Tsh. Trilioni moja kwa mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kumekuwa na malalamiko kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii haina fedha za kutosha kulipa wanachama wake kwa kuwa nyingi ya fedha zake zimekopwa na serikali na hazijalipwa kwa wakati.

Jambo la kusikitisha ni kuwa serikali imelipa fedha hizo ili eti mifuko ya hifadhi ya jamii iweze kutimiza lengo/sera ya serikali ya Tanzania ya viwanda. Huu ni upotoshaji. Lengo kuu la kuanzisha mifuko ya hifadhi ya jamii si kufungua viwanda. Ni kutunza na kukuza fedha kwa minajili ya kulipa mafao.

Aina ya uwekezaji na mahali pa kuwekeza si kazi ya serikali. Ni jukumu la mifuko.
 
Acheni kuna watu hawajapewa viinua migongo vyao mpaka leo.
Akili nyingi mbele giza
 
Ndiyo inakuzwa kwa kuwekeza kwenye viwanda.
Si kwa amri ya serikali. Ni uamuzi ,mipango ya mifuko.Investment ya viwanda ni massive. Ni capital intensive. Returns zake zinachukua muda mrefu. Kuna uwezekano wa hasara pia.
 
Heshima Kwenu,

Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ametoa taarifa kuwa serikali imelipa deni la zaidi ya Tsh. Trilioni moja kwa mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kumekuwa na malalamiko kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii haina fedha za kutosha kulipa wanachama wake kwa kuwa nyingi ya fedha zake zimekopwa na serikali na hazijalipwa kwa wakati.

Jambo la kusikitisha ni kuwa serikali imelipa fedha hizo ili eti mifuko ya hifadhi ya jamii iweze kutimiza lengo/sera ya serikali ya Tanzania ya viwanda. Huu ni upotoshaji. Lengo kuu la kuanzisha mifuko ya hifadhi ya jamii si kufungua viwanda. Ni kutunza na kukuza fedha kwa minajili ya kulipa mafao.

Aina ya uwekezaji na mahali pa kuwekeza si kazi ya serikali. Ni jukumu la mifuko.
Mkuu hii taarifa ni ya lini.
 
Nina ndugu yangu amestafuu tangu tarehe 04.03.2017 akiwa mwnachama wa pspf lakini had I Leo tarehe 19.10.2017 hajalipwa mafao yake , anasema kuwa wanasubili afe ndio wapate sababu ya kutumia Fedha zake.kweli inauma sana.
 
Waziri Mkuu analeta siasa kwenye madai na haki za wanachama wa mifuko ya jamii. PPF wanadai Wizara Ujenzi na Uchukuzi pesa za wastaafu ATCL lakini hadi leo hakuna kilicholipwa japo Katibu Mkuu Ikulu alishatoa maelekezo ya kulipa. Waziri Mkuu awe mtendaji wa kusimamia wizara zote na si kutangaza siasa kwenye haki za watu.
 
Back
Top Bottom