Oppomall
JF-Expert Member
- Feb 8, 2017
- 3,496
- 3,595
Salaam wakuu,
Nijielekeze kwenye hoja.
Serikali ilikuja na Mpango mzuri sana wa kukusanya kodi za majengo kupitia matumizi ya Umeme (Luku)
Ulikuwa ni mpango mzuri sana kwakua hakuna mtu anayeweza kukwepa kutumia umeme na hakuna anaeweza kuacha kununua umeme for a life time.
Hata kama akinunua mara moja wa mwaka mzima malimbikizo yake atayakuta tu.
Sasa changamoto imekuja baada ya Serikali kupandisha kodi kutoka ile 27,000 ya zamani hadi 350,000/=
Kwanza hii gharama haijaangazia vipato vya wananchi na haijalenga kuwasaidia walipa kodi.
Pili,imewafanya Wananchi wengi kughaili ama kuchelewa kuingiza umeme maana hapo utakuta kuna gharama zingine kama nguzo kwa walio mbali, ufundi,wiring,vifaa vya ndani nk.
Hao wananchi wanapoacha kuingiza umeme ama kuchelewa ifahamike kuwa Majengo yao yanakaa bila kulipia kodi na Serikali inapata hasara,aidha wengine wanaenda mbali zaidi wanachukua Umeme wa jua kutoka Makampuni ya kukopesha kisha wanalipa kidogo kidogo,suala la kodi halipo tena hapo.
Ushauri wangu, litizameni hili kwa manufaa na maslahi mapana ya Taifa letu.
Nawasilisha.
Nijielekeze kwenye hoja.
Serikali ilikuja na Mpango mzuri sana wa kukusanya kodi za majengo kupitia matumizi ya Umeme (Luku)
Ulikuwa ni mpango mzuri sana kwakua hakuna mtu anayeweza kukwepa kutumia umeme na hakuna anaeweza kuacha kununua umeme for a life time.
Hata kama akinunua mara moja wa mwaka mzima malimbikizo yake atayakuta tu.
Sasa changamoto imekuja baada ya Serikali kupandisha kodi kutoka ile 27,000 ya zamani hadi 350,000/=
Kwanza hii gharama haijaangazia vipato vya wananchi na haijalenga kuwasaidia walipa kodi.
Pili,imewafanya Wananchi wengi kughaili ama kuchelewa kuingiza umeme maana hapo utakuta kuna gharama zingine kama nguzo kwa walio mbali, ufundi,wiring,vifaa vya ndani nk.
Hao wananchi wanapoacha kuingiza umeme ama kuchelewa ifahamike kuwa Majengo yao yanakaa bila kulipia kodi na Serikali inapata hasara,aidha wengine wanaenda mbali zaidi wanachukua Umeme wa jua kutoka Makampuni ya kukopesha kisha wanalipa kidogo kidogo,suala la kodi halipo tena hapo.
Ushauri wangu, litizameni hili kwa manufaa na maslahi mapana ya Taifa letu.
Nawasilisha.