Kiumbe duni
Senior Member
- Dec 3, 2011
- 100
- 8
Kumekuwa na tabia ambayo imejitokeza na inayozidi kushika kasi pale ambapo yanapotokea maafa kuna baadhi ya medi na kampuni binafsi kujifanya ni waungwana sana na kuhamasisha wananchi kuchangia kupitia vyombo vyao. Serikali inajua jinsi Watanzania tusivyokuwa waaminifu, halafu inaruhusu (media,kampuni za simu za mkononi) binafsi kuendesha michango hii. Serikali hii inajua jinsi haya makampuni ya simu yanavyochakachua masalio yetu na kuendesha bahati nasibu za kizushi halafu inakaa kimya tuendelee kuibiwa. Serikali anzisheni utaratibu maalum yanapotokea maafa wananchi hata walio mbali waweze kuchangia moja kwa moja kupitia kwenu hivi vyombo binafsi viwe vinahamsisha tu, sio kuchukua michango. Wanachangisha kwa maslahi binafsi hawana wema hawa, Kama wameweza kuwaibia uso kwa uso wasanii wa muziki wa kizazi kipya sembuse sisi tunaochangi kwa kutumia simu za mkononi!. Wadau nawasilisha...