Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally, Katibu Mkuu mstaafu ndugu Yusufu Makamba, Spika mstaafu Pius Msekwa na viongozi mbalimbali wa dini kwa nyakati tofauti wamejitokeza kukemea vitendo vinavyofanywa na viongozi hasa vijana wenye umri mdogo kuwa wanaenda kinyume na maadili ya jamii.
Akiungana na Katibu Mkuu Spika wa bunge mstaafu na aliyekuwa Makamu Mkiti wa CCM Pius Msekwa amesema,
“Katibu Mkuu yuko sahihi. Sisi wakati wetu tulikuwa na vyuo vya chama kwa ajili hiyo. Kulikuwa na chuo cha Kivukoni ambacho kilianzishwa tangu wakati wa uhuru kwa madhumuni ya kuwaandaa viongozi baada ya uhuru.”
Naye katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba amesema viongozi wengi vijana wa sasa hawana staha, adabu na heshima.
“Ukitoa hoja zako, kwa sababu hawana staha na hawana adabu, hawana heshima watakufuatilia wewe. Ndiyo maana siku hizi tunaogopa kuzungumza na vyombo vya habari,” alisema Makamba.
Ukiacha RC Makonda anayejadiliwa sana, viongozi wengine vijana ambao wengi ni wakuu wa wilaya, wamekuwa wakishutumiwa kwa kuwaweka rumande watumishi wa umma, wananchi na wengine kukwaruzana na wawekezaji na watendaji wa serikali.
Wengi wa vijana hawa (wanaokemewa) ni zao la Jumuiya ya Umoja wa vijana wa CCM UVCCM. Maadili yanayofundishwa ndani ya UVCCM ya leo ya kina Shaka ni tofauti kabisa na maadili yaliyokuwa yanafundishwa na UVCCM iliyowazaa kina Kikwete, Lowassa, ni tofauti na UVCCM ya kina Guninita, kina Nchimbi, Nape na kadhalika.
Ukipandacho ndicho ukivunacho.
Miaka ya hivi karibuni imekuwa ni jambo la kawaida kukuta mitandaoni vijana wakiandika maandishi ya hatari ya kudhuru binadamu mengine ya kuhatarisha usalama wa nchi bila kuchukuliwa hatua na vyombo vya usalama, na ukifuatilia aliyeandika utaambiwa ni kiongozi wa UVCCM mkoa au wilaya, hawa ndio viongozi wanaotegemewa pengine kuwa marais au mawaziri.
Jamii imekuwa ikikemea vitendo hivi bila mafanikio, bila viongozi wa Chama na serikali kuingilia kati, badala yake wameonekana wakiongezewa vyeo. Matokeo yake wanajawa na viburi na kupelekea kutenda vitendo vya ajabu katika jamii.
Siku hizi ukitaka kudhuru kimbilia UVCCM, ukitaka kutukana kimbilia UVCCM, ukitaka kuanzisha gazeti la kutukana na kukashifu kimbilia UVCCM hakuna chombo chochote kitakachokuuliza, nje ya hapo utashukiwa kama mwewe.
Vitendo hivi vikiachwa bila kukemewa tutazalisha taifa la ajabu sana siku zijazo, hawa vijana wanaoachwa wafanye watakavyo kuna siku ndoto zao hazitatimizwa na chama watazitafuta nje ya chama.
Ni wito kwa viongozi mbalimbali, wazee, wastaafu, viongozi wa dini, vyombo vya serikali na jamii kwa ujumla, kujitokeza waziwazi kukemea vitendo hivi, tuwaunge mkono makatibu wa CCM, Askofu Shoo, Freeman Mbowe, Msekwa, Waziri wa Afya Ummy, walioanzisha vita hii kukemea vitendo vinavyofanywa na viongozi vijana vilivyo kinyume na maadili ikiwemo, ubaguzi, uonevu, kuingilia taaluma na fani za watu kwenye maeneo wanayoyaongoza.
Kitengo cha usalama wa Taifa, TISS kina wajibu wa kuchunguza viongozi wa kitaifa wanaoandaliwa, taifa likipata kiongozi asiye na maadili, atakayeliharibu taifa TISS hawatakwepa lawama. Chama cha Mapinduzi kwa upande wake hakinabudi kuhakikisha vijana wake hawakiuki maadili na kama kitengo kiafuata katiba yake na malengo ya kuanzishwa kwake.
Akiungana na Katibu Mkuu Spika wa bunge mstaafu na aliyekuwa Makamu Mkiti wa CCM Pius Msekwa amesema,
“Katibu Mkuu yuko sahihi. Sisi wakati wetu tulikuwa na vyuo vya chama kwa ajili hiyo. Kulikuwa na chuo cha Kivukoni ambacho kilianzishwa tangu wakati wa uhuru kwa madhumuni ya kuwaandaa viongozi baada ya uhuru.”
Naye katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba amesema viongozi wengi vijana wa sasa hawana staha, adabu na heshima.
“Ukitoa hoja zako, kwa sababu hawana staha na hawana adabu, hawana heshima watakufuatilia wewe. Ndiyo maana siku hizi tunaogopa kuzungumza na vyombo vya habari,” alisema Makamba.
Ukiacha RC Makonda anayejadiliwa sana, viongozi wengine vijana ambao wengi ni wakuu wa wilaya, wamekuwa wakishutumiwa kwa kuwaweka rumande watumishi wa umma, wananchi na wengine kukwaruzana na wawekezaji na watendaji wa serikali.
Wengi wa vijana hawa (wanaokemewa) ni zao la Jumuiya ya Umoja wa vijana wa CCM UVCCM. Maadili yanayofundishwa ndani ya UVCCM ya leo ya kina Shaka ni tofauti kabisa na maadili yaliyokuwa yanafundishwa na UVCCM iliyowazaa kina Kikwete, Lowassa, ni tofauti na UVCCM ya kina Guninita, kina Nchimbi, Nape na kadhalika.
Ukipandacho ndicho ukivunacho.
Miaka ya hivi karibuni imekuwa ni jambo la kawaida kukuta mitandaoni vijana wakiandika maandishi ya hatari ya kudhuru binadamu mengine ya kuhatarisha usalama wa nchi bila kuchukuliwa hatua na vyombo vya usalama, na ukifuatilia aliyeandika utaambiwa ni kiongozi wa UVCCM mkoa au wilaya, hawa ndio viongozi wanaotegemewa pengine kuwa marais au mawaziri.
Jamii imekuwa ikikemea vitendo hivi bila mafanikio, bila viongozi wa Chama na serikali kuingilia kati, badala yake wameonekana wakiongezewa vyeo. Matokeo yake wanajawa na viburi na kupelekea kutenda vitendo vya ajabu katika jamii.
Siku hizi ukitaka kudhuru kimbilia UVCCM, ukitaka kutukana kimbilia UVCCM, ukitaka kuanzisha gazeti la kutukana na kukashifu kimbilia UVCCM hakuna chombo chochote kitakachokuuliza, nje ya hapo utashukiwa kama mwewe.
Vitendo hivi vikiachwa bila kukemewa tutazalisha taifa la ajabu sana siku zijazo, hawa vijana wanaoachwa wafanye watakavyo kuna siku ndoto zao hazitatimizwa na chama watazitafuta nje ya chama.
Ni wito kwa viongozi mbalimbali, wazee, wastaafu, viongozi wa dini, vyombo vya serikali na jamii kwa ujumla, kujitokeza waziwazi kukemea vitendo hivi, tuwaunge mkono makatibu wa CCM, Askofu Shoo, Freeman Mbowe, Msekwa, Waziri wa Afya Ummy, walioanzisha vita hii kukemea vitendo vinavyofanywa na viongozi vijana vilivyo kinyume na maadili ikiwemo, ubaguzi, uonevu, kuingilia taaluma na fani za watu kwenye maeneo wanayoyaongoza.
Kitengo cha usalama wa Taifa, TISS kina wajibu wa kuchunguza viongozi wa kitaifa wanaoandaliwa, taifa likipata kiongozi asiye na maadili, atakayeliharibu taifa TISS hawatakwepa lawama. Chama cha Mapinduzi kwa upande wake hakinabudi kuhakikisha vijana wake hawakiuki maadili na kama kitengo kiafuata katiba yake na malengo ya kuanzishwa kwake.