Serikali mbioni kufilisi mifuko ya jamii

Serikali mbioni kufilisi mifuko ya jamii

Bahati furaha

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2012
Posts
3,077
Reaction score
1,438
Tunalazimika tena leo kuitahadharisha Serikali kuhusu athari zinazotokana na utamaduni wake wa kutolipa madeni.

Miezi minne tu iliyopita tuliitahadharisha kuhusu jambo hilo na kusema dunia sasa inajua kwamba Serikali yetu imelimbikiza madeni kiasi cha kudaiwa kila kona, huku ikielekeza fedha nyingi katika matumizi yasiyo ya lazima.

Tulionyesha wasiwasi kuhusu kasi yake ya kukopa na kusema Deni la Taifa lipatalo zaidi ya Sh30 trilioni linazidi kupaa na sio muda mrefu nchi yetu itakuwa haikopesheki iwapo Serikali haitabadili mwelekeo. Itakumbukwa kuwa, Machi mwaka jana deni hilo lilikuwa Sh23.6 trilioni.

Inasikitisha kuona kwamba hadhari yetu hiyo bado haijachukuliwa kwa uzito stahiki na Serikali, kwani imeendeleza dhana kwamba bado nchi inakopesheka na kwamba Deni la Taifa bado ni endelevu.

Dhana hiyo tunayoweza kuiita potofu imeongezwa nguvu na kauli iliyotolewa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Shirika la Fedha Duniani (IMF), Kanda ya Afrika, Antoinette Sayeh kwamba Deni la Taifa halijavuka kiwango na kwamba Tanzania inaweza kuendelea kukopa iwapo tu fedha hizo zitaelekezwa kwenye ujenzi wa miundombinu na miradi ya maendeleo.

Wakati mkurugenzi huyo wa IMF akitoa kauli hiyo, zimekuja taarifa kwamba madeni sugu ya Serikali yanatishia uhai wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini, huku Mamlaka ya Usimamizi ya Mifuko hiyo (SSRA), ikitoa angalizo kwa Serikali kwamba deni lake la Sh8.43 trilioni kwa mifuko hiyo litaifilisi mifuko hiyo siyo tu kiasi cha kushindwa kujiendesha, bali pia kuikwamisha na kushindwa kuwalipa mafao wanachama wake.

Deni hilo, ambalo baadhi ya wataalamu wa uchumi wanasema haliwezi kulipika kirahisi, linatokana na Serikali na taasisi zake kukopa kwenye mifuko hiyo na kutopeleka michango ya wanachama.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), juzi ililazimika kuwakutanisha wakurugenzi wa mifuko hiyo, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Gavana wa Benki Kuu (BoT) na SSRA kwa lengo la kutafuta suluhisho la tatizo hilo.

Pande zote zilikubaliana kwamba suluhisho pekee ni Serikali kulipa madeni hayo, ambayo ni takribani nusu ya bajeti ya Serikali kwa mwaka, vinginevyo mifuko hiyo itafilisika na kusababisha madhara makubwa kiuchumi.

Tunaambiwa kwamba katika mazungumzo hayo, Serikali ilithibitisha kulitambua deni hilo, lakini ilishindwa kueleza lini italilipa wala utaratibu utakaotumika kulilipa. Hata hivyo, sisi hatuna ugomvi kuhusu Serikali kukopa, isipokuwa kinachopaswa kuangaliwa kwanza ni Serikali inakopa fedha kufanya shughuli gani.

Ndiyo maana tulipaza sauti kupinga Bajeti ya mwaka wa fedha uliopita, ambapo ilitenga zaidi ya asilimia 60 ya bajeti kwa matumizi ya kawaida, huku miradi na shughuli za maendeleo zikipewa chini ya asilimia 40.

Katika Bajeti ya mwaka huu wa fedha, miradi na shughuli za maendeleo zimetengewa Sh6,445 trilioni sawa na asilimia 32.4 ya bajeti nzima ya Sh19.9 trilioni, huku matumizi ya kawaida yakitengewa Sh13.408 trilioni sawa na asilimia 67.4 ya bajeti hiyo.

Hapo ndipo lilipo tatizo. Serikali inakopa fedha kwa matumizi yasiyo na tija kwa nchi. Kwa utamaduni huu wa kukopa na kutolipa madeni, nchi yetu huko tuendako haiwezi kuepuka kufilisi mifuko hiyo na hivyo kuathiri ustawi wa wafanyakazi ambao ni wanachama na kugeuza wastaafu kuwa ombaomba.


Chanzo: Gazeti Mwananchi
 
Halafu unaambiwa mkubwa sana ni mchumi si afadhali na yule mwandishi wetu nchi iliheshimika na hela ikawa na thamani.Hivi usalama walikuwa wapi hadi tukapitisha majanga tena mara mbili.Mkubwa sana anaona raha kusafiri tu.
 
Halafu unaambiwa mkubwa sana ni mchumi si afadhali na yule mwandishi wetu nchi iliheshimika na hela ikawa na thamani.Hivi usalama walikuwa wapi hadi tukapitisha majanga tena mara mbili.Mkubwa sana anaona raha kusafiri tu.

Na ndiko pesa zinakoishia mkuu. Ni bora hata ofisi angeihamishia pale New VIP JNIA.
 
Na ndiko pesa zinakoishia mkuu. Ni bora hata ofisi angeihamishia pale New VIP JNIA.
Sawa kabisa ili akiota anasafiri aamke tu na kusafiri tena ingeepusha foleni na ving'ora!!.Kwa kweli inasikitisha nawashauri usalama ni lazima wajipange sana.Watu wanajua wanakopa bado matumizi ni yale yale,wanatembelea magari ya kifahari utafkiri wao ndo wanadai.
 
kwa hili deni la trilion 32 ,tusitegemee maisha bora kwa kila mtanzania ,ila bora maisha kwa kila mtanzania ,ukicheki ufisad wa fedha za escrow zinatumiwa na wazir mkuu kutoa hongo ili apitishwe kwenye kinyanganyiro cha kamati kuu ya ccm ,ili agombee urais ,kwa nin hizo fedha zisipelekwe kwenye mirad ya maendeleo kama hawa viongoz wa ccm wanaitakia mema nchi hii iliyoachwa na baba wa taifa jk nyerere ikiwa haina maden yasiyolipika kama haya ya leo ,
 
Sawa kabisa ili akiota anasafiri aamke tu na kusafiri tena ingeepusha foleni na ving'ora!!.Kwa kweli inasikitisha nawashauri usalama ni lazima wajipange sana.Watu wanajua wanakopa bado matumizi ni yale yale,wanatembelea magari ya kifahari utafkiri wao ndo wanadai.
Mkuu ni shida na ndo maana wakakataa kipengele cha maadili ya viongozi kwenye rasimu ya katiba kuwa na nguvu.
 
Mkuu ni shida na ndo maana wakakataa kipengele cha maadili ya viongozi kwenye rasimu ya katiba kuwa na nguvu.
Hivi katiba ya kutungwa na akina Chenge itakuwa katiba ya wananchi au majambazi?Yaani hii nchi aliyebaki wa kutusaidia ni Mungu tu.
 
kwa hili deni la trilion 32 ,tusitegemee maisha bora kwa kila mtanzania ,ila bora maisha kwa kila mtanzania ,ukicheki ufisad wa fedha za escrow zinatumiwa na wazir mkuu kutoa hongo ili apitishwe kwenye kinyanganyiro cha kamati kuu ya ccm ,ili agombee urais ,kwa nin hizo fedha zisipelekwe kwenye mirad ya maendeleo kama hawa viongoz wa ccm wanaitakia mema nchi hii iliyoachwa na baba wa taifa jk nyerere ikiwa haina maden yasiyolipika kama haya ya leo ,

Hata Chinga aliiacha pazuri co kama huyu zuzu mkuu!
 
Hivi katiba ya kutungwa na akina Chenge itakuwa katiba ya wananchi au majambazi?Yaani hii nchi aliyebaki wa kutusaidia ni Mungu tu.

Itabidi tupige kampeni ya HAPANA mtandaoni na mitaani ili kuikwamisha hii katiba haramu.
 
Msiwe na wasiwasi tumejipanga tunayo mafuta na gesi ya kutosha hayo madeni yote yatalipwa ndani ya muda mfupi.
 
Kukopakopa hovyo na kushindwa kulipa kwa wakati ni dalili za kushindwa kwa utawala. Mkulu na timu yake wame-prove failure katika kui-manage nchi. Wamekalia kupaa tu hata kuwazidi wanaanga wa NASA na kupewa vipande vya vitambaa kutoka kwa wapigaji kina Gucii.
Lakini watz walitonywa na marehemu baba wa taifa juu ya mtu huyu tukajitia uziwi. Sasa yanatukuta tunapiga mayowe ya kuomba msaada. Tumechelewa mno.
Hivi wakuu, laana kwenye ukoo huwa haiishi vizazi na vizazi? Lile la mangungo kuuza nchi kwa kipande cha nguo limeibuka tena kwani wakulu wanauza nchi kwa suti.
 
Si ndo Mambo yetu ya uswahili yale, ukijua kuna ela itaingia unaanza kukopakopa, yeye anajua gas ipo ndo maana mambo meeeengi yako katika mipango yatafanyika, kama kuboresha daftari la wapiga kula, kula ya maoni, uchaguzi serikali za mitaa n.k. Ndo maana mtwara walikula kibano saana
 
Kukopakopa hovyo na kushindwa kulipa kwa wakati ni dalili za kushindwa kwa utawala. Mkulu na timu yake wame-prove failure katika kui-manage nchi. Wamekalia kupaa tu hata kuwazidi wanaanga wa NASA na kupewa vipande vya vitambaa kutoka kwa wapigaji kina Gucii.
Lakini watz walitonywa na marehemu baba wa taifa juu ya mtu huyu tukajitia uziwi. Sasa yanatukuta tunapiga mayowe ya kuomba msaada. Tumechelewa mno.
Hivi wakuu, laana kwenye ukoo huwa haiishi vizazi na vizazi? Lile la mangungo kuuza nchi kwa kipande cha nguo limeibuka tena kwani wakulu wanauza nchi kwa suti.

Hata EL pia alizungumziwa na huyo mzee kipindi hichohicho cjui sasa tutaamuaje!!!!!!!!!!!
 
Hata EL pia alizungumziwa na huyo mzee kipindi hichohicho cjui sasa tutaamuaje!!!!!!!!!!!

kwa uziwi na upofu wetu utaona anachaguliwa kuwaongoza as if hakuna wenye utashi wa kuongoza nchi hii. Shida yetu watz ni kukosa utashi wa kuamua ndo maana kila kitu tunaamuliwa. Niwasihi tu kuwa tujifunze kusema hapana kwa mambo yasiyo na tija kwa nchi yetu. Tuitangulize nchi kabla ya tumbo letu!
 
Back
Top Bottom