Yaani serikali haina pesa za kutosha kugharamia mambo yake na imeshindwa kupewa mikopo na dhamana haziuziki so inataka iprint pesa zingine ili igharamie shughuli zake sasa pesa hii itaingia kwenye mzunguko itakuwa nyingi kuliko shughuli za uzalishaji matokeo yake pesa itaporomoka thamani zaidi.Kuprint not mpya me sijaelewa yaani nizilezile ila wanaziongeza nyingine au wanazibadilisha kabisa wanaleta zaaina nyingine
Sent using Jamii Forums mobile app
Tuko karne ya 21 hao unawaita mafisadi hawataumbuka tutaumbuka sisi walala hoi. Dunia imebadilika kama inaweza kwenda popote duniani na card ya bank ya Tanzania na ukatoa pesa kwenye ATM ya nchi hiyo, au ukanunua na card ya tembo kwenye dika lolote duniani bado unafikiri kuna kuumbuka kwa mafisadi na siyo sisi wakala hoi? Nchi kama Uingereza ukinunua nyumba ya kawaida kwa cash na resident permit wanakupa unafungua account na siyo lazima uishi uingereza unafungua business zako. Huoni watafungua account kwenye nchi za jirani hata Kenya na business zao.Mafisadi mnaogopa lazima kiwanuke, hizo hela zenu zinawaozea lah-sivyo zirudi ktk mzunguko.
JPM kawabana kama mjusi chini ya Mlango
Ila mkuu hii taarifa inauhakika kiasi gani maana habari nzito hiiYaani serikali haina pesa za kutosha kugharamia mambo yake na imeshindwa kupewa mikopo na dhamana haziuziki so inataka iprint pesa zingine ili igharamie shughuli zake sasa pesa hii itaingia kwenye mzunguko itakuwa nyingi kuliko shughuli za uzalishaji matokeo yake pesa itaporomoka thamani zaidi.
Kuchapa pesa zaidi kupo ila tu pale inapohitajika yaani ikiwa scarce zaidi
Mimi mtu nisie muamini katika nchi hii kwa ufupi ni Dr.Philip Mpango,huyu mtu ni hatari kuliko eboraHivi elfu kumi unaitafuta kwa shida, na ukiipata unanunua vitu vichache , jina la uchumi wa namna hii ni lipi?
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama litafanyika hili basi tutegemee kutumbukia shimoni kabisa maana uchumi ukishaharibika kuurekebisha ni kazi ngumu lakini yote haya ni mavuno ya kutokuwa msikivu na kujifanya anajua kila kitu mkemia yy, injinia yy, mchumi yy lakini ifahamike wazi hawa aliowaita wanyonge watapata tabu sana kiasi cha kujuta kuzaliwa TanzaniaBAADA ya uchumi wa nchi kuyumba na maisha ya wananchi kuwa magumu, Rais John Magufuli anahaha kufyatua noti mpya.
SAUTI KUBWA inatambua kwamba tayari serikali imeshaanza mradi wa ufyatuaji wa noti hizo.
Hata hivyo, mradi huo umekwama kwa muda kwa sababu ya kugubikwa na sintofahamu kati ya rais na washauri wake; na miongoni mwa kampuni zilizoingia katika mchakato huo.
Kampuni za kimataifa ambazo zimetambulika kuingia katika mzozo huo ni De la Rue International, Oberthur Fiduciare, na M/s Crane Currency.
Vyanzo vinataja ufisadi katika mchakato kama sababu mojawapo iliyosababisha mzozo huo. SAUTI KUBWA inafuatilia habari za kina kuhusu mzozo huo.
Baadhi ya washauri wa serikali wanapinga ufyatuaji wa noti mpya wakidai utaongeza mfumuko wa bei, utashusha zaidi thamani ya shilingi ya Tanzania; na utafanya maisha ya wananchi yawe magumu zaidi.
Baadhi ya wachambuzi na wachumi waliozungumza na SAUTI KUBWA wanasema iwapo serikali itachapisha noti hizo nchi inaweza kukumbwa na mdororo wa kiuchumi kama uliokumba Zimbabwe katika utawala wa Robert Mugabe.
Mchambuzi mmoja amesema: “Itasababisha mfumuko wa bei za kila kitu kwa namna itakayoifanya shilingi yetu isiwe na thamani kabisa. Hiki ndicho alichokifanya Mugabe miaka ya nyuma baada ya kunyang’anya wazungu mashamba yao na vitega uchumi kutoka nje kukauka.
“Matokeo yake ni kwamba Zimdollar ilipoteza thamani hadi ikabidi ifutwe kabisa. Leo Zimbabwe haina sarafu yake yenyewe, na wananchi wanalazimika kutumia dola ya Marekani na rand ya Afrika Kusini kwa ajili ya manunuzi ya kila aina. Huko ndiko Magufuli anapotaka kupeleka Tanzania. Ataharibu kila kitu kilichobaki.”
Mchumi mmoja anayeheshimika nchini, ambaye SAUTI KUBWA haitataja jina lake, amezungumzia mfumuko wa bei na mzunguko wa fedha. Anasema:
“Mfumuko wa bei uko chini ya asilimia nne (4%). Si mbaya sana. Mzunguko wa hela ni kidogo. Hii ni mbaya. Kuchapisha hela ni uamuzi mbaya kiuchumi. Ujazo wa fedha katika uchumi lazima uendane na kiwango cha shughuli za uzalishaji katika uchumi. Kuchapisha hela ni njia ya ‘kiswahili’ ya kukabiliana na changamoto ya kiuchumi.”
Uamuzi wa Magufuli kuagiza ufyatuaji wa noti mpya, unaakisi kituko cha Idi Amini (dikteta wa Uganda 1971-1979) ambaye alipoelezwa juu ya upungufu wa fedha katika mzunguko, aliamuru benki kuu: “fyatua nyingi zaidi.”
Akijadili hali hii, mhadhiri wa uchumi anayeishi Marekani, anasema kwa kirefu:
Kwanza, tuanze na kujua sababu za lazima za kuchapa pesa. Hii ni kweli kuwa serikali haina fedha za kuendesha shughuli zake na kulipa madeni.
Pili, ni kwa nini serikali haina fedha? Kwa kawaida, ukiacha misaada, serikali ina vyanzo vikubwa viwili vya mapato: (1) Kodi, (2) kuuza dhamana au bonds.
Kwa hiyo, yawezekana ukusanyaji wa mapato ya kodi umepungua Ila serikali haisemi ukweli ili kijipatia sifa za kijinga.
Pia dhamana za serikali huenda haziuziki kama ilivyokuwa awali.
Mambo yote mawili, kupungua kwa mapato ya kodi na dhamana hutokea iwapo uchumi umesinyaa: hakuna uzalishaji wa kutosha kutokana na kudorora kwa uzalishaji kiuchumi.
Nini hufanyika? Serikali ingeweza kukopa zaidi. Huenda wakopeshaki hawapo tayari kwa kuwa kiwango cha uaminifu wa serikali kimeshuka. Utakupunga credit rating ya Tanzania imeshuka sana kwa sasa.
Pia, serikali ingeweza kubana zaidi matumizi yake. Lakini hili nalo Ni gumu sana kwa sasa kwa kuwa tayari imebana hadi ukomo wake. Kumbuka pia kubana matumizi ya serikali hupunguza ukuaji wa uchumi. Kudorora kwa sekta binafsi ni matokeo ya serikali kupana matumizi.
Nini matokeo ya kuchapa pesa? Uchapaji fedha huwa na madhara hasi kiuchumi iwapo uzalishaji haukui. Yaani, kutakuwa na fedha zaidi kwenye mzunguko zisizo na thamani. Matokeo yake ni mfumuko mkubwa wa bei. Kumbuka kilichotokea Zimbabwe kwa utawala wa Mugabe.
Mfumo wa bei usioendana na kipato halisi cha watu, utapunguza uwezo wa kutumia (purchasing power) na matumizi (consumption). Hapo uchumi utaendelea kuelekea shimoni zaidi.View attachment 853999
Fungua hiyo attachment utaelewa.Kichwa cha Habari na Habari yenyewe Kuna makosa ya uandishi Au kupotoshwa. Kuna vitu viwili lazima vieleweke moja ni KUPRINT NOTE MPYA kwa maana ya mwonekano mpya. pili ni kuprint notes hizi zinazotumika mpya ziingizwe kwenye uchumi. Kuprint note mpya kwa maana ya mwonekano haina madhara kabisa kiuchumu Sana Sana itasaidia kiuchumu .HILI LA PILI NDIO JIPU. yaan kuprint notes hizi zinazotumika Hapo ndio hatari Sana.ukiangalia hali ya uchumi kwa Sasa haaitaji kuongezea fedha kwenye mzunguko kwa njia ya printing itatupeleka Zimbabwe kabisa bila chenga .serikali ijikite kukopa Au kutafuta wawekezaji wakubwa na stimulas package zingine. Serikali na BOT wanayo haki ya kuprint notes zingine lakini si kwa Sasa ambapo wote ni mashahidi benki zinafungwa na kupost profit kushuka pia biashara Kubwa nyingi zinafungwa na Hakuna wawekezaji wapya wakubwa. Serikali iache uchumi ujiendeshe wenyewe kwa kuwa na uwiano halisi baina ya production na money supply. STOP INJECTING NEW NOTES IN THE ECONOMY
Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui walikuwa wanafuta ili kuficha nini!!Hii taarifa imeletwa mara nyingi na imefutwa mara nyingi sana ! hongera mkuu kwa uzi wako kubaki
Sijui maana hata mm ndo nasoma hapa inatumia Wasiwasi kuhold pesa benki tena kwa denomination ya shilingi ya Tzn ni vyema wahusika waweke sawa hii taarifa inatia mashaka tuendakoIla mkuu hii taarifa inauhakika kiasi gani maana habari nzito hii
Sent using Jamii Forums mobile app
Dah hiii hatari kama itakuwa Nikweli nibora tungepambana kivingine lakini sio kuingiza pesa not mpyaSijui maana hata mm ndo nasoma hapa inatumia Wasiwasi kuhold pesa benki tena kwa denomination ya shilingi ya Tzn ni vyema wahusika waweke sawa hii taarifa inatia mashaka tuendako
But ukitaka kujua ukweli hebu angalia muitikio wa dhamana za setikali lakini pia je wafanyabiashara wanachukua mikopo benki? Na je benki zinakopesha? Juzi kati nilisoma humu pia benki kuu imeshusha riba ya kukopesha commercial banks hiyo ilikuwa round ya pili kama sikosei
Ni hatari kuliko kawaida Mungu aepushe mbali na wahusika wawe wasikivu mara mia hizo pesa zisichapwe kwa minajiri ya mtoa mada mtasambaratisha familia zetu jamaniKama litafanyika hili basi tutegemee kutumbukia shimoni kabisa maana uchumi ukishaharibika kuurekebisha ni kazi ngumu lakini yote haya ni mavuno ya kutokuwa msikivu na kujifanya anajua kila kitu mkemia yy, injinia yy, mchumi yy lakini ifahamike wazi hawa aliowaita wanyonge watapata tabu sana kiasi cha kujuta kuzaliwa Tanzania
Huyo ndio "Jiwe" katika ubora wake.Ni hatari kuliko kawaida Mungu aepushe mbali na wahusika wawe wasikivu mara mia hizo pesa zisichapwe kwa minajiri ya mtoa mada mtasambaratisha familia zetu jamani
Labda zimechakaa!Kuprint not mpya me sijaelewa yaani nizilezile ila wanaziongeza nyingine au wanazibadilisha kabisa wanaleta zaaina nyingine
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sasa ukipata fedha ya akiba bora uitunze kwenye dollar tena cash sio bank maana huwa kuna kipindi rationing au ukomo wa kuwithdraw unawekwa bila kujalisha uliitolea jasho au pesa yeyote ya nje yenye thamani maana yajayo yanatia mashakaDah hiii hatari kama itakuwa Nikweli nibora tungepambana kivingine lakini sio kuingiza pesa not mpya
Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi mkuu kwalocal bank kama nmb naweza kuwa naweka pesa ila kwadola yaani naenda nahela zakibongo ila nikifika nawaambia waziweke kwamtindo wadola inawezekana?Kwa sasa ukipata fedha ya akiba bora uitunze kwenye dollar tena cash sio bank maana huwa kuna kipindi rationing au ukomo wa kuwithdraw unawekwa bila kujalisha uliitolea jasho au pesa yeyote ya nje yenye thamani maana yajayo yanatia mashaka