Serikali mbili hazikwepeki, bwana ismail jussa upo?

Serikali mbili hazikwepeki, bwana ismail jussa upo?

ebaeban

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,205
Reaction score
2,707
Serikali mbili hazikwepeki, Bwana Ismail Jussa upo?

Zanzibar huru yenye mamlaka kamili ni jambo la hatari, Inchi ya Zanzibar imekaa kama eneo la kimbinu (Strategic point), kuiachia Zanzibar ijitawale ni sawa kabisa na wabara kujitoa mhanga maana itakuwa hatari sana kwao kama ilivyoanza kuwa hatari sasa, matukio ya hivi karibuni ya Mapadri kupigwa risasi au kumwagiwa tindikali ni viashiria tu vya hatari hizo.

Kuna ushahidi wa kimazingira unaoonyesha hatari hizo zitapunguzwa kwa kiasi Fulani au hazitakuwepo tu kwa uwepo wa muungano, na hatari hizo zitapungua zaidi kwa uwepo muungano ulio imala, serikali ya Bwana Kikwete imefanya makosa makubwa kuacha inchi ya Zanzibar kuandika katiba yoa, hii ni sawa na kuweka ufa mkubwa sana ndani ya muungano.

kwa manufaa ya iliyokuwa Tanganyika inafaa muungano uimarishwe zaidi hata ikibidi kuwe na serikali moja tu yenye nguvu huko mbeleni. Kama Israel inavyoona kuwa haiwezekeni kuiachia milima ya kimbinu ya GOLANI, hivyo hivyo ni haiwezekani kuiachia Zanzibar ijitenge kwani bara itapata shida sana kama Kenya ilivyoanza kupata shida sasa zidi ya wasomali, wasomali wanavyofanya kwa Kenya ndiyo hivyo hivyo watu wabaya watakavyoifanyia Tanzania bara kupitia Zanzibar.

Ni ukweli usiopingika kwamba Zanzibar ikiwa huru basi itakuwa ndio mwisho wa makanisa huko visiwani na utakuwa mwanzo wa mambo mengine maovu ambayo sitaweza kuyasema hapa. Hivyo wanainchi wenzangu maeneo yote ya KIMBINU, maeneo yote ya ki-mkakati huwa hayaachiwagi hivi hivi kimasihala ni lazima kupigania mpaka tone la mwisho la damu limemwamwagike ndio huwa kuna ku-surrender.

Natoa wito UKAWA warudi kwenye bunge la katiba watetee serikali mbili ili tuendelee kuwepo japo kwa manyanyaso, sasa kero za muungano zilizopo ni nusu shari muungano ukivunjika itakuwa shari kamili.
 
haf unavyosema au unavyotumiaa neno kuiachia unamaana umeishika au neno lako lina maana gani?
 
ujinga huu,marekani ikiamua kutupga tutawazuia na zanzibar yetu?
 
Ni kweli bila muungano hata Polisi wasingembambikizia risasi nyumbani kwake Mansour Himid Yusuf
 
Kama serikali mbili haziwekani bora moja kuliko tatu ni shida tu kunana watu watalazimishwa kuvaa mavazi fulani
 
Hili huenda likawa limetumwa na kina Kikwete hilooo tupa kule Zanzibar chukueni nchi yenu muwe kama Dubai hiyo inawezekana kabisa Zanzibar itakuwepo na Makanisa na Wakristo watakuwepo tu hakuna cha ati Makanisa yatachomwa moto hii ya uchomaji moto si ajabu unafanywa na serikali ya CCM na Ile Ya CCM huku Zanziba SMZ ili tu kuwatisha wananchi ati Zanzibar itakuwa hivyo CCM ni watu wa kuogopwa sana sana.Ati leo hii wamemakamata Mansor ati ana SMG na yanasema anamiliki kihalali lakni ana Risasi nyingi hapa moja kwa moja naona atakuwa kabambikiziwa kesi huyu bwana kwa kuwa tu hayupo tena CCM na kwa kuwa alikuwa kinyume nao kwani yeye ni mdau wa serikali 3 sasa kama ni kweli, naomba niwaulize wadau humu ndani je huyu bwana kaanza kumiliki silaha wakati ashatoka CCM au baada ya kutoka na kama kaanza kumiliki kipindi hicho akiwa CCM kwa nini wasingemkamata kipindi hicho??Hapo kuna mkono wa Mwigulu Mchemba na subirini mtasikia ana kesi ya Ugaidi na anafadhili wamwaga tindikali lol.Hivi Adam Malima ile kesi yake ya kukamatwa na Mbunduki wa kijeshi mbona hatatiwa ndani iweje huyu ati kwa kuwa sio CCM atiwe ndani?Uko wapi the so called Muungano wa Udungu usio na ubaguzi??
 
unaongelea kuvunjika kwa muungano ama unaongelea muundo wa serikali? maana kama ukisema s1,2 au s3 unaongelea muundo wa serikali kikakatiba, na unaposema kuichia au kuishikilia zanzibar hapo sijakuelewa mkuu ufaafanuzi tafadhali
 
Hiyo siyo sababu tosha kuitawala Zanzibar. Ni uwoga na udikteta tu! Siku moja inshallah, Zanzbar itakuwa huru!
 
Bora kilamtu na serikali yake ,yaani tuwe wa mwanzo kuanzisha Private government :wacko: hapa ulimwenguni !
 
Back
Top Bottom