Serikali itutake radhi kuhusu Katiba mpya

cjilo

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
884
444
Naandika uzi huu kwa masikitiko makubwa, serikali ya CCM imetufikisha pabaya sana kiuchumi.

Pamoja na ushauri uliokuwa ukitolewa na viongozi wa dini, asasi za kiraia na wapinzani kuwa mchakato wa katiba mpya uvunjwe na bunge lisiendelee na vikao vya kuijadili serikali ikiongozwa na Sita ilijifanya kichwa ngumu.

Mchakato huo toka mwanzo haukuonesha kama utakamilika zaidi ya kutupotezea muda na fedha. Pamoja na hayo bado mchakato umeacha aibu kubwa kwa CCM na Mh Kikwete.

Ni wazi kuwa huu mchakato hauwezi kuwepo tena kabla ya uchaguzi mkuu au hata baada ya uchaguzi mkuu.

Mamilion yaliyopotea yangeweza kutumika kununua madawa ya hospitalini na kuokoa maisha ya watanzania wagonjwa.

Serikali ilikosea, inakosea na itakosea pasipo kujitokeza hadharani na kukiri makosa na kutuomba msamaha
.
 
Wakati wa Bunge la Katiba,'umoja na mshikamano' wa CCM ulionekana. Kila Mjumbe aliyekuwa ana mahusiano na CCM alilinda na kutetea msimamo wa chama chetu. Kila Mjumbe wetu alifoka,aling'aka na kusisitiza juu ya msimamo wa chama.

Jambo kubwa lililopingwa bila kuungwa ni gharama za uendeshaji wa Serikali. Rasimu za Tume ya Warioba ilipendekeza Serikali tatu. Hoja kubwa ya kupinga Serikali tatu ilikuwa kuongezeka kwa gharama. Yaani,Serikali tatu zingewaelemea wananchi.

Wajumbe wa CCM walitupa vijembe,kejeli,nyodo;kumwaga povu na kusisitiza kuhusu hilo. Lakini,CCM sasa inafanya unafiki badala ya urafiki. Kupitia NEC,CCM na Serikali yake inapanga kuongeza majimbo ya Ubunge. Yakiongezeka majimbo,viti maalum navyo vitaongezeka. Vipi kuhusu kuongezeka kwa gharama?

Kwa ukígeugeu huu,CCM iwahi kuomba radhi. Iseme ukweli juu ya Serikali tatu. Huu ni mwaka wa uchaguzi. Usanii,uongo,ulaghai na utapeli wa kisiasa utatugharimu. Hatutaaminika kwenye Urais,Ubunge na Udiwani. CCM,shime iharakishe kuomba radhi. Muda ni huu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kanda ya Kati)
 
uongo, usanii na ghiliba za ccm katika kupata ushindi wake. ilipiga makelele mengi kwamba serikali tatu ni gharama ili kuhalalisha muundo wa serikali mbili. leo hojahiyo haisemwi kwenye mchakato wa kugawa majimbo ili kuendelea kuwnyonya wananchi kupitia posho za wabunge na mifuko ya jimbo. ccm wanapaswa kuwaomba watanzania radhi kwa mengi.
 
Mkuu yalipotea mabilioni si mamilioni, ule msafara wa magari ya tume ya jaji warioba ulikuwa unatumia magari ambayo hayaendani na uchumi wa Taifa hili ylikuwa na hadhi ya kutumiwa labda na Nigiria au Afrika kusini, na sasa washajigawia hii ccm haiwezi kuwa na huruma kwa sababu ni majitu yaliyojitoa ufahamu, mtu anatukana viongozi wa dini ili waendelee kuibia watanzania eti sasa anautaka urais hata wa urambo haupati.

Na msamaha kutoka kwa CCM haiwezi kutokea aliekuwa anaweza kuomba msamaha CCM ikikosea ni hayati sokoine peke yake, hawa waliobaki ni ubabe, dharau ndio tutaendelea kupokea toka kwao, tafakari chukua hatua.
 
Mzee Tupa Tupa CCM majimbo yote ambayo upinzani una nguvu kwa sasa ndo kete yao ya kuwa na watu wa ndio mjengoni hata kwa mambo yasiyo na masilahi kwa taifa.

Vipi kesho utakwenda A town kumsikiliza Laigwanani EL?
 
cjilo

Unajilisha upepo!na leo umeamka vibaya na inaelekea huna kazi ya kufanya ukaamua kuja humu kuchafua hali ya hewa nini cha ajabu au hujui Taifa lako linaelekea wapi,usilete siasa uchwara kwenye masuala yaliyopo kisheria kwani unafikiri mchakato huo ni wa RAIS au wa chama??kama uko huko pole sana!
 
Last edited by a moderator:
Wajumbe wengi wa lile Bunge la Katiba walipatikana ki-magumashi - wakakaririshwa kutoa hoja ambazo hata hawaelewi mantiki yake - wakakaririshwa hadi kumkashifu Mzee wetu Warioba!!

Ndugu zangu hawa watu hawana nia nanjema na taifa letu. Huwezi kuongoza nchi ki-magumashi namna hii.
 
Wajumbe wengi wa lile Bunge la Katiba walipatikana ki-magumashi - wakakaririshwa kutoa hoja ambazo hata hawaelewi mantiki yake - wakakaririshwa hadi kumkashifu Mzee wetu Warioba!!

Ndugu zangu hawa watu hawana nia nanjema na taifa letu. Huwezi kuongoza nchi ki-magumashi namna hii.

Aaa inaelekea ulikosa ujumbe na umeathirika kisaikolojia teh teh pole sana subiri mwaka 2090 labda mkuu wa nchi atakufikiria!!
 
Mkuu yalipotea mabilioni si mamilioni, ule msafara wa magari ya tume ya jaji warioba ulikuwa unatumia magari ambayo hayaendani na uchumi wa Taifa hili ylikuwa na hadhi ya kutumiwa labda na Nigiria au Afrika kusini, na sasa washajigawia hii ccm haiwezi kuwa na huruma kwa sababu ni majitu yaliyojitoa ufahamu, mtu anatukana viongozi wa dini ili waendelee kuibia watanzania eti sasa anautaka urais hata wa urambo haupati.

Na msamaha kutoka kwa CCM haiwezi kutokea aliekuwa anaweza kuomba msamaha CCM ikikosea ni hayati sokoine peke yake, hawa waliobaki ni ubabe, dharau ndio tutaendelea kupokea toka kwao, tafakari chukua hatua.
You are absolutely right, mchakato wa kupata katiba mpya ya nchi siyo umeteketeza mamilioni ya shilingi bali ni mabilioni.

Wataalamu wa uchumi wanakadiria pesa iliyotumiwa kuanzia wakati wa ukusanyaji maoni uliofanywa na Tume ya Warioba, mapesa yaliyotumika kuwalipa wabunge wa BMK, uchapaji wa katiba pendekezwa ya Lumumba, iliyoandikwa na nyoka mwenye makengeza, uchapaji wa katiba hizo pendekezwa na usambazaji wake nchi nzima, inskadiriwa hadi sasa mchakato huo ushateketeza pesa zinazokadiriwa kuwa ni shilingi bilioni 200, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Kwa tafsiri nyingine ni kuwa hizo bilioni 200 zilizoteketea katika usakaji katiba mpya, ni sawasawa kama tungelinganisha na ajali ya moto ambayo imetoeketeza benki iliyokuwa imehifadh hizo bilioni 200.

Lakini hakuna watu wengine wowote wa kulaumiwa kwa 'kubuma' kupatikana kwa katiba mpya zaidi ya watawala wetu wa Sisiem, ambao walifanya kosa kubwa 'lisilosameheka' kwa kuidump kwenye 'dustbin' rasimu ya kattiba yenye maoni ya wananchi yaliyoratibiwa na Tume ya Warioba, na badala yake wakatuchomekea katiba yao mbadala ya Lumumba!

Kutokana na kufeli kupatikana kwa katiba mpya, kama alivyotuahidi JK kuwa ingepatikana kabla ya yeye kuondoka madarakani mwezi Oktoba mwaka huu, inatupa fundisho kubwa sana kwa waTz.

Funzo hilo kwa watawala wetu ni kuwa hawapaswi kupuuza sauti ya walio wengi, kwa kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
 
Wakati wa Bunge la Katiba,'umoja na mshikamano' wa CCM ulionekana. Kila Mjumbe aliyekuwa ana mahusiano na CCM alilinda na kutetea msimamo wa chama chetu. Kila Mjumbe wetu alifoka,aling'aka na kusisitiza juu ya msimamo wa chama.

Jambo kubwa lililopingwa bila kuungwa ni gharama za uendeshaji wa Serikali. Rasimu za Tume ya Warioba ilipendekeza Serikali tatu. Hoja kubwa ya kupinga Serikali tatu ilikuwa kuongezeka kwa gharama. Yaani,Serikali tatu zingewaelemea wananchi.

Wajumbe wa CCM walitupa vijembe,kejeli,nyodo;kumwaga povu na kusisitiza kuhusu hilo. Lakini,CCM sasa inafanya unafiki badala ya urafiki. Kupitia NEC,CCM na Serikali yake inapanga kuongeza majimbo ya Ubunge. Yakiongezeka majimbo,viti maalum navyo vitaongezeka. Vipi kuhusu kuongezeka kwa gharama?

Kwa ukígeugeu huu,CCM iwahi kuomba radhi. Iseme ukweli juu ya Serikali tatu. Huu ni mwaka wa uchaguzi. Usanii,uongo,ulaghai na utapeli wa kisiasa utatugharimu. Hatutaaminika kwenye Urais,Ubunge na Udiwani. CCM,shime iharakishe kuomba radhi. Muda ni huu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kanda ya Kati)

Mzee wangu Pole...........Ndiyo yalishatokea...........Mtoto yule sasa ana MJUKUU....Ila usijali mimi nipo tayari kukupigia kampeni pale ukisema tu unataka kugombea UBUNGE,sababu ninauhakika UZALENDO na zile KANUNI KUMI ZA TANU na CCM unazijua fika na unaziishi na ungetamani wenzako pia wazijue na waziishi.......

Lakini kwa MASHARTI ya NO KWA KATIBA PENDEKEZWA
 
You are absolutely right, mchakato wa kupata katiba mpya ya nchi siyo umeteketeza mamilioni ya shilingi bali ni mabilioni.

Wataalamu wa uchumi wanakadiria pesa iliyotumiwa kuanzia wakati wa ukusanyaji maoni uliofanywa na Tume ya Warioba, mapesa yaliyotumika kuwalipa wabunge wa BMK, uchapaji wa katiba pendekezwa ya Lumumba, iliyoandikwa na nyoka mwenye makengeza, uchapaji wa katiba hizo pendekezwa na usambazaji wake nchi nzima, inskadiriwa hadi sasa mchakato huo ushateketeza pesa zinazokadiriwa kuwa ni shilingi bilioni 200, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Kwa tafsiri nyingine ni kuwa hizo bilioni 200 zilizoteketea katika usakaji katiba mpya, ni sawasawa kama tungelinganisha na ajali ya moto ambayo imetoeketeza benki iliyokuwa imehifadh hizo bilioni 200.

Lakini hakuna watu wengine wowote wa kulaumiwa kwa 'kubuma' kupatikana kwa katiba mpya zaidi ya watawala wetu wa Sisiem, ambao walifanya kosa kubwa 'lisilosameheka' kwa kuidump kwenye 'dustbin' rasimu ya kattiba yenye maoni ya wananchi yaliyoratibiwa na Tume ya Warioba, na badala yake wakatucjomekea katiba yao mbadala ya Lumumba!

Kutokana na kufeli kupatikana kwa katiba mpya, kama alivyotuahidi JK kuwa ingepatikana kabla ya yeye kuondoka madarakani mwezi Oktoba mwaka huu, inatupa fundisho kubwa sana kwa waTz.

Funzo hilo kwa watawala wetu ni kuwa hawapaswi kupuuza sauti ya walio wengi, kwa kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.

Sauti ya walio wengi wapi hao??usilete mambo ya kufikirika hapa kama maoni yako binafsi yalitupwa usituleteehabari za maoni ya wananchi kutupwa wawapi hao, kasome vizuri then ukapige kura kama huelewi uliza!!
 
You are absolutely right, mchakato wa kupata katiba mpya ya nchi siyo umeteketeza mamilioni ya shilingi bali ni mabilioni.

Wataalamu wa uchumi wanakadiria pesa iliyotumiwa kuanzia wakati wa ukusanyaji maoni uliofanywa na Tume ya Warioba, mapesa yaliyotumika kuwalipa wabunge wa BMK, uchapaji wa katiba pendekezwa ya Lumumba, iliyoandikwa na nyoka mwenye makengeza, uchapaji wa katiba hizo pendekezwa na usambazaji wake nchi nzima, inskadiriwa hadi sasa mchakato huo ushateketeza pesa zinazokadiriwa kuwa ni shilingi bilioni 200, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Kwa tafsiri nyingine ni kuwa hizo bilioni 200 zilizoteketea katika usakaji katiba mpya, ni sawasawa kama tungelinganisha na ajali ya moto ambayo imetoeketeza benki iliyokuwa imehifadh hizo bilioni 200.

Lakini hakuna watu wengine wowote wa kulaumiwa kwa 'kubuma' kupatikana kwa katiba mpya zaidi ya watawala wetu wa Sisiem, ambao walifanya kosa kubwa 'lisilosameheka' kwa kuidump kwenye 'dustbin' rasimu ya kattiba yenye maoni ya wananchi yaliyoratibiwa na Tume ya Warioba, na badala yake wakatuchomekea katiba yao mbadala ya Lumumba!

Kutokana na kufeli kupatikana kwa katiba mpya, kama alivyotuahidi JK kuwa ingepatikana kabla ya yeye kuondoka madarakani mwezi Oktoba mwaka huu, inatupa fundisho kubwa sana kwa waTz.

Funzo hilo kwa watawala wetu ni kuwa hawapaswi kupuuza sauti ya walio wengi, kwa kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
Kabisa mkuu na hii ndio iwe fimbo ya kuwachapia wote wanaogombea ubunge watueleze kwa nini walipoteza hela zetu hali wakijua kabisa katiba haitapatikana? Hii pia ni sababu ya kushuka kwa thamani ya shilingi yetu, ni wazi ccm hawatujali na hivyo sie tusiwakubali kabisa waondoke na makabrasha yao ya katiba waende na watajuta siku moja.
 
Kabisa mkuu na hii ndio iwe fimbo ya kuwachapia wote wanaogombea ubunge watueleze kwa nini walipoteza hela zetu hali wakijua kabisa katiba haitapatikana? Hii pia ni sababu ya kushuka kwa thamani ya shilingi yetu, ni wazi ccm hawatujali na hivyo sie tusiwakubali kabisa waondoke na makabrasha yao ya katiba waende na watajuta siku moja.

Uzembe wako mwenyewe wa kutoa maoni pumba uuhamishie kwa wabunge wewe kilaza kweli tena ukute hata hujui tarehe ya kujiandikisha katika eneo lako unakalia kurukaruka acha uzembe wewe!!
 
Kabisa mkuu na hii ndio iwe fimbo ya kuwachapia wote wanaogombea ubunge watueleze kwa nini walipoteza hela zetu hali wakijua kabisa katiba haitapatikana? Hii pia ni sababu ya kushuka kwa thamani ya shilingi yetu, ni wazi ccm hawatujali na hivyo sie tusiwakubali kabisa waondoke na makabrasha yao ya katiba waende na watajuta siku moja.
Mtasema sana mchana, usiku mtalala, aliyewaambia mkimbie bungeni nani adu mje kulalamika eti mmekula fedha za walala hoi, nyie mmekuwa madebe matupu yasiyo na kitu ndo maana mnapiga makelele ovyo ovyo.
 
Mzee wangu Pole...........Ndiyo yalishatokea...........Mtoto yule sasa ana MJUKUU....Ila usijali mimi nipo tayari kukupigia kampeni pale ukisema tu unataka kugombea UBUNGE,sababu ninauhakika UZALENDO na zile KANUNI KUMI ZA TANU na CCM unazijua fika na unaziishi na ungetamani wenzako pia wazijue na waziishi.......

Lakini kwa MASHARTI ya NO KWA KATIBA PENDEKEZWA
Utabaki kuwa mtumwa wa ukawa mpaka kufa kwako wewe -----, poteza muda wako kwa malipo ya jero jero, lkn kwa hilo la katiba umechemsha.
 
Sauti ya walio wengi wapi hao??usilete mambo ya kufikirika hapa kama maoni yako binafsi yalitupwa usituleteehabari za maoni ya wananchi kutupwa wawapi hao, kasome vizuri then ukapige kura kama huelewi uliza!!

Umeandika pumba tupu
 
Sauti ya walio wengi wapi hao??usilete mambo ya kufikirika hapa kama maoni yako binafsi yalitupwa usituleteehabari za maoni ya wananchi kutupwa wawapi hao, kasome vizuri then ukapige kura kama huelewi uliza!!

Mbona jazba Mkuu? WaTanzania Tupende tusipende hatuna budi ku "revisit" mwenendo mzima wa mchakato wa upatikananaji wa Katiba tunayoitaka.
Kukemea mawazo ya msingi yanayotolewa kuhusu gharama na rasilimali ziizotumika wakati hatujafikia hatua muafaka sio sahihi.
Wala kuwaburuza wengine kwa kuwa majority inayosemekana ilikuwepo ni ile ya idadi ya wanachama wa Chama fulani Bungeni tu, sio uhalali wala utetezi mawazo yako!

Na tutaendelea kulisema hili hadi mwisho wake!
 
Back
Top Bottom