Serikali isimamie riba zinazotozwa na mabenki

Koryo2

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
2,056
2,515
Kama Mwananchi na Mtanzania riba inayotozwa na Mabenki hapa nchini kwa wananchi ni KUBWA SANA. Mfano hai mtu anapokopa anatakiwa kulipa riba ya 19% mpaka 22% wakati mwananchi huyo huyo akiweka fedha zake Benki anapewa riba ya 3%. Hapa hakuna usawa kabisa na kuonekana kuwa wananchi wananyonywa katika nchi yao. Tunaiomba Serikali yetu sikivu isimamie Mabenki nchini ili riba inayotolewa iwe rafiki kwa wananchi.
 
Labda wangekopa vyama pinzani ndio wangeona tatizo.Hapa nchini ni viongozi wa siasa si viongozi wa wanyonge.
 
Benki nyingine ni za kibiashara, huwezi kuwazuia na huku hizo riba ndio zinawaongezea faida.
 
Kama Mwananchi na Mtanzania riba inayotozwa na Mabenki hapa nchini kwa wananchi ni KUBWA SANA. Mfano hai mtu anapokopa anatakiwa kulipa riba ya 19% mpaka 22% wakati mwananchi huyo huyo akiweka fedha zake Benki anapewa riba ya 3%. Hapa hakuna usawa kabisa na kuonekana kuwa wananchi wananyonywa katika nchi yao. Tunaiomba Serikali yetu sikivu isimamie Mabenki nchini ili riba inayotolewa iwe rafiki kwa wananchi.
Nenda Islamic Banks
 
Riba za benki ni ukoma. Nishakopa benki mara mbili. Na sitakoma sababu nina shida na hela. First time nlikopa 9mil nikardisha kwa miaka 3 na riba ya 3.7 mil. Nikamaliza mkopo 2016 jun. July nikakopa tena 11 mill, saizz nakukuruka na makato kweny mshahara, nalipa riba ya 4+mil so benki ni majanga. Nikikopa tena baada ya miaka mitatu ndo utakuwa mkopo wangu wa mwisho kukopa kwa kukatwa mshahara. Maana nitachukua 15mil kwa ajili ya mtaji
 
Kama Mwananchi na Mtanzania riba inayotozwa na Mabenki hapa nchini kwa wananchi ni KUBWA SANA. Mfano hai mtu anapokopa anatakiwa kulipa riba ya 19% mpaka 22% wakati mwananchi huyo huyo akiweka fedha zake Benki anapewa riba ya 3%. Hapa hakuna usawa kabisa na kuonekana kuwa wananchi wananyonywa katika nchi yao. Tunaiomba Serikali yetu sikivu isimamie Mabenki nchini ili riba inayotolewa iwe rafiki kwa wananchi.
Tumeshaingia kwenye uchumi wa soko huria,usitegemee government intervation kwenye kila kitu.
Any way,Naomba ufahamu kwamba hizi riba benki hazijipangii tu,Bank kuu umeweka kiwango ch ajuu na cha chini kwa mabank kukopesha fedha,Sasa ukiona bank inakopesha kwa rate ya 22% au 23%,ujue kabisa wako within the limit hawajavuka limit iliyowekwa na bank kuu.Khusu hiyo 3% unayosema bank inalipa,ni sawa kutokana na aina ya acount uliyoweka fedha zako,Rate kama hizo mara nyingi huwa ni kwa ajili ya serving acounts,Sasa accoun hizi huwa bank zinalipa interest kutokana na minimum balance iliyo katika acoount yako katika mwezi huo.Sasa kwa akili ya kawaida bank haiwezi kukupa interest ya 20% wakati unaweza kuja na kutoa hela zako muda wowote.
Bank inatoa riba nzuri kwenye fixed deposit accounts,hadi sasa riba ni 12.5 hadi 13.5 inategemea na bank na demand waliyonayo kwa wakati ule.Riba za fixed deposit au investment accounts huwa zinatolewa kulingana na riba ya Treasury bills kwa wakati huo,mfano kwa sasa riba ni 12.5,kwa hiyo bank nyingi hutoa riba kuanzia 12.5% na kuendelea,Mfano inaweza kuwa TB+1.5=14% n.k..
Ukiweka pesa kwenye serving account usitegemee kutapa riba zaidi ya 7%.Hii pia BOT wameweka limit ili ku balance ushindani katika soko.
 
Kaha! Kama hawa airtel wanatoza riba ya kama 30% kwa wiki mbili. Je kwa mwezi si ndio wanatoza 60%! Hivi vimikopo vya TIMIZA ni unyonyaji wa aina yake!
 
Tukubaliane, duniani kote walimu ndiyo huleta mapinduzi ya kweli. Walimu wanabenki yao tena kwa mitaji yao wenyewe ni ngekuwa mwenye mamlaka, ningetamka riba ni 7% hadi labda 10% kwa mkopo. Kutokana na wingi wao, maana ndiyo wakopaji, kwa vyovyote vile benki nyingine zingeshusha tu! Wangekoswa wakopaji. Hivi mbona zipo Sacco's mkopo riba ni 3% MTU analamba 50m ,etc. Naishauri serikali walione hili, hizo riba ni wizi tu, zinasababisha mfumko wa bei tu! Benki hiyo ya walimu na Posta serikali ingezitumia kushusha riba hizo. serikali ikiamua fedha yetu inakuwa thamani, walimu maisha yanaboreka si mtaji wao. Miriba mikubwa ni vicious circle ya inflation. Serikali iweke fedha huko,kushusha mariba hayo.
 
Tukubaliane, duniani kote walimu ndiyo huleta mapinduzi ya kweli. Walimu wanabenki yao tena kwa mitaji yao wenyewe ni ngekuwa mwenye mamlaka, ningetamka riba ni 7% hadi labda 10% kwa mkopo. Kutokana na wingi wao, maana ndiyo wakopaji, kwa vyovyote vile benki nyingine zingeshusha tu! Wangekoswa wakopaji. Hivi mbona zipo Sacco's mkopo riba ni 3% MTU analamba 50m ,etc. Naishauri serikali walione hili, hizo riba ni wizi tu, zinasababisha mfumko wa bei tu! Benki hiyo ya walimu na Posta serikali ingezitumia kushusha riba hizo. serikali ikiamua fedha yetu inakuwa thamani, walimu maisha yanaboreka si mtaji wao. Miriba mikubwa ni vicious circle ya inflation. Serikali iweke fedha huko,kushusha mariba hayo.
Sidhani kwa Serikali yetu itaiweza hii vita, na hapo ndipo uelewe hata ma Landlords wanavyolalamika na kutoza kodi zao..Its a cycle, wananchi tumepiga kelele mpaka sauti zimekauka, wahusika viziwi, ila kama alivyosema Bujibuji, tulalamike hata kwenye mawasiliano TCRA Vodacom Tanzania @tigotanzania @airteltanzania..Tozo kwenye mawasiliano ni kubwa zaidi na ina wateja zaidi, kwanini hawawahurumii raia? Hapo ndipo tunakuna vichwa..
 
Kama Mwananchi na Mtanzania riba inayotozwa na Mabenki hapa nchini kwa wananchi ni KUBWA SANA. Mfano hai mtu anapokopa anatakiwa kulipa riba ya 19% mpaka 22% wakati mwananchi huyo huyo akiweka fedha zake Benki anapewa riba ya 3%. Hapa hakuna usawa kabisa na kuonekana kuwa wananchi wananyonywa katika nchi yao. Tunaiomba Serikali yetu sikivu isimamie Mabenki nchini ili riba inayotolewa iwe rafiki kwa wananchi.
Mbona hiyo riba ni ndogo, mimi nilichukua mkopo bank ya fnb kwa riba ya 23% baada ya miezi6 ikapandisha 2% zaidi ikawa asilimia 25 sasa ukiuliza wanakwambia sijui uendeshaji umekuwa juu, sasa kama yeye undeshaji umekuwa mbovu je mimi niliekopa kwao na huenda zilishaisha nazitoa wapi!?
 
Maisha yanatofautiaana masikini anaweka pesa bank. Tajiri anakwenda Bank anakopa pesa Anazungusha na kupata faida
 
Tatizo mnafikiri biashara ya benki ni kama kuendesha duka la mangi.Sasa ukitoa mikopo kwa asilimia 7,Je mteja utampa riba gani kwenye serving and time deposit accounts?.Maana lazima kuwe na spread btn give and take.Maana pesa unazokopesha ni pesa za watu na kila mwezi kuna cost of fund unalipa kwa wateja for holding their funds.Benki haiendeshwi na voluntary contributions kama saccos.
 
Mbona hiyo riba ni ndogo, mimi nilichukua mkopo bank ya fnb kwa riba ya 23% baada ya miezi6 ikapandisha 2% zaidi ikawa asilimia 25 sasa ukiuliza wanakwambia sijui uendeshaji umekuwa juu, sasa kama yeye undeshaji umekuwa mbovu je mimi niliekopa kwao na huenda zilishaisha nazitoa wapi!?
Kwenye mkataba wako na benki an sure kuna kipengele kinachsema"Rate is subject to change where necessary" Sijui kama huwa mnasoma hii mikataba/offer letter vizuri.
 
Nimesoma mawazo yenu na ninawashukuru lakini hata hivyo Mabenki bado wanawaibia Wananchi. Chukua mfano mtu anaweka fixed deposit anapewa 3% au 4% lakini huyo mtu akikopa Benki anatakiwa kulipa 23% tofauti ya 20%. Hata kama ni gharama za uendeshaji wa Benki hiyo tofauti ya asilimia ni kubwa sana. Ni vyema Serikali ikaingilia kati na kuwawekea Mabenki kiwango cha juu cha riba. Wananchi wanaumia sana na mikopo ya Mabenki.
 
Nimesoma mawazo yenu na ninawashukuru lakini hata hivyo Mabenki bado wanawaibia Wananchi. Chukua mfano mtu anaweka fixed deposit anapewa 3% au 4% lakini huyo mtu akikopa Benki anatakiwa kulipa 23% tofauti ya 20%. Hata kama ni gharama za uendeshaji wa Benki hiyo tofauti ya asilimia ni kubwa sana. Ni vyema Serikali ikaingilia kati na kuwawekea Mabenki kiwango cha juu cha riba. Wananchi wanaumia sana na mikopo ya Mabenki.
Kabisa kabisa, kama walivyofanya kwenye nyumba za kupangisha, wamekubali na watatii, hawa mabenki dawa ya inachemka, rate zao ziko juu mno mno..
 
Back
Top Bottom