Kila siku mambo muhimu ya kiserikali yanafanyika Dar es Salaam, lakini tumeambiwa na kutangaziwa kuwa serikali na bwana mkubwa Rais wamehamia rasmi Dodoma.
Mawaziri wanaapishiwa Dar
Mabalozi wanaapishiwa Dar
Mabalozi wa kigeni wanawasilisha hati zao za viapo Dar
Rais muda wote yupo Dar
Mkataba wa Barrick a.k.a Acacia na Serikali/Twiga umesainiwa Ikulu Dar
Makamu wa Rais muda wote yupo Dar
Jaji Mkuu na viongozi wa vyombo vya usalama muda wote wapo Dar
Waziri Zungu karipoti Dar kwa ofisi ya Makamu wa Rais
Waziri Jafo naye yupo Dar
Mimi naomba kueleweshwa Dodoma wamehamia kina nani? Ni serikali ipi imehamia Dodoma?
Kwa mifumo ya mawasiliano E Gov , ugatuzi madaraka, mbali ya Wabunge nani Mtanzania anahitaji kufika wizarani kwa lipi!?Tumepoteza pesa bure maamuzi Dom, hapakuwa na uhitaji as planned earlier.
Huwa nikisikia story za kitapeli za awamu hii nacheka vibaya sana. Na watu unawakuta ni wasomi wako macho makavu kabisa, wanasema ndoto ya Nyerere toka mwaka 73 imetekelezwa kuhamia Dodoma! Kichekesho anayesema hivyo yuko hapa Dar, na ukimuuliza mbona we uko hapa Dar, anasema unapinga kila kitu!
Kwa mifumo ya mawasiliano E Gov , ugatuzi madaraka, mbali ya Wabunge nani Mtanzania anahitaji kufika wizarani kwa lipi!?Tumepoteza pesa bure maamuzi Dom, hapakuwa na uhitaji as planned earlier.
Sisi ni waumini wa sera za mwalimu Nyerere,tutatekeleza kila alichopanga kufanya,kiwe na faida au kisiwe na faida, sasa naelewa why wazungu wanapenda kusafiri sana duniani,exposure ni darasa on its own
Kuweni na Subira, akishazindua rasmi hiyo Interchange ya Ubungo atarejea rasmi Makao Makuu ya Nchi. Najua hata wewe mleta uzi unajua wazi utamu wa ule upepo unaovuma kutoka bahari ya Hindi.