shikulaushinye
JF-Expert Member
- Aug 29, 2014
- 828
- 456
Kwa muda mrefu, elimu ya Tanzania imekuwa ikishuka hasa masomo ya sayansi na hisabati. Binafsi nina mtoto anayesoma shule chekechea ktk shule moja hapa Tanzania, huwa ninakaa na mtoto kuangalia maendeleo yake, siku moja katika kukagua daftari za mtoto.
Nilipigwa swali na mtoto, swali lenyewe lilikuwa nimtajie aina za insects, basi nikamtajia akanikumbusha kuwa nimesahau Snake na Frog, yaani nyoka na chura. Nikamwambia hao siyo insects, basi akakataa akanilitea kitabu kweli kitabu mtunzi kaandika snake yaani nyoka na chura wapo katika kundi la insects. ilikuwa kazi sana kumfanya aaache kuamini alichofundishwa na Mwalimu wake kupitia kitabu hiki.
Inashangaza sana hata walimu wana copy na paste bila kungalia kama kitabu kimeandikwa sahihi, hii ina maana hata uwezo wa walimu wetu ni mdogo na ndiyo chanzo cha kukosa wataalamu katika Sayansi na Hisabati.
Watanzania wenzangu, hii elimu huria ni tatizo. Serikali imeachia kila kitu, mbaya zaidi, serikali kupitia wizara wa Elimu na ufundi imekuwa ikitoa baraka kutumika vitabu hivi bila hata kuangalia madhara kwa jamii ya Watanzania.
Kwa lengo la kutoa ujembe na kuikumbusha serikali yetu, kuviangalia vitabu vinavyotumika mashuleni basi nimeweka baadhi ya kurasa za kitabu, mtunzi na jina. Pia nimefanya utafiti mdogo kitabu hiki kinatumiwa na shule nyingi za English medium hapa Tanzania. Hivyo watoto wengi wamemezeshwa sumu kupitia kitabu hiki.
Pili: wale wataalamu wa Elimu tunaomba mtusaidie hivi ni sahihi mtoto wa chekechea/KG umri wa miaka 4-5 kufundishwa mambo mazito kama haya wakati hata kusoma bado wanajifunza? Darasa la kwanza watasoma mambo gani iwapo kg wanasoma mambo kama haya?
Nilipigwa swali na mtoto, swali lenyewe lilikuwa nimtajie aina za insects, basi nikamtajia akanikumbusha kuwa nimesahau Snake na Frog, yaani nyoka na chura. Nikamwambia hao siyo insects, basi akakataa akanilitea kitabu kweli kitabu mtunzi kaandika snake yaani nyoka na chura wapo katika kundi la insects. ilikuwa kazi sana kumfanya aaache kuamini alichofundishwa na Mwalimu wake kupitia kitabu hiki.
Inashangaza sana hata walimu wana copy na paste bila kungalia kama kitabu kimeandikwa sahihi, hii ina maana hata uwezo wa walimu wetu ni mdogo na ndiyo chanzo cha kukosa wataalamu katika Sayansi na Hisabati.
Watanzania wenzangu, hii elimu huria ni tatizo. Serikali imeachia kila kitu, mbaya zaidi, serikali kupitia wizara wa Elimu na ufundi imekuwa ikitoa baraka kutumika vitabu hivi bila hata kuangalia madhara kwa jamii ya Watanzania.
Kwa lengo la kutoa ujembe na kuikumbusha serikali yetu, kuviangalia vitabu vinavyotumika mashuleni basi nimeweka baadhi ya kurasa za kitabu, mtunzi na jina. Pia nimefanya utafiti mdogo kitabu hiki kinatumiwa na shule nyingi za English medium hapa Tanzania. Hivyo watoto wengi wamemezeshwa sumu kupitia kitabu hiki.
Pili: wale wataalamu wa Elimu tunaomba mtusaidie hivi ni sahihi mtoto wa chekechea/KG umri wa miaka 4-5 kufundishwa mambo mazito kama haya wakati hata kusoma bado wanajifunza? Darasa la kwanza watasoma mambo gani iwapo kg wanasoma mambo kama haya?