Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Sisi wakazi wa Mivumoni, Madale na Wazo hili tulikuwa tunafurahia uzuri wa barabara zetu kuu zitokazo Wazohill kuelekea Mivumoni na Madale mpaka Mbezi, hizi ni barabara za vumbi lakini zilikuwa zinafanyiwa matengenezo ya kila mara karibu kila baada ya miezi mitatu. lakini baada ya uchaguzi uliofanyika Oct 2010 na CCM kupoteza jimbo hilo la Kawe na kuchukuliwa na Halima Mdee(CHADEMA) hiyo barabara haijaguswa hata siku moja, kwasasa imekuwa ni ngumu sana kupita hiyo barabara kwa gari ndogo. kumekuwa na maoni tofauti kuhusiana na ni kwanini hiyo barabara imesusiwa na serikali
1. Baadhi ya watu wanadai Serikali ilikuwa inaifanyia matengenezo ya mara kwa mara kwasababu Kawawa alikuwa bado hai.
2. Wengine wanadai Serikali ya CCM inalipiza kisasi kwa wananchi kwa kutokuichagua na hivyo kupelekea ushindi wa Halima Mdee.
Je inawezekana kweli serikali ilikuwa inakarabati barabara ikimuogopa Kawawa? au ni kweli Serikali inalipiza kisasi?
1. Baadhi ya watu wanadai Serikali ilikuwa inaifanyia matengenezo ya mara kwa mara kwasababu Kawawa alikuwa bado hai.
2. Wengine wanadai Serikali ya CCM inalipiza kisasi kwa wananchi kwa kutokuichagua na hivyo kupelekea ushindi wa Halima Mdee.
Je inawezekana kweli serikali ilikuwa inakarabati barabara ikimuogopa Kawawa? au ni kweli Serikali inalipiza kisasi?