Jenerali Ambamba
JF-Expert Member
- Sep 8, 2014
- 3,344
- 2,537
Serikali ya Tanzania inaishi kwa matumaini kwani haina fedha, kwa sasa inategemea makusanyo ya kodi ya mwezi kutoka TRA ambazo hazizidi milioni 900 kwa mwezi, ambapo katika hizo bado mishahara ya kila mwezi ya wafanyakazi wake, gharama za uendeshaji wa shughuli za siku kwa siku za serikali na kulipa madeni yake ya ndani na nje na kwa makandarasi wa miradi ya barabara.
Sasa serikali baada ya kukopa bank ya NMB na NBC kulipa mishahara ya wafanyakazi, kiwango cha kukopa kwake kilifika mwisho, mathalani bank ya NBC ambapo serikali ina hisa, kiwango chake kama mwanahisa cha kukopa kilifika mwisho hivyo ikazuiwa na mwanahisa mwenzake kutokukopa.
Hivyo taarifa zinasema Serikali imeingia makubaliano na bank ya Baclays ili kuweza kukopa kulipa mishahara ya kila mwezi kwa wafanyakazi wake.
Ndiyo maana kwa sasa bank nyingi hazikopeshi raia mmoja mmoja (mteja wa bank).
Sasa serikali baada ya kukopa bank ya NMB na NBC kulipa mishahara ya wafanyakazi, kiwango cha kukopa kwake kilifika mwisho, mathalani bank ya NBC ambapo serikali ina hisa, kiwango chake kama mwanahisa cha kukopa kilifika mwisho hivyo ikazuiwa na mwanahisa mwenzake kutokukopa.
Hivyo taarifa zinasema Serikali imeingia makubaliano na bank ya Baclays ili kuweza kukopa kulipa mishahara ya kila mwezi kwa wafanyakazi wake.
Ndiyo maana kwa sasa bank nyingi hazikopeshi raia mmoja mmoja (mteja wa bank).