Chikuvi2021
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 459
- 517
CAG kwenye ukaguzi wake kwa mwaka wa fedha 2020/2021 miongoni mwa mambo mengine, alitoa hoja ya ukaguzi wizara ya Ujenzi na Uchukuzi -Mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania ya kulipa fidia kwa wakazi wa Kipunguni A,Kipawa na Kigilagila waliofanyiwa uhakiki na tathamini miaka ya 1994-1997 -Lakini wakazi wa kipawa na kigilagila walipewa fidia mwaka 2011 kwa tathamini ya nyuma.
Serikali tayari imeshajenga terminal 3.Wananchi wa kipawa na kigilagila walipunjwa, lakini kwa uzalendo wao,,walipisha ujenzi wa terminal 3.
-, Serikali iliwazuia wananchi wa Kipunguni A kuendeleza au kufanyia matengenezo nyumba zao. -Kwenye hoja zake za Ukaguzi kwa mwaka 2020/2021 1. CAG kichere alipendekeza Serikali ilipe fidia kwa wakazi wa Kipunguni A kupisha upanuzi wa JNIA 2.CAG alipendekeza Serikali ilipe fidia (nyongeza ya 6%kwa kila) kwa wakazi wa kipawa na kigilagila ambao wamehamishiwa Kigogo Fresh,Zavala,Kinyamwezi na Nyeburu, lakini wengi wao wameshindwa kumalizia kujenga nyumba zao.
Kwa mujibu wa taarifa ya CAG madai hayo yaliongezeka kwa asilimia 301 (kipindi cha ukaguzi wake). 3. CAG aliagiza Serikali kupitia Mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania wakae na Mthamini Mkuu wa Serikali kupitia upya madai ya wananchi wa kipawa, kigilagila na Kipunguni A,na walipe fidia stahili, kuepusha kuongezeka kwa gharama.
Serikali ya awamu ya sita ya mama Samia,imefanya tathamini kwa nyumba za wakazi wa Kipunguni A na juzi ijumaa tarehe 6July 2023 Waziri wa fedha Dr Mwigulu Nchemba, Naibu Spika Na Mbunge wa Ilala Mh Mussa Hassan Zungu, Mh Bona Kamori Mbunge wa Segerea na viongozi wengine wa chama na Serikali walihudhuria kwenye mkutano wa Kipunguni A kutangaza kuwa zoezi la uhakiki na tathamini kwa wakazi wa Kipunguni A limekamilika na jumla ya bilioni 140 zitalipwa kwa wakazi wa Kipunguni A kuanzia Mwezi August 2023.
Serikali ya awamu ya sita ipewe maua, Lakini wananchi wa kipawa na kigilagila kigilagila ambao nyumba zao zilivunjwa kupisha ujenzi wa terminal 3 na wao walipwe asilimia 6 kama alivyo shauri CAG ili kufunga hoja ya ukaguzi. Ninawasilisha
Serikali tayari imeshajenga terminal 3.Wananchi wa kipawa na kigilagila walipunjwa, lakini kwa uzalendo wao,,walipisha ujenzi wa terminal 3.
-, Serikali iliwazuia wananchi wa Kipunguni A kuendeleza au kufanyia matengenezo nyumba zao. -Kwenye hoja zake za Ukaguzi kwa mwaka 2020/2021 1. CAG kichere alipendekeza Serikali ilipe fidia kwa wakazi wa Kipunguni A kupisha upanuzi wa JNIA 2.CAG alipendekeza Serikali ilipe fidia (nyongeza ya 6%kwa kila) kwa wakazi wa kipawa na kigilagila ambao wamehamishiwa Kigogo Fresh,Zavala,Kinyamwezi na Nyeburu, lakini wengi wao wameshindwa kumalizia kujenga nyumba zao.
Kwa mujibu wa taarifa ya CAG madai hayo yaliongezeka kwa asilimia 301 (kipindi cha ukaguzi wake). 3. CAG aliagiza Serikali kupitia Mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania wakae na Mthamini Mkuu wa Serikali kupitia upya madai ya wananchi wa kipawa, kigilagila na Kipunguni A,na walipe fidia stahili, kuepusha kuongezeka kwa gharama.
Serikali ya awamu ya sita ya mama Samia,imefanya tathamini kwa nyumba za wakazi wa Kipunguni A na juzi ijumaa tarehe 6July 2023 Waziri wa fedha Dr Mwigulu Nchemba, Naibu Spika Na Mbunge wa Ilala Mh Mussa Hassan Zungu, Mh Bona Kamori Mbunge wa Segerea na viongozi wengine wa chama na Serikali walihudhuria kwenye mkutano wa Kipunguni A kutangaza kuwa zoezi la uhakiki na tathamini kwa wakazi wa Kipunguni A limekamilika na jumla ya bilioni 140 zitalipwa kwa wakazi wa Kipunguni A kuanzia Mwezi August 2023.
Serikali ya awamu ya sita ipewe maua, Lakini wananchi wa kipawa na kigilagila kigilagila ambao nyumba zao zilivunjwa kupisha ujenzi wa terminal 3 na wao walipwe asilimia 6 kama alivyo shauri CAG ili kufunga hoja ya ukaguzi. Ninawasilisha