Serikali ikanushe uongo huu wa SABC kumsema vibaya Rais wetu Magufuli kuwa ni Dikteta!

Wanabodi,

Uzalendo ni kutokubali na kutonyamaza kimya wakati rais wako anaposemwa vibaya kwa hoja za uongo na media za nchi nyingine, bali ni kwa media zetu kujitokeza, kuukanusha uongo kwa kuusema ukweli na ikibidi serikali yetu sio tuu ikanushe bali pua ihitaji kuombwa radhi!.

Pamoja na matatizo yote na mapungufu yote ya rais wetu Magufuli, kwa sababu na yeye ni binadamu na sio malaika, Watanzania wote wazalendo wa kweli wa nchi yetu, tusikubali rais wetu kudhalilishwa kwa kusemwa vibaya, na kusingiziwa uongo na media za nje bila ya media za ndani kukanusha na kumtetea, au kuunyamazia udhalilishaji kama huu ni sawa na kushangilia rais wetu kudhalilishwa.

Hoja hii ni kufuatia makala hii
SABC News - Tanzania’s Magufuli descends from darling to despot:Sunday 9 April 2017

Kulikopelekea kuibuka kwa mjadala huu SABC NEWS: Magufuli kutoka rais apendwae mpaka kuwa dikteta!

Wito.
Natoa wito kwa Waziri wa Habari, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Idara ya Habari Maelezo kuukanusha uongo huu unaoenezwa kumhusu rais wetu, kwa sababu uongo ukisemwa sana na kuachwa bila kukanushwa mwishowe sio utaonekana kama ni ukweli, bali utageuka ukweli.

Jumatatu Njema.

Paskali.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Tension between Tanzania's 'bulldozer' president and opposition
Hakuna cha kukanusha, acha na dunia ijue tuko kwenye hali gani. Na tunajua utawala huu si wa kusikiliza wananchi wanahitaji nini. Sisi ndio tupo mtaani, tunajua mahitaji yetu, leo hii hao wamekaa kwenye viti vyao wanajifanya hawasikii sauti zetu, hawaoni maumivu yetu na bila shaka hawaumizwi na machozi yetu. walikuja kwa unyenyekevu na upole sana walipoomba kupewa nafasi kutawala. Wakae wakijua, kila wafanyalo tutalihesabu na hatutasahau.
NB dunia inaona...
 
Bashite kamsababishia yote haya, kiufupi uvamizi wa kituo cha habari halafu mtu asichukuliwe hatua yoyote kumekera vyombo vya habari na waandishi wa habari wengi sana duniani. Tegemeeni bad publicity throughout!!!
 
Pascal Myalla a.k.a pascal njaa.

Kwanza kabisa naomba utoe neno uzalendo kwenye bandiko lako ulitakiwa useme watanzania tunaopenda unafiki na maslahi binafsi na sio watanzania wazalendo.

Unachopendekeza hata wana habari wenzako wakiskia hawawezi kukusapoti kivyovyote sana sana watakuona mwehu tu kama huyo unaemtetea hapa.

Kimsingi watanzania wazalendo wanafurahi kuona Zisonje akianikwa hivi na vyombo vya habari vya nje hili ulimwengu ujue ni jinsi gani yeye ni kiongozi wa ovyo. Tena mimi nataka hao SABC wawe kila siku wanatoa habari zake ambazo sio rahisi kuchapishwa na magazeti ya hapa nyumbani, hatuwezi tukatetea uzandiki hata Mungu atazidi kutulaani.
 
Tutakanusha mangapi? Kwa maoni yangu wala hakuna haja kama wao wanaona hivyo so be it, lkn siyo kazi yetu kuwapangia jinsi wanavyotuona isitoshe unajua J.Zuma anaandikwa vipi na media za nje? Je unafikiri Serikali ya AK hupoteza muda wake kutaka maelezo ktk hizo media?
Kuna kitu kimeandikwa hapo ambacho ni cha uongo? Au hakikutokea? Tuacha unafiki!
 
Wanabodi,

Uzalendo ni kutokubali na kutonyamaza kimya wakati rais wako anaposemwa vibaya kwa hoja za uongo na media za nchi nyingine, bali ni kwa media zetu kujitokeza, kuukanusha uongo kwa kuusema ukweli na ikibidi serikali yetu sio tuu ikanushe bali pua ihitaji kuombwa radhi!.

Pamoja na matatizo yote na mapungufu yote ya rais wetu Magufuli, kwa sababu na yeye ni binadamu na sio malaika, Watanzania wote wazalendo wa kweli wa nchi yetu, tusikubali rais wetu kudhalilishwa kwa kusemwa vibaya, na kusingiziwa uongo na media za nje bila ya media za ndani kukanusha na kumtetea, au kuunyamazia udhalilishaji kama huu ni sawa na kushangilia rais wetu kudhalilishwa.

Hoja hii ni kufuatia makala hii
SABC News - Tanzania’s Magufuli descends from darling to despot:Sunday 9 April 2017

Kulikopelekea kuibuka kwa mjadala huu SABC NEWS: Magufuli kutoka rais apendwae mpaka kuwa dikteta!

Wito.
Natoa wito kwa Waziri wa Habari, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Idara ya Habari Maelezo kuukanusha uongo huu unaoenezwa kumhusu rais wetu, kwa sababu uongo ukisemwa sana na kuachwa bila kukanushwa mwishowe sio utaonekana kama ni ukweli, bali utageuka ukweli.

Jumatatu Njema.

Paskali.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Tension between Tanzania's 'bulldozer' president and opposition
Likiongea shirika la habari la nchi,kama lilivyofanya shirika hili la afrika kusini,ni sawa na Afrika kusini kutoa angalizo kwa dunia nzima na afrika kuhusu hali ya Tanzania,shirika la habari la nchi ni mdomo wa nchi na huwakilisha maoni ya nchi kuhusu mambo mbalimbali duniani.

Mimi nauchukua msimamo huu kuwa ni msimamo kamili wa Afrika kusini.

Tuliwakomboa,sasa wao wanatukomboa
 
Wanabodi,

Uzalendo ni kutokubali na kutonyamaza kimya wakati rais wako anaposemwa vibaya kwa hoja za uongo na media za nchi nyingine, bali ni kwa media zetu kujitokeza, kuukanusha uongo kwa kuusema ukweli na ikibidi serikali yetu sio tuu ikanushe bali pua ihitaji kuombwa radhi!.

Pamoja na matatizo yote na mapungufu yote ya rais wetu Magufuli, kwa sababu na yeye ni binadamu na sio malaika, Watanzania wote wazalendo wa kweli wa nchi yetu, tusikubali rais wetu kudhalilishwa kwa kusemwa vibaya, na kusingiziwa uongo na media za nje bila ya media za ndani kukanusha na kumtetea, au kuunyamazia udhalilishaji kama huu ni sawa na kushangilia rais wetu kudhalilishwa.

Hoja hii ni kufuatia makala hii
SABC News - Tanzania’s Magufuli descends from darling to despot:Sunday 9 April 2017

Kulikopelekea kuibuka kwa mjadala huu SABC NEWS: Magufuli kutoka rais apendwae mpaka kuwa dikteta!

Wito.
Natoa wito kwa Waziri wa Habari, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Idara ya Habari Maelezo kuukanusha uongo huu unaoenezwa kumhusu rais wetu, kwa sababu uongo ukisemwa sana na kuachwa bila kukanushwa mwishowe sio utaonekana kama ni ukweli, bali utageuka ukweli.

Jumatatu Njema.

Paskali.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Tension between Tanzania's 'bulldozer' president and opposition


Ha ha haaa... We jamaa mjanja Sana.. Unarusha jiwe kisha unakaa pembeni... Inahitaji akili kubwa kukuelewa..
 
wewe mbona hujakanusha kwa kuweka fact?? Unatikisa ili ujumuishwe serikalini eeh! Njia unayotumia ishashtukiwa,kukosoa ili upewe cheo Kisha ubadilike ghafla kama kina polipoli na yule mshauri wa Act. Kwakuwa u msukuma penginepo utapata kakitu... Kukosolewa vyakweli si dhambi ila bahati na kutakiwa mema mbeleni
Pasco kabadilika sana siku hizi.
 
Back
Top Bottom